-
Jeshi katili la Israel laendelea kumwaga damu za Wapalestina Gaza
Mar 24, 2025 23:21Wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamewaua shahidi Wapalestina wengine 17 katika mashambulizi ya alfajiri ya leo katika Ukanda wa Gaza, siku moja baada ya kuua shahidi Wapalestina zaidi ya 60 akiwemo ripota wa Al Jazeera, Hossam Shabat katika ukanda huo.
-
Tunisia yajitoa kwenye Mahakama ya Haki za Binadamu na Watu ya Umoja wa Afrika
Mar 23, 2025 23:01Tunisia imetangaza kujitoa katika Mahakama ya Haki za Binadamu na Watu ya Umoja wa Afrika (AfCHPR), jambo linaloashiria kupuuza serikali ya Tunis masuala ya haki na kesi zinazoendeshwa katika nchi hiyo ya Kaskazini mwa Afrika.
-
Hamas: Mauaji ya Wapalestina akiwemo Mbunge yataimarisha Muqawama
Mar 23, 2025 07:29Jeshi la Israel limefanya mashambulizi mapya ya kutisha ya anga katika Ukanda wa Gaza na kuua shahidi watu wasiopungua 40, akiwemo Salah al-Bardawil, Mbunge wa Palestina na Mjumbe wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas.
-
Israel yapigwa na makombora kutoka Yemen, ving'ora vyahanikiza
Mar 23, 2025 07:21Vikosi vya Ulinzi vya Yemen vimevurumisha makombora kuelekea katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Israel, na kuwatia kiwewe na hofu Wazayuni; huku safari za ndege zikisimamishwa Tel Aviv.
-
UN, EU zataka kusitishwa vita Gaza huku Israel ikifanya mashambulizi mapya
Mar 22, 2025 01:02Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya zimetoa wito wa kusitishwa mara moja mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel huko Gaza, huku Israel ikianzisha tena vita vya mauaji ya kimbari kwenye ukanda huo.
-
Israel yaua watu wengine 71 katika mashambulizi dhidi ya Gaza na kuikalia tena Netzarim
Mar 20, 2025 06:56Ripoti zinaonyesha kuwa ndani ya saa 24 zilizopita wanajeshi wa Israel wamewaua shahidi Wapalestina zaidi ya 71 katika miji ya Beit Lahiya, Rafah na Khan Yunis, huku wengine wengi wakijeruhiwa.
-
Moto mpya wa vita wawashwa na utawala wa Kizayuni huko Gaza kwa msaada wa Marekani
Mar 20, 2025 06:22Kwa kukiuka makubaliano ya usitishaji vita huko Ghaza yaliyoanza kutekelezwa tarehe 19 Januari, utawala wa Kizayuni umeanzisha tena vita vya umwagaji damu dhidi ya eneo hilo lililoharibiwa na vita, kwa kufanya mashambulizi makubwa ya kinyama ambayo yamesababisha mauaji ya mamia ya mashahidi wa Kipalestina na kujeruhi wengine wengi katika ukanda huo.
-
Netanyahu: Mashambulio yalioua watoto 174 Gaza ni mwanzo tu
Mar 19, 2025 23:40Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu ametangaza kushadidi mashambulio mabaya dhidi ya Gaza, akionya kwamba mashambulizi ya hivi karibuni ya anga, ambayo yaliua watoto wasiopungua 174 katika ukanda huo, ni mwanzo tu wa uchokozi mkubwa zaidi dhidi ya Wapalestina.
-
"Chuki dhidi ya Uislamu ni chombo cha kuhalalisha jinai za Israel"
Mar 15, 2025 03:36Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amelaani mwenendo unaoongezeka wa kueneza chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu duniani na kusema kuwa, chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) ni nyenzo ya kuhalalisha uvamizi na jinai za utawala wa Kizayuni.
-
Wataalamu wa UN waituhumu Israel kwa udhalilishaji wa kingono dhidi ya Wapalestina
Mar 14, 2025 11:28Wataalamu wa Umoja wa Mataifa wameituhumu Israel kuwa imewadhalilisha kingono na kijinsia Wapalestina wakati wa vita na mauaji ya kimbari ya utawala huo dhidi ya wakazi wa Gaza.