Asasi za Kiafrika zinazoshiriki katika mkutano wa 22 wa mabadiliko ya tabianchi nchini Morocco zimesisitiza juu ya udharura wa kutekelezwa vipengee vya mkataba wa mabadiliko ya tabianchi vilivyopasishwa katika mkutano wa Paris, Ufaransa.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon, amesema jitihada za kupambana na mabadiliko ya tabianchi ni kwa ajili ya vizazi vijavyo, wakati ambapo kila siku rekodi za uchafuzi wa hali ya hewa zinavunjwa.