Jarida la kila wiki la Newsweek la nchini Marekani limeandika kuwa, uanachama wa kudumu wa Iran katika Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai utazidi kuibana Magharibi katika kukabiliana na mradi wa nyuklia wa Iran.
Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Tehran ni mshirika huru na wa kuaminika na iko tayari kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kieneo na kimataifa.