-
WHO: Zaidi ya wagonjwa 16,000 huko Gaza wanasubiri kupelekwa nje kwa ajili ya matibabu
Nov 11, 2025 10:45Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema kuwa wagonjwa wasiopungua 16,500 katika Ukanda wa Gaza wanasubiri kupelekwa nje kwa ajili ya matibabu na kusisitiza kuwa suhula zake za tiba ziko tayari mpakani lakini haziwezi kuingia katika eneo hilo kufuatia Israel kufunga vivuko hivyo.
-
HAMAS: Lengo la safari ya rais wa Israel Afrika ni kubadilisha misimamo ya nchi zinazounga mkono Palestina
Nov 10, 2025 06:18Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetangaza kuwa safari ya rais wa utawala ghasibu wa kizayuni katika nchi za Afrika ni jaribio la kutaka kubadilisha msimamo wa nchi hizo wa zinazopinga ukoloni na kuunga mkono haki za watu wa Palestina.
-
Palestina: Hati zilizotolewa na Uturuki za kukamatwa viongozi wa Israel ni 'ushindi kwa haki'
Nov 09, 2025 03:29Palestina imesifu na kupongeza hatua ya Uturuki ya kutoa hati za kukamatwa viongozi 37 wa utawala wa kizayuni wa Israel na kuielezea kuwa ni 'ushindi kwa haki' huku ikizitolea mwito nchi zingine kufuata mfano wa Ankara.
-
UN: Mashambulizi ya walowezi wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukingo wa Magharibi yamefikia kiwango cha juu zaidi
Nov 08, 2025 07:57Umoja wa Mataifa umetangaza kwamba walowezi wa Israel wamefanya mashambulizi yasiyopungua 264 dhidi ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu mwezi uliopita wa Oktoba, ikiwa ni idadi kubwa zaidi ya kila mwezi tangu maafisa wa Umoja wa Mataifa walipoanza kufuatilia mashambulizi kama hayo mwaka 2006.
-
Utafiti: Vita vya mauaji ya kimbari vya Israel vimegharimu zaidi ya miaka milioni 3 ya maisha ya mwanadamu huko Gaza
Nov 05, 2025 03:06Utafiti wa hivi karibuni uliochapishwa katika jarida la Lancet umefichua kuwa zaidi ya miaka milioni tatu ya maisha ya binadamu yamepotea katika Ukanda wa Gaza tangu utawala ghasibu wa Israel uanzishe kampeni yake ya mauaji ya kimbari dhidi ya watu Ukanda wa Gaza ulio chini ya mzingiro, mwezi Oktoba mwaka 2023.
-
Nyaraka za jeshi la Israel zafichua: Mfungwa wa Kipalestina aliyebakwa alikuwa raia, si mpiganaji
Nov 04, 2025 11:18Waraka wa siri wa jeshi la Israel umefichua kwamba mtu aliyeshambuliwa kikatili na kubakwa na kundi la wanajeshi wa Israel katika gereza maarufu la Sde Teiman mnamo Julai mwaka jana hajawahi kushtakiwa kwa uhalifu wowote na alikuwa raia, kinyume na madai kwamba alikuwa na mwanachama harakati za mapambano ya Hamas.
-
Israel yaandaa muswada wa 'kifashisti' wa kuruhusu utoaji wa hukumu ya adhabu ya kifo kwa Wapalestina
Nov 04, 2025 02:25Kamati moja ya wabunge wa utawala wa kizayuni wa Israel imeidhinisha muswada wa kuanzisha utoaji wa adhabu ya kifo kwa Wapalestina wanaoshikiliwa kwenye magereza ya utawala huo, na kufungua njia ya kusomwa hoja hiyo kwa mara ya kwanza bungeni licha ya kuandamwa na lawama nyingi.
-
Israel yaendelea kuwatesa kwa njaa Wapalestina kwa kuruhusu 24% tu ya misaada kuingizwa Ghaza
Nov 02, 2025 06:50Mamlaka za Palestina katika Ukanda wa Ghaza zimetangaza kuwa utawala wa kizayuni wa Israel umeruhusu kuingizwa katika eneo hilo sehemu ndogo tu ya misaada ya kibinadamu kinyume na ilivyoafikiwa katika makubaliano ya usitishaji mapigano yanayosimamiwa na serikali ya Marekani, ambayo yalianza kutekelezwa mwezi uliopita.
-
UNICEF: Usitishaji vita Gaza ni fursa muhimu ya kukidhi mahitaji ya watoto
Oct 28, 2025 03:14Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umetangaza kuwa, usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza unaweza kuwa "fursa muhimu" ya kulinda maisha, utu na mahitaji muhimu ya watoto milioni moja wa Kipalestina.
-
Hamas yasisitiza haki ya Wapalestina ya kuwa na nchi huru; yasema imesitisha mapigano Gaza
Oct 27, 2025 06:28Afisa wa ngazi ya juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amesisitiza dhamira isiyoyumba ya harakati hiyo ya kutekeleza usitishaji vita huko Gaza na kusema Wapalestina hawataki kitu chochote isipokuwa haki yao inayotambulika kimataifa ya kuwa na nchi huru.