-
Waziri wa Ulinzi wa Qatar: Hatutashiriki katika vita vyovyote dhidi ya Iran
Jun 04, 2018 01:29Khalid bin Mohammad Al Attiyah, Naibu Waziri Mkuu wa Qatar ambaye pia ni Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo amesema kuwa nchi yake haitoshiriki katika vita vyovyote dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kuongeza kwamba, haamini kuwa Marekani pia itatekeleza vita vya namna hiyo dhidi ya Tehran.
-
Saudia yatishia kuishambulia kijeshi Qatar iwapo itanunua S-400 kutoka Russia
Jun 02, 2018 03:27Mfalme Salman Bin Abdul Aziz Aal-Saud wa Saudi Arabia ametishia kuwa Riyadh itachukua hatua za kijeshi dhidi ya Qatar iwapo serikali ya Doha itaendelea na mpango wake wa kununua mfumo wa makombora wa S-400 kutoka Russia.
-
Mgogoro wa Qatar na nchi za Kiarabu wazidi kutokota, Doha yapiga marufuku bidhaa za Saudia, Imarati, Bahrain na Misri
May 27, 2018 00:13Katika hali inayoonekana ni kuzidi kuwa mkubwa mgogoro wa Qatar na nchi nne za Kiarabu zilizoizingira kila upande nchini hiyo, wizara ya uchumi na biashara ya Qatar jana ilipiga marufuku kuhifadhi, kunua na kuuza bidhaa yoyote iliyotengenezwa Saudi Arabia, Umoja wa Falme za Kiarabu yaani Imarati, Bahrain na Misri.
-
Mwanamfalme wa Qatar: Saudia iliyoiuza al-Aqsa kwa adui, haina haki ya kusimamia al-Kaabah
May 19, 2018 09:35Mjukuu wa mwasisi wa taifa la Qatar sambamba na kukosoa vikali mienendo ya Mfalme Salman bin Abdulaziz Al Saud wa Saudi Arabia kwa kuitumikia Marekani na utawala wa Kizayuni, amesema kuwa mtu ambaye ameiuza Masjidul-Aqsa kwa adui wa Uislamu, hafai kuwa msimamizi wa nyumba ya Mwenyezi Mungu ya al-Kaabah.
-
Qatar kuendelea kuisaidia Somalia huku mgogoro na Imarati ukitokota
May 15, 2018 09:14Qatar imeahidi kuendelea kuunga mkono jitihada za serikali ya Somalia za kurejesha uthabiti na uhuru wa kujitawala huku mgogoro kati ya nchi hiyo ya Pembe ya Afrika na Umoja wa Falme za Kiarabu ukiendelea kutokota.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar: mzingiro dhidi ya Qatar ni kwa ajili ya kuficha matatizo ya ndani Saudia
May 13, 2018 11:12Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar amesema kuwa sababu iliyopelekea nchi yake kuwekewa mzingiro ni kutaka kuficha matatizo ya matukio ya ndani ya Saudi Arabia, Imarati na Bahrain.
-
Saudia: Sharti serikali ya Qatar itume vikosi Syria ili isipinduliwe
Apr 25, 2018 02:57Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia amesema iwapo serikali ya Qatar inataka isiondolewe madarakani na iendelee kudhaminiwa usalama na Marekani, sharti itume wanajeshi wake nchini Syria.
-
Nchi zinazoizingira Qatar zakariri madai yao kwa Doha kama sharti la kufungua upya mahusiano
Apr 13, 2018 02:53Kwa mara nyingine nchi nne za Kiarabu zainazoizingira Qatar ambazo ni Saudi Arabia, Bahrain, Imarati na Misri, zimekariri masharti yao 13 kwa serikali ya Doha kama njia ya kufungua upya uhusiano wao na nchi hiyo.
-
Marekani yaiuzia Qatar makombora 5000 huku mgogoro na Saudia ukitokota
Apr 11, 2018 00:05Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imetangza idhini ya kuiuzia Qatar makombora 5000 yenye thamani ya dola milioni 300 huku mgogoro baina ya nchi hiyo ndogo na Saudia ukizidi kutokota.
-
Saudia inapanga kuigeuza Qatar kisiwa na jalala la takataka za nyuklia
Apr 10, 2018 12:25Saudi Arabia inapanga kuanzisha mradi wa ujenzi wa mfereji kwenye mpaka wake wa pamoja wa ardhini na Qatar ambao utaigeuza nchi hiyo ndogo ya Kiarabu katika Ghuba ya Uajemi kuwa kisiwa.