-
Iran, Mhimili wa Muqawama zalaani ushadidishaji 'hatari' wa mashambulio ya Israel ndani ya Lebanon
Nov 07, 2025 08:06Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani wimbi jipya la uchokozi wa kijeshi unaozidi kufanywa na utawala wa kizayuni wa Israel dhidi ya Lebanon, na kuikumbusha jamii ya kimataifa na nchi za kikanda kuhusu wajibu wao wa kukabiliana na uchochezi wa vita wa Tel Aviv, kwa kuuwajibisha na kuuadhibu utawala huo ghasibu.
-
UN: Israel imekataa maombi zaidi ya 100 ya kuingiza misaada Ghaza tangu vita viliposimamishwa
Nov 07, 2025 06:47Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, tangu yalipoanza kutekelezwa makubaliano ya kusitisha vita tarehe 10 Oktoba, utawala wa kizayuni wa Israel umekataa maombi 107 ya kuingizwa vifaa vya misaada katika Ukanda wa Ghaza, na hivyo kuzuia vifaa muhimu vya kibinadamu kuwafikia Wapalestina wa eneo hilo wanaoishi katika mazingira magumu na ya mateso.
-
El Fasher, Hadithi ya Kuanguka Mji
Nov 07, 2025 13:02El Fasher sio jina la mji tu; bali ni jeraha lililowazi la dhamiri ya dunia. Katika kipindi chetu leo, tunasimulia mzingiro uliozuia mkate wa watu, na hujuma iliokata pumzi za watoto. Ni simulizi fupi lakini sahihi, inayotuhimiza sisi sote kuelekeza mazingatio yetu kwa maafa ya binadamu yanayotokea huko Sudan....
-
Ripoti ya kushtusha ya Umoja wa Mataifa; mauaji ya kimbari ya Wapalestina Ghaza yangali yanaendelea
Nov 06, 2025 23:17Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, mauaji ya kimbari ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza yangali yanaendelea.
-
Hizbullah: Mazungumzo na adui hayana maslahi na taifa
Nov 06, 2025 07:14Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon imesitiza kuwa kufanya mazungumzo na adui si kwa maslahi yoyote ya kitaifa, na kubainisha kuwa baadhi walijaribu kukabidhi silaha za muqawama dhidi ya adui kama ushahidi wa nia njema ya Lebanon.
-
Tehran yasema 'vita halisi vya kikanda' na Israel vinaendelea, yapuuza mazungumzo na Marekani
Nov 04, 2025 08:07Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Iran amesema kwamba eneo la Magharibi mwa Asia kwa sasa limo katika na "vita halisi" na utawala wa Israel, akisisitiza kwamba hali ya eneo hilo iimekwenda mbali zaidi ya vitisho tu.
-
Nyaraka za jeshi la Israel zafichua: Mfungwa wa Kipalestina aliyebakwa alikuwa raia, si mpiganaji
Nov 04, 2025 07:48Waraka wa siri wa jeshi la Israel umefichua kwamba mtu aliyeshambuliwa kikatili na kubakwa na kundi la wanajeshi wa Israel katika gereza maarufu la Sde Teiman mnamo Julai mwaka jana hajawahi kushtakiwa kwa uhalifu wowote na alikuwa raia, kinyume na madai kwamba alikuwa na mwanachama harakati za mapambano ya Hamas.
-
Israel yaandaa muswada wa 'kifashisti' wa kuruhusu utoaji wa hukumu ya adhabu ya kifo kwa Wapalestina
Nov 03, 2025 22:55Kamati moja ya wabunge wa utawala wa kizayuni wa Israel imeidhinisha muswada wa kuanzisha utoaji wa adhabu ya kifo kwa Wapalestina wanaoshikiliwa kwenye magereza ya utawala huo, na kufungua njia ya kusomwa hoja hiyo kwa mara ya kwanza bungeni licha ya kuandamwa na lawama nyingi.
-
Israel yaendelea kuwatesa kwa njaa Wapalestina kwa kuruhusu 24% tu ya misaada kuingizwa Ghaza
Nov 02, 2025 03:20Mamlaka za Palestina katika Ukanda wa Ghaza zimetangaza kuwa utawala wa kizayuni wa Israel umeruhusu kuingizwa katika eneo hilo sehemu ndogo tu ya misaada ya kibinadamu kinyume na ilivyoafikiwa katika makubaliano ya usitishaji mapigano yanayosimamiwa na serikali ya Marekani, ambayo yalianza kutekelezwa mwezi uliopita.
-
Israel yaendelea kukiuka makubaliano na Lebanon, yashambulia na kuua watu 4 na kujeruhi 3
Nov 02, 2025 02:57Shambulio la anga lililofanywa na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel limesababisha vifo vya watu wanne na kuwajeruhi wengine watatu kusini mwa Lebanon ukiwa ni mwendelezo wa mashambulizi ya kigaidi yanayofanywa na Tel Aviv ndani ya ardhi ya nchi hiyo, ambayo yanakiuka makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyofikiwa mwishoni mwa Novemba 2024 kati ya Harakati ya Muqawama ya Hizbullah na utawala huo ghasibu.