-
Taasisi za Palestina: Maelfu ya wafungwa wanateswa katika magereza ya Israel
Dec 27, 2025 06:01Asasi mbili za Kipalestina yametangaza kwamba, zaidi ya mateka na wafungwa 9,300 wa Palestina wanaoshikiliwa katika magereza na vituo vya kuzuiliwa vya Israel wanakabiliwa na "mateso yaliyopangwa."
-
Waziri wa Vita: Israel kamwe haitaondoka Ukanda wa Gaza
Dec 26, 2025 11:52Israel Katz Waziri wa Vita wa Israel amesisitiza kuwa Tel Aviv "kamwe haitaondoka " Gaza, na kwamba watajenga vitongoji vya walowezi wa Kizayuni kaskazini mwa ukanda huo, hatua ambayo ni kinyume na makubaliano ya kusitisha mapigano.
-
Nchi 14 zikiwemo za EU zalaani mpango wa ujenzi haramu Ukingo wa Magharibi
Dec 25, 2025 06:40Kundi la nchi 14 zikiwemo za Ulaya limetoa taarifa ya pamoja ya kulaani vikali uamuzi wa Israel wa kuanzisha ujenzi mpya wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan unaokaliwa kwa mabavu, na kuitaja hatua hiyo kuwa ni ukiukaji wa sheria za kimataifa.
-
Mwanaharakati Muaustralia aliyesilimu kutokana na Palestina: Nashangaa watu wote si Waislamu
Dec 24, 2025 06:18Robert Martin, mwandishi na mwanaharakati Muaustralia mtetezi na muungaji mkono wa Palestina, ambaye amesilimu hivi karibuni amesema, uungaji mkono wake kwa Palestina na safari yake ya kiimani kuelekea kwenye dini tukufu ya Uislamu vimechochewa na miaka kadhaa ya uanaharakati na tajiriba aliyopata katika safari za misafara ya meli za Uhuru, ambazo zimejaribu kuvunja kizuizi kilichowekwa na Israel dhidi ya Ukanda wa Ghaza.
-
Mufti wa Al-Azhar: Kiwango cha dhulma ilichofikia kadhia ya Palestina hakimruhusu mtu kubaki njiapanda
Dec 24, 2025 02:39Taasisi kubwa zaidi ya Kiislamu nchini Misri ya Al-Azhar imesema, piganio la haki la Palestina limefikia kiwango cha dhulma na ukandamizwaji ambacho hakimruhusu mtu kubaki njiapanda na kudai kuwa haegemei upande wowote.
-
Uhaba wa dawa za matibabu Gaza umefikia viwango vya kutisha kufuatia mzingiro wa Israel
Dec 22, 2025 10:52Wizara ya Afya ya Gaza imetahadharisha kuhusu uhaba mkubwa na hatari zaidi wa dawa na vifaa vya matibabu. Imesema kuwa uhaba huo umelemaza uwezo wa eneo hilo wa kutoa huduma ya dharura ya matibabu na kuokoa maisha ya wagonjwa kufuatia kuendelea mzingiro wa Israel dhidi ya Gaza.
-
Albanese: Misri inaunga mkono mauaji ya halaiki ya Wapalestina
Dec 22, 2025 02:51Ripota Maalum wa Umoja wa Mataifa ameitaja hatua ya Misri ya kuidhinisha makubaliano ya ununuzi wa gesi kutoka kwa utawala wa Israel kuwa ni uungaji mkono wa nchi hiyo kwa mauaji ya halaiki yanayofanywa na Wazayuni huko Gaza.
-
Ripoti: Watoto wa Gaza wanateseka na baridi kali
Dec 21, 2025 02:35Dhoruba za majira ya baridi kali zimesababisha vifo vya Wapalestina wasiopungua 17 katika Ukanda wa Gaza mwezi huu wa Disemba pekee.
-
Mtazamo wa Tunisia na Afrika: Palestina ni jeraha kubwa zaidi la mfumo wa haki wa kimataifa
Dec 16, 2025 12:12Tunisia imeitangaza kadhia ya Palestina kuwa ni jeraha kubwa zaidi la mfumo wa haki duniani.
-
Iran yaitaka dunia izuie kuendelea mauaji ya Wapalestina Gaza
Dec 16, 2025 06:49Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghaei, amelaani vikali kuendelea kwa mauaji ya halaiki ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, akiashiria mashambulizi ya mabomu yanayoendelea kufanywa na Wazayuni na kuzuiwa kwa misaada ya kibinadamu.