-
Rouhani: Iran ina nafasi nzuri duniani katika kukabiliana na corona
Mar 29, 2020 13:11Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, ripoti iliyotolewa na Waziri wa Afya hapa nchini kuhusiana na ugonjwa wa COVID-19 (corona) inaonyesha kuwa, Iran iko kwenye nafasi inayokubalika katika kutibu na kupambana na maambukizi ya virusi hivyo.
-
Rais Hassan Rouhani asisitiza kutekelezwa kikamilifu mipango yote ya kukabiliana na Corona
Mar 28, 2020 12:27Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, ili kukabiliana na virusi vya Corona, ni lazima kutekelezwa kikamilifu na kwa uangalifu mpango wa mtengano wa kijamii nchini Iran.
-
Rouhani atangaza mikakati mipya ya kukabili corona Iran, waliopona ni zaidi ya 10,000
Mar 26, 2020 12:05Rais Hassan Rouhani wa Iran ametangaza mipango na mikakati mipya ya kudhibiti maambukizi ya kirusi cha corona hapa nchini ndani ya wiki mbili zijazo.
-
Rouhani: Nchi na mataifa yote yanapaswa kushirikiana katika kupambana na corona
Mar 24, 2020 08:19Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa kasi ya maambukizi ya virusi vya corona imekuwa maudhui ya kimataifa na kuongeza kuwa, nchi na mataifa yote yanalazimika kupambana na janga hilo.
-
Rais Rouhani: Misaada ya Marekani kwa Iran ni hadaa na uongo mkubwa wa kihistoria
Mar 23, 2020 14:06Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, madai ya Wamarekani wanaosema kuwa wako tayari kutoa msaada wa kukabiliana na virusi vya corona kwa Iran, ni hadaa na uongo mkubwa wa kihistoria.
-
Rais Rouhani: Takwimu za mapambano ya corona nchini Iran zinatia matumaini
Mar 21, 2020 11:51Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewapongeza wananchi kutokana na kutilia maanani maagizo yanayotolewa na maafisa wa Tume ya Taifa ya Kupambana na Virusi vya Corona na kusema: Takwimu na ripoti zinazohusiana na mapambano dhidi ya virusi vya corona nchini Iran zinatia matumaini.
-
Rais Rouhani: Wananchi wa Marekani wasikubali nyaraka za historia ya Marekani zizidi kuwa chafu zaidi ya hivi
Mar 21, 2020 04:05Rais Hassan Rouhani amewatumia ujumbe maalumu wananchi wa Marekani akitahadharisha kuwa: Siasa zozote za uono finyu na za uhasama zitazolenga kudhoofisha mfumo wa utabibu na kuviwekea mpaka vyanzo vya fedha vya kushughulikia hali mbaya iliyoko Iran zitakuwa na athari ya moja kwa moja kwa mchakato wa kupambana na janga la dunia nzima la corona katika nchi zingine.
-
Rais Rouhani: Mwaka uliopita ulijaa hamasa kubwa ya wananchi wa Iran
Mar 20, 2020 08:23Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika ujumbe wake wa mwaka mpya wa 1399 Hijria Shamsia kwamba: Mwaka uliopita ulikuwa mwaka wa matukio na hamasa nyingi, na kwamba matukio makubwa zaidi katika historia ya nchi hii na hamasa zenye fahari kubwa zimetengenezwa na wananchi mashujaa wa Iran katika mwaka huo.
-
Kuzinduliwa miradi ya kiuchumi na miundo msingi; ishara ya uwezo mkubwa wa Iran
Mar 18, 2020 07:45Tukiwa katika siku za mwisho za mwaka wa Kiirani wa 1398 Hijria Shamshia ambao unamalizika 20 Machi 2020, vyombo vya habari vinajishughulisha kuakisi habari zinazohusu kuenea ugonjwa wa COVID-19 au corona.
-
Rais Rouhani: Takwimu na kiwango cha mwenendo wa mapambano ya virusi vya Corona, ni zenye kutia matumaini
Mar 16, 2020 12:20Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran sambamba na kupongeza juhudi zisizo na kifani za watumishi wa sekta ya afya nchini hapa katika kupambana na ugonjwa wa Corona, amesema kuwa takwimu na kiwango cha mwenendo wa mapambano dhidi ya virusi vya Corona nchini Iran ni zenye kutia matumaini.