-
Vikosi vya Haftar vyafanya hujuma ya kukata umeme katika mji mkuu wa Libya, Tripoli
Apr 10, 2020 23:45Vikosi vya kundi linalojiita Jeshi la Taifa la Libya (LNA) linaloongozwa na jenerali muasi Khalifa Haftar vimefanya hujuma ya kusababisha umeme kukatika katika baadhi ya maeneo ya mji mkuu wa Libya, Tripoli.
-
Vikosi vya Haftar vyadai vimetungua drone 2 za Uturuki huko Libya
Apr 09, 2020 03:51Kundi la wanamgambo wanaojiita Jeshi la Tifa la Libya wanaoongozwa na jenerali Khalifa Haftar linadai kuwa limetungua ndege mbili zisizo na rubani za Uturuki zilizokuwa zikiruka katika anga ya nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
UN yalaani shambulio la wanamgambo wa Haftar dhidi ya hospitali ya wagonjwa wa Corona Libya
Apr 08, 2020 08:40Umoja wa Mataifa umelaani vikali shambulio lililofanywa na wanamgambo watiifu kwa jenerali muasi nchini Libya Khalifa Haftar dhidi ya hospitali ya kulazwa wagonjwa wa virusi vya Corona kusini mwa mji mkuu wan chi hiyo Tripoli.
-
Vikosi vya serikali ya Libya vyaripua ndege yenye shehena ya silaha ya kundi la Khalifa Haftar
Apr 06, 2020 03:14Vikosi vya Serikali ya Maafikiano ya Kitaifa ya Libya (GNA) vimeiteketeza ndege moja iliyokuwa imebeba shehena ya silaha na zana za kijeshi kwa ajili ya kundi linalojiita Jeshi la Taifa la Libya (LNA) linaloongozwa na Khalifa Haftar.
-
UN yataka kusitishwa vita haraka nchini Libya na kutiliwa maanani virusi vya corona
Apr 05, 2020 06:18Ofisi ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Libya imetoa wito wa kusitishwa mapigano mara moja na kusitishwa vita nchini humo kwa ajili ya kukabiliana na maambukizi ya virusi vya corona.
-
Baada ya kushindwa kutatua mgogoro wa Libya, Arab League yasema inasikitishwa na mapigano wakati huu wa kushughulikia corona
Apr 04, 2020 22:22Baada ya Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) kushindwa kutatua mgogoro wa Libya na kukomesha mapigano katika nchi hiyo ya Kiarabu ya kaskazini mwa Afrika, Katibu Mkuu wa jumuiya hiyo ameishia kusema anasikitishwa na vita vinavyoendelea huko Libya badala ya kuelekezwa nguvu katika kupambana na ugonjwa wa COVID-19.
-
Uingiliaji wa moja kwa moja wa Uturuki katika masuala ya ndani ya Libya
Apr 03, 2020 06:20Licha ya matamshi ya hivi karibuni ya Rais Recep Tayyip Erdogan ya kutangaza kukomeshwa vita vyote vya nchi hiyo katika eneo hili na duniani kiujumla kutokana na wimbi la kuenea kirusi cha corona, lakini kuna taarifa mpya zinazosema kuwa jeshi la Uturuki linaingilia moja kwa moja masuala ya ndani ya Libya.
-
Kuanza operesheni ya "Dhoruba ya Amani" ya vikosi vya Serikali ya Maafikiano ya Kitaifa ya Libya dhidi ya wapiganaji wa Haftar
Mar 26, 2020 22:04Licha ya mgogoro wa virusi vya Corona na takwa la jamii ya kimataifa la kusimamishwa vita katika mataifa yenye mapigano na machafuko, lakini vikosi vya Serikali ya Maafikiano ya Kitaifa ya Libya vimeanzisha operesheni mpya iliyopewa jina la "Dhoruba ya Amani" dhidi ya wapiganaji wa kundi linalojiita Jeshi la Taifa la Libya (LNA) linaloongozwa na jenerali muasi Khalifa Haftar.
-
Vikosi vya GNA Libya vyaanzisha operesheni ya "Dhoruba ya Amani" dhidi ya wapiganaji wa Haftar
Mar 26, 2020 03:34Vikosi vya jeshi la Serikali ya Maafikiano ya Kitaifa ya Libya (GNA) vimetangaza kuwa vimeanzisha operesheni iliyopewa jina la "Dhoruba ya Amani" dhidi ya wapiganaji wa kundi linalojiita Jeshi la Taifa la Libya (LNA) linaloongozwa na Khalifa Haftar.
-
Kukaribisha Umoja wa Mataifa makubaliano ya usitishaji vita katika vita vya ndani nchini Libya
Mar 24, 2020 09:00Vita vya ndani nchini Livya viliibua wasiwasi mkubwa kufuatia mashambulio ya mara kwa mara ya Jeshi la Taifa la Libya linaloongozwa na jenerali Khalifa Haftar yaliyoanza Aprili mwaka jana kwa shabaha ya kuiangusha Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa.