Jumuiya ya Waislamu wa Marekani imetangaza kuwa, rais wa nchi hhiyo Joe Biden atakuwa msaliti kama atasaini msaada mpya wa kijeshi kwa utawala wa Kizayuni unaoua kwa umati watoto wadogo huko Ghaza na atakuwa amevuruga kabisa uhusiano wake na Waislamu.
Idara ya Mahakama ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeitoza Marekani faini ya dola bilioni moja kwa kuunga mkono jinai za utawala wa Kipahlavi uliokuwa madarakani Iran kabla ya Mapinduzi ya Kiislamu ya mwaka 1979.
Marekani ambayo ni muungaji mkono mkuu wa Israel kwa mara nyingine imetumia kura ya turufu (Veto) na kuzuia kupasishwa uanachama kamili wa Palestina ndani ya Umoja wa Mataifa.
Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imelaani hatua ya Marekani ya kuzuia ombi la Palestina la kutaka uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa, huku Israel ikiendeleza mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza kwa msaada wa baadhi ya nchi za Magharibi hususan Marekani.
Marekani, ambayo ni muungaji mkono mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, imeendeleza sera yake ya kudhoofisha kupatikana haki za Wapalestina kwa kutumia vibaya haki yake ya kura ya turufu na kukwamisha azimio la kuipatia Palestina uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa.
Patrick Ryder Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) amekiri juu ya nguvu za kijeshi za Iran katika kutoa jibu la kijeshi kwa utawala wa Israel.
Marekani inazishinikiza kwa siri nchi wanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kukataa ombi la Palestina kuwa mwanachama kamili wa taasisi hiyo kuu ya kimataifa.
Rais wa Marekani kwa mara nyingine tena, katika uingiliaji wa wazi na kuunga mkono utawala wa Israel, ameiomba Jamhuri ya Kiislamu ya Iran isijibu mashambulizi ya utawala huo kwenye ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus huko Syria.
Kiongozi Muadhamu wa wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei anasema utawala wa Kizayuni wa Israel "lazima uadhibiwe na kutiwa adabu" kwa shambulio lake baya dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran katika mji mkuu wa Syria, Damascus.
Waziri wa Ulinzi wakati wa utawala wa Barack Obama Rais mstaafu wa Marekani amesema kuwa haishangazi kwamba Waisraeli wamekiri makosa yao baada ya shambulio la hivi karibuni na mauaji dhidi ya watoa misaada wa kimataifa wa shirika la World Central Kitchen (WCK), kwa sababu kwa kawaida wao kwanza hupiga risasi na kisha huuliza maswali!