-
Ikhwanul Muslimin wakanusha kufanya mazungumzo ya siri na serikali ya Misri
Jul 07, 2018 00:09Msemaji wa harakati ya Ikhwanul Muslimin ya Misri amekanusha habari ya kufanyika mazungumzo ya siri baina ya harakati hiyo kubwa zaidi ya kisiasa ya upinzani na serikali ya nchi hiyo.
-
Misri: Migogoro ya kieneo haiwezi kupatiwa ufumbuzi kwa mtutu wa bunduki
Jul 05, 2018 03:03Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Misri amesema kuwa, nchi yake inafanya juhudi kubwa katika mwenendo wa kupatiwa ufumbuzi migogoro wa Syria na Libya na kusisitiza kwamba, migogoro inayoshuhudiwa hivi sasa katika eneo la Mashariki ya Kati na kaskazini mwa Afrika ufumbuzi wake sio mtutu wa bunduki.
-
Ikwanul Muslimin yapinga hatua ya al Sisi ya kuwapa kinga makamanda wa jeshi la Misri
Jul 04, 2018 08:42Msemaji wa harakati ya Ikhwanul Muslimin nchini Misri amekosoa hatua ya serikali ya Jenerali Abdul Fattah al Sisi ya kuimarisha nafasi ya wanajeshi nchini humo na mwafaka wa Bunge wa kuwapa kinga ya sheria makamanda wa jeshi la nchi hiyo.
-
Mashirika ya kutetea haki za binadamu yaitaka Ufaransa iache kuiuzia silaha Misri
Jul 02, 2018 03:13Mashirika kadhaa ya kutetea haki za binadamu yameitaka serikali ya Ufaransa kusimamisha uuzaji wa silaha kwa Misri, yakisisitiza kuwa silaha hizo zinatumiwa na vyombo vya usalama kuwanyamazisha na kuwawekea mbinyo wapinzani na wakosoaji wa serikali.
-
Makahama ya Misri yaakhirisha hukumu ya watuhumiwa wa Medani ya Rabia
Jun 30, 2018 11:46Mahakama ya Jinai ya Cairo leo Jumamosi imeamua kuakhirisha hukumu ya mwisho dhidi ya watu 739 walioshiriki katika maandamano ya mwaka 2013 ambayo yalisambaratishwa kwa mabavu na vyombo vya usalama na kusababisha moja kati ya mauaji makubwa zaidi ya raia katika historia ya sasa ya nchi hiyo.
-
"Saudia iliipa hongo timu ya taifa ya Misri ikubali kuifunga kombe la dunia" - Mwandishi
Jun 27, 2018 03:25Mwandishi mmoja wa Misri amelalamika kuwa serikali ya nchi yake ilipokea rushwa na hongo kutoka kwa Saudi Arabia na kuilazimisha timu ya taifa ya nchi hiyo ikubali kufungwa na Saudia katika mashindano ya fainali za kombe la dunia yanayoendelea nchini Russia hivi sasa.
-
Hali ya hatari yarefushwa nchini Misri
Jun 24, 2018 22:24Bunge la Misri kwa mara ya nne limeongeza muda wa hali ya hatari kwa miezi mingine mitatu.
-
Harakati ya mitandao ya kijamii ya kumtaka Rais Sisi wa Misri aondoke madarakani
Jun 23, 2018 20:44Kufuatia kuendelea kuwa mbaya mgogoro wa kiuchumi na kisiasa nchini Misri, wananchi ambao wanakandamizwa sasa wameamua kutumia mitandao ya kijamii hasa Twitter kulalamikia utawala wa Rais Abdel Fatah el Sisi huku wengi wakimtaka aondoke madarakani.
-
Misri yachukua hatua kali za usalama kukabiliana na malalamiko ya wananchi
Jun 17, 2018 22:36Serikali ya Misri imechukua hatua kali za kiusalama kwa ajili ya kukabiliana na malalamiko ya wananchi baada ya kuzidishwa bei ya nishati nchini humo.
-
Al Azhar yalaani wito wa kufutwa aya za Qur'ani
Jun 12, 2018 03:47Sheikh Mkuu wa Al Azhar nchini Misri, Ahmad Tayyib amekosoa vikali wito uliotolewa na kundi la eti wasomi na wanasiasa wa Ufaransa wa kufutwa aya za Qur'ani tukufu.