-
Korea Kaskazini yaipa Marekani muhula na kuitaka ibadili mienendo
Apr 14, 2019 02:54Kim Jong-un, Kiongozi wa Korea Kaskazini ameonya kuwa, mazungumzo mengine kati yake na Rais Donald Trump wa Marekani yatafanyika tu iwapo Washington itabadilisha mienendo na misimamo yake.
-
Wayemen wasusia 'New York Post' kwa kumshambulia mbunge Muislamu wa US
Apr 14, 2019 02:53Muungano wa wafanyabiashara unaojumuisha wauza magazeti raia wa Yemen wanaoishi nchini Marekani umetangaza kuwa hautauza wala kununua tena gazeti la New York Post, baada ya gazeti hilo kumshambulia Mbunge Muislamu katika Baraza la Wawakilishi la Marekani, Ilhan Omar.
-
Marekani yasema huenda ikalazimika kubakia Somalia baada ya 2026
Apr 13, 2019 22:36Marekani imedai kuwa inatazamia kukamilisha operesheni zake nchini Somalia ndani ya miaka saba ijayo, lakini iwapo italazimu, vikosi vyake vitasalia nchini humo kwa muda zaidi.
-
Trump aionya ICC dhidi ya kuchunguza jinai za kivita za Marekani na Israel
Apr 13, 2019 03:35Rais Donald Trump ameionya vikali Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) dhidi ya kuchunguza jinai za kivita za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
China na Umoja wa Ulaya zatangaza tena kuunga mkono mapatano ya nyuklia ya JCPOA
Apr 12, 2019 10:49Mapatano ya kimataifa ya nyuklia ya Iran maarufu kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezwaji (JCPOA) yanahesabiwa kuwa mapatano muhimu sana katika fremu ya usalama na amani ya kimataifa. Lakini pamoja na hayo, mnamo Mei 8 mwaka 2018, Marekani ilichukua uamuzi wa pande moja na kujiondoa katika mapatano hayo.
-
Ayatullah Kermani: Marekani ni mama wa ugaidi, Trump ni mpumbavu kwa kuinasibisha IRGC na ugaidi
Apr 12, 2019 10:48Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyoswaliwa leo hapa mjini Tehran amesema kuwa, hatua ya Washington ya kuliweka Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran IRGC katika orodha yake ya makundi ya kigaidi ni ya kipumbavu na kwamba Marekani ndiye mama wa ugaidi duniani.
-
Upinzani: Uingereza haipaswi kumkabidhi Julian Asange kwa Marekani
Apr 12, 2019 10:27Kiongozi wa chama Leba nchini Uingereza amekosoa vikali kitendo cha kutiwa mbaroni mjini London mwasisi wa mtandao unaojishughulisha na kufichua siri na kashfa wa WikiLeaks, Julian Assange.
-
Maandamano yashuhudiwa London baada ya kukamatwa mwasisi wa Wikileaks
Apr 11, 2019 23:59Maandamano yameshuhudiwa nje ya ubalozi wa Ecuador mjini London baada ya polisi ya Uingereza kumtia mbaroni mwasisi wa mtandao unaofichua fedheha nyingi za nchi na viongozi mbalimbali duniani wa WikiLeaks, Julian Assange, ambaye amekuwa akiishi ubalozini hapo tokea mwaka 2012.
-
Rais wa Lebanon: Tangazo la Trump kuhusu miinuko ya Golan na Quds ni kinyume na maazimo ya kimataifa
Apr 11, 2019 23:55Rais Michel Aoun wa Lebanon kwa mara nyingine tena amesisitiza kuwa, tangazo la Rais Donald Trump wa Marekani kuhusiana na umiliki wa utawala vamizi wa Israel kwa miinuko ya Golan ya Syria linakinzana na maazimio ya kimataifa.
-
Nasrullah: Hatua ya US dhidi ya IRGC ni thibitisho kuwa Washington imefeli katika eneo
Apr 11, 2019 09:26Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Lebanon (Hizbullah) sambamba na kulaani hatua ya Rais Donald Trump ya kuliweka Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC katika orodha ya Marekani ya makundi ya kigaidi amesisitiza kuwa, kitendo hicho ni ithibati tosha kuwa Washington imefeli katika njama zake ghalati katika eneo la Asia Magharibi.