Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limetangaza kuwa, wafungwa 130 wa Misri wanafanya mgomo wa kula katika mojawapo ya jela za nchi hiyo.
Rahaf al Qanun binti wa miaka 18 wa Saudi Arabia hatimaye amefanikiwa kupata hifadhi nchini Canada baada ya kutoroka nchini mwake kwa tabu sana.
Wananchi wa Bahrain jana usiku walifanya maandamano makubwa katika maeneo mbalimbali nchini humo lengo likiwa ni kuwaunga mkono na kuonyesha mshikamano wao kwa maulamaa na wanazuoni wa kidini wanaoshikiliwa kwenye jela za utawala wa Aal Khalifa.
Afisa mmoja wa utawala wa Aal Saud amesema Mut'ib bin Abdullah, mkuu wa zamani wa gadi ya taifa ambaye alikuwa amewekwa kizuizini, ameachiwa huru baada ya kutoa kikomboleo cha dola bilioni moja.
Mkuu wa Shirika la Amani kwa Ajili ya Demokrasia na Haki za Binadamu nchini Bahrain amesema raia 15,000 wametiwa nguvuni nchini humo katika kipindi cha miaka saba iliyopita.
Watu wasiopungua 11 wameuawa huku wafungwa 930 wakitoroka jela wakati watu wenye silaha wasiojulikana walipovamia jela moja iliyoko kwenye mji wa Beni, kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Ripoti mpya iliyotolewa hivi karibuni inaonyesha kuwa idadi ya wafungwa wanaoshikiliwa katika jela za Marekani ni kubwa zaidi kuliko ya nchi zote duniani na hivi sasa kuna karibu wafungwa milioni mbili na laki tatu katika jela za nchi hiyo.
Matukio yanayojiri nchini Bahrain yanaonyesha kuwa utawala wa Aal Khalifa unazidisha hatua za ukandamizaji dhidi ya wananchi kiasi kwamba kuwatia nguvuni na kuwafungulia kesi wanaharakati wa kisiasa kunazidi kuchukua sura pana zaidi inayozidi kutia wasiwasi siku baada ya siku.