-
Azimio la UN: Israel iachane na silaha za nyuklia, ijiunge na NPT
Dec 08, 2022 23:10Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limeunga mkono kwa wingi mkubwa mno wa kura azimio la kuutaka utawala haramu wa Kizayuni wa Israel uachane na silaha zake za nyuklia na kujiunga na Mkataba wa Kuzuia Uundaji na Uenezaji Silaha za Nyuklia (NPT).
-
Israel yaendelea kumwaga damu za Wapalestina Jenin
Dec 08, 2022 07:21Jeshi katili la utawala haramu wa Israel limewaua shahidi vijana watatu wa Kipalestina katika mji wa Jenin, kaskazini mwa Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Hizbullah yaipongeza timu ya soka ya Morocco kwa kuinyuka Uhispania na kuinua bendera ya Palestina
Dec 07, 2022 10:22Naibu Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon, Sheikh Naim Qassem ametuma ujumbe kwenye mtandao wa kijamii wa "Twitter" ambapo ameipongeza Morocco kwa ushindi wa timu ya kandanda ya nchi hiyo dhidi ya Uhispania hiyo jana na kufuzu kuingia robo fainali ya mechi za Kombe la Dunia zinazoendelea nchini Qatar.
-
Al Jazeera yawasilisha mashtaka ya mauaji Shireen kwenye mahakama ya kimataifa ya ICC
Dec 06, 2022 23:43Mtandao wa Habari wa Al -Jazeera umetangaza kuwa umewasilisha kesi ya mauaji ya mfanyakazi wake, Shireen Abu Akleh, katika Mahakama ya Jinai ya Kimataifa huko Hague.
-
Kuwait kujinaisha kuanzishwa uhusiano wa kawaida na Israel
Dec 04, 2022 04:22Bunge la Kuwait kwa mara nyingine limechukua hatua inayoashiria msimamo usiotetereka wa nchi hiyo kuhusiana na Palestina, na sasa linaandaa mpango wa kisheria wa kufanya kuwa jinai mpango wowote wa kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel.
-
UN yaunga mkono kutambuliwa Siku ya Nakba ya Wapalestina
Dec 01, 2022 09:46Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepiga kura ya kuunga mkono azimio lenye maslahi kwa Palestina la kutaka kuadhimishwa Siku ya Nakba, inayokumbusha tukio chungu la kuasisiwa utawala bandia na haramu wa Israel mwaka 1948.
-
Kanali ya Kizayuni: Israel inakabiliwa na Intifadha mpya ya Wapalestina
Nov 30, 2022 07:15Chombo kimoja cha habari cha Kizayuni kimesema hali ya usalama katika eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan linalokaliwa kwa mabavu ni ya 'hatari' na kwamba Tel Aviv inakabiliwa na Intifadha mpya ya Wapalestina.
-
Uingereza yasisitiza haitauhamishia ubalozi wake Quds
Nov 22, 2022 04:06Kwa mara nyingine, Uingereza kutokana na mashinikizio na ukosoaji wa ndani na nje ya nchi, imesisitiza kuwa haina mpango wa kuuhamishia ubalozi wake katika mji wa Quds tukufu, huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
Kombe la Dunia; Vijana wa Kiarabu wakataa kuzungumza na wanahabari wa Israel
Nov 21, 2022 07:55Mashabiki wa soka wa nchi za Kiarabu wamekataa kuzungumza na waandishi wa habari wa mashirika ya utawala haramu wa Israel nchini Qatar, kunakofanyika fainali za Kombe la Dunia za mwaka huu 2022; kuonyesha upinzani wao wa kuanzishwa uhusiano wa kawaida na utawala huo bandia unaokalia kwa mabavu ardhi za Palestina.
-
Israel yatumia bunduki za roboti dhidi ya Wapalestina Ukingo wa Magharibi
Nov 17, 2022 03:25Jeshi la utawala haramu wa Israel limepeleka silaha mpya za roboti katika eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, huku makabiliano baina ya Wazayuni na Wapalestina yakipamba moto.