-
Balozi mdogo wa Saudia nchini Uturuki atoroka usiku usiku, Bin Salman apata pigo jingine
Oct 17, 2018 08:54Balozi mdogo wa Saudi Arabia mjini Istanbul, Mohammed al-Otaibi ametoroka usiku kutoka Uturuki na kuelekea Riyadh.
-
New York Times: Washukiwa wote wa mauaji ya Khashoggi ni watu wa karibu kwa Bin Salman
Oct 17, 2018 05:26Gazeti la New York Times la Marekani limefichua kwamba washukiwa wa mauaji ya mwandishi na mkosoaji wa utawala wa Saudia, Jamal Khashoggi katika ubalozi wa nchi hiyo mjini Istanbul huko Uturuki wana uhusiano na mrithi wa kiti cha ufalme wa utawala huo, Muhammad bin Salman.
-
Waziri wa Mafuta wa Iran: Marekani lazima iondoe vikwazo ili bei ya mafuta ishuke
Oct 17, 2018 00:48Bijan Namdar Zangeneh, Waziri wa Mafuta wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, iwapo Marekani itaiondolea vikwazo Iran, bei ya mafuta katika soko la dunia itapungua na hali ya kuvurugika uthabiti iliyopo katika soko hilo hivi sasa itaondoka.
-
UN yataka kuondolewa kinga ya kutoshtakiwa wanadiplomasia wa Saudia wanaohusishwa na kadhia ya Khashoggi
Oct 16, 2018 10:40Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ametaka kuondolewa kinga ya kutoshtakiwa wanadiplomasia wa Saudi Arabia ambao inawezekana wamehusika na kutoweka nchini Uturuki, Jamal Khashoggi, mwandishi wa habari raia wa Saudia.
-
Serikali ya Qatar nayo yaitaka Saudi Arabia kueleza walipo raia wake waliotekwa nyara na nchi hiyo
Oct 15, 2018 01:16Huku dunia ikiwa bado inaishinikiza Saudia kuweka wazi hatma ya mwandishi wa habari na mkosoaji wake aliyetoweka katika ubalozi wa nchi hiyo nchini Uturuki, serikali ya Qatar kupitia mkuu wa kamisheni ya kitaifa ya haki za binaadamu, ameitaka Riyadh kuieleza Doha kuhusu hatma ya raia wake waliotekwa nyara na utawala wa Aal Saud.
-
HRW yataka Saudia ifukuzwe katika Baraza la Haki za Binadamu la UN
Oct 13, 2018 12:25Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limetoa wito wa kufukuzwa Saudi Arabia katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa.
-
Makabiliano ya kidiplomasia yajiri kati ya Iran, Marekani na Saudia katika Umoja wa Mataifa
Oct 13, 2018 04:40Mjumbe wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Kamati ya Kwanza ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa amewakabili wawakilishi wa Marekani na Saudi Arabia katika umoja huo na kuwaeleza kwamba, utawala wa kifalme wa Saudia ni utawala wa kigaidi ambao hata waandishi wa habari pia hawasalimiki na mauaji ya kigaidi yanayofanywa na utawala huo.
-
Ujerumani yaionya Saudia yasema ni lazima iweke wazi hatma ya Jamal Khashoggi
Oct 13, 2018 04:23Serikali ya Ujerumani imeitaka Saudi Arabia kuweka wazi hatma ya Jamal Khashoggi, mwandishi wa habari mwenye uraia wa nchi hiyo na mkosoaji wa utawala wa Aal-Saud aliyetoweka baada ya kuingia kwenye ubalozi mdogo wa Saudia mjini Istanbul, Uturuki.
-
Mkuu wa Benki ya Dunia asusia mkutano wa Saudi Arabia, kisa, mauaji ya Khashoggi
Oct 12, 2018 23:15Mkuu wa Benki ya Dunia amekataa kushiriki katika mkutano wa wawekezaji uliopangwa kufanyika Saudi Arabia.
-
Uturuki: Tuna mkanda unaothibitisha Saudia imemuua Khashoggi
Oct 12, 2018 13:42Afisa mmoja wa masuala ya usalama wa Uturuki amesema kuwa, kuna mkanda wa sauti na video unaothibitisha kuwa mwandishi habari na mkosoaji wa utawala wa kifalme wa Saudi Arabia, Jamal Khashoggi ameuawa ndani ya ubalozi wa nchi hiyo nchini Uturuki.