Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa: " Chanzo cha izza inayoongezeka na ustawi wa hali ya juu wa taifa la Iran katika kipindi cha miaka 40 iliyopita ni kutekeleza mafundisho ya Qur'ani Tukufu hasa kuhusu kusimama kidete na leo pia njia pekee ya kupata ushindi dhidi ya mashetani na makafiri ni kusimama kidete."
Qarii mashuhuri wa Qur'ani Tukufu kutoka nchini Tanzania Ustadh Rajayi Ayoub amesema Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani ya Iran ni fursa muhimu ya kuleta umoja miongoni mwa Waislamu duniani.
Qarii wa Qur'ani Tukufu kutoka Kenya ambaye ameshiriki katika Mashindano 36 ya Kimataifa ya Qur'ani ya Iran amesema mashindano hayo yanaimarisha umoja baina ya Waislamu.
"Kutekeleza mafundisho ya Qur'ani kunaandaa uwanja wa kupatikana izza (heshima), ustawi, maendeleo, nguvu, mshikamano, mtindo mzuri wa maisha katika dunia na kudhaminiwa saada na ufanisi wa Akhera."
Mashindano ya 36 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu yamemalizika leo Jumapili, Aprili 14, 2019 hapa mjini Tehran na kushindanisha washiriki kutoka nchi 83 za dunia.
Katika harakati nyingine ya uenezaji chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia), kiongozi wa chama kimoja cha mrengo wa kulia chenye misimamo ya kufurutu mpaka nchini Denmark ameuchoma moto msahafu mbele ya jengo la bunge la nchi hiyo.
Mashindano ya 33 ya kitaifa ya kila mwaka ya Qur'ani nchini Nigeria yanaendelea kufanyika kwa kushirikisha majimbo 33 ya nchi hiyo katika fani sita za Qur'ani tukufu.
Akademia ya Uislamu katika Sayansi na Jamii ya Chuo Kikuu cha Goethe nchini Ujerumani imeunda makundi mawili ya utafiti kwa lengo la kubuni mfumo wa kidijitali wa kuhifadhi maelezo na uchambuzi wa Qurani Tukufu na 'Sheria za Qurani'.
Sheikh Mkuu wa Al Azhar nchini Misri, Ahmad Tayyib amekosoa vikali wito uliotolewa na kundi la eti wasomi na wanasiasa wa Ufaransa wa kufutwa aya za Qur'ani tukufu.
Mkuu wa Kituo cha Kiislamu nchini Uingereza ameashiria Wasia wa Kimaanawi na Kisiasa wa Imam Khomeini MA, mwasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kueleza kwamba, kwa mtazamo wa kiongozi huyo Qur'ani imeleta ujumbe wa amani na umoja kwa jamii ya wanadamu.