-
Bunge la Cuba lautaka utawala wa Kizayuni uache kuwashambulia Wapalestina
May 16, 2021 07:37Kamisheni ya Uhusiano wa Kimataifa ya Bunge la Cuba imelaani jinai na mashambulio ya kikatili yanayofanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya watu wasio na hatia na kuitaka Israel ikomeshe ukatili wake huo.
-
Zarif afuta safari yake Austria akipinga kuwekwa bendera za Israeli kwenye majengo ya serikal
May 16, 2021 00:02Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran amefuta safari yake rasmi nchini Austria akipinga hatua ya nchi hiyo ya kupeperusha bendera za utawala haramu wa Israel juu ya majengo ya serikali katika mji mkuu wa nchi hiyo Vienna, huku Israel ikiendelea kuwaua kinyama raia wa Palestina.
-
Jinai mpya za Wazayuni; Israel yaua kwa umati familia ya watu saba Ghaza
May 15, 2021 03:08Utawala wa Kizayuni unaendelea kufanya jinai za kinyama na za kutisha dhidi ya Wapalestina. Habari za karibuni kabisa zinasema kwamba utawala huo katili umeua kwa umati familia ya watu saba magharibi mwa mji wa Ghaza katika shambulio lake la anga. Watu hao waliouliwa kikatili na Wazayuni ni wanawake watano na watoto wadogo wawili
-
Vita vya "Saifel Quds" na maafa yake kwa utawala wa Kizayuni wa Israel
May 15, 2021 00:00Siku kadhaa zimepita tangu kuanza vita vya Israel na muqawama wa Palestina vinavyojulikana kwa jina la "Saifel Quds" na ingawa kutokana na ukatili wake usio na kifani, utawala wa Kizayuni unasababisha hasara kuwba za roho na mali za Wapalestina kwa kushambulia makazi ya watu, lakini vita hivyo ni kengele ya hatari kwa Israel kwa ushahidi mbalimbali.
-
Netanyahu azishukuru Marekani, Ufaransa, Uingereza na Ujerumani kwa kuunga mkono jinai za Israel
May 14, 2021 23:59Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel amewashukuru na kuwapongeza marais Joe Biden wa Marekani na Emmanuel Macron wa Ufaransa, Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson na Kansela Angela Merkel wa Ujerumani kwa kuunga mkono utawala huo dhalimu katika jinai unazoendelea kufanya dhidi ya wananchi madhulumu wa Palestina.
-
Makumi ya Walebanon wavuka mpaka na kuingia Palestina inayokaliwa kwa mabavu
May 14, 2021 23:56Vyombo vya habari vimeripoti kuwa makumi ya Walebanon wamevunja uzio wa mpaka wa pamoja wa nchi hiyo na ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu zilizopewa jina la Israel na kuingia katika ardhi hizo kuonyesha uungaji mkono wao kwa wananchi wanaodhulumiwa wa Palestina.
-
Makundi ya kutetea haki za binadamu yapinga uamuzi wa Ufarasa wa kupiga marufuku maandamano dhidi ya Israel
May 14, 2021 08:07Wanaharakati na makundi ya kutetea haki za binadamu yamepinga uamuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ufaransa wa kupiga marufuku maandamano ya kupinga ukatili na mauaji yanayofanywa na Israel dhidi ya watu wa Palestina ambayo yamepangwa kufanyika mwishoni mwa wiki hii.
-
Arsenal yamtetea Elneny kwa kuwaunga mkono Wapalestina, yasema wachezaji wana haki ya kueleza maoni yao
May 14, 2021 05:30Klabu ya soka ya Arsenal nchini Uingereza imemtetea mchezaji wake Muislamu raia wa Misri, Mohamed Elneny aliyetuma ujumbe kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter akiwaunga mkono na kueleza mshikamano wake na watu wa Palestina wanaoendelea kushambuliwa na kuuawa na jeshi la utawala haramu wa Israel.
-
Hania awataka Waislamu, watu huru duniani kutetea Msikiti wa al Aqsa
May 14, 2021 04:28Mkuu wa Idara ya Siasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) ameutaka Umma wa Kiislamu na Kiarabu kufanya maandamano na mikutano ya kutetea na kuunga mkono Msikiti wa al Aqsa na watu wa Palestina.
-
Wazayuni wakiri kipigo, wameshapata hasara ya dola milioni 160 kwa mashambulio ya muqawama
May 13, 2021 07:23Chama cha Wazalishaji Bidhaa cha utawala wa Kizayuni kimetangaza kuwa, tangu yalipoanza mashambulizi ya makombora wanamapambano wa Palestina siku chache zilizopita hadi hivi sasa, sekta ya uzalishaji bidhaa ya Israel imeshapata hasara ya dola miliioni 160.