Jan 23, 2024 05:34
Misri imeuonya utawala wa Kizayuni wa Israel kwamba jaribio lolote la kuikalia kwa mabavu sehemu ya ardhi inayotenganisha eneo la Wapalestina lililozingirwa la Ukanda wa Gaza na Misri, linalojulikana kama Korido ya Philadelphi, litakuwa ni "tishio kubwa" kwa uhusiano kati ya pande hizo mbili.