-
HRW: Saudia imruhusu mtoto wa Khashoggi kuondoka nchini humo
Oct 24, 2018 23:04Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limetangaza kuwa, serikali ya Saudi Arabia inapaswa kumruhusu mwana wa kiume wa mwandishi na mkosoaji wa nchi hiyo aliyeuawa ndani ya ubalozi wa Saudia mjini Istanbul huko Uturuki, Jamal Khashoggi kuondoka nchini humo.
-
Rais wa Marekani akiri kwamba, Bin Salman alihusika katika mauaji ya Khashoggi
Oct 24, 2018 04:30Rais Donald Trump wa Marekani amethibitisha kwamba, Muhammad bin Salman mrithi wa kiti cha ufalme wa Saudi Arabia alihusika katika mauaji ya Jamal Khashoggi, mwandishi wa habari na mkosoaji mkubwa wa utawala wa Aal Saud.
-
OCHA: Yemen inakabiliwa na hali mbaya ya baa la njaa
Oct 24, 2018 04:22Ofisi ya Uratibu ya Umoja wa Mataifa Inayoshughulikia Masuala ya Kibinaadamu (OCHA) imetangaza kuwa, nchi ya Yemen inakabiliwa na hali mbaya ya baa la njaa.
-
Kushadidi radiamali za Ulaya dhidi ya jinai za Saudi Arabia
Oct 22, 2018 23:33Utawala wa Saudi Arabia ambao daima umekuwa ukijifakharisha kuwa na uhusiano mzuri na madola ya Magharibi, filihali unakabiliwa na changamoto ambayo haijawahi kushuhudiwa katika uga wa kimataifa.
-
Mfalme Salman wa Saudia awapiga kalamu nyekundu maafisa watano wa vyombo vya usalama
Oct 20, 2018 12:40Kufuatia faili la kuuawa Jamal Khashoggi, mwandishi wa habari na mkosoaji wa utawala wa Aal-Saud, maafisa watano wa vyombo vya usalama wa wamepigwa kalamu nyekundu na mfalme Salman bin Abdulaziz wa Saudia.
-
Balozi mdogo wa Saudia nchini Uturuki atoroka usiku usiku, Bin Salman apata pigo jingine
Oct 17, 2018 08:54Balozi mdogo wa Saudi Arabia mjini Istanbul, Mohammed al-Otaibi ametoroka usiku kutoka Uturuki na kuelekea Riyadh.
-
New York Times: Washukiwa wote wa mauaji ya Khashoggi ni watu wa karibu kwa Bin Salman
Oct 17, 2018 05:26Gazeti la New York Times la Marekani limefichua kwamba washukiwa wa mauaji ya mwandishi na mkosoaji wa utawala wa Saudia, Jamal Khashoggi katika ubalozi wa nchi hiyo mjini Istanbul huko Uturuki wana uhusiano na mrithi wa kiti cha ufalme wa utawala huo, Muhammad bin Salman.
-
Waziri wa Mafuta wa Iran: Marekani lazima iondoe vikwazo ili bei ya mafuta ishuke
Oct 17, 2018 00:48Bijan Namdar Zangeneh, Waziri wa Mafuta wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, iwapo Marekani itaiondolea vikwazo Iran, bei ya mafuta katika soko la dunia itapungua na hali ya kuvurugika uthabiti iliyopo katika soko hilo hivi sasa itaondoka.
-
UN yataka kuondolewa kinga ya kutoshtakiwa wanadiplomasia wa Saudia wanaohusishwa na kadhia ya Khashoggi
Oct 16, 2018 10:40Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ametaka kuondolewa kinga ya kutoshtakiwa wanadiplomasia wa Saudi Arabia ambao inawezekana wamehusika na kutoweka nchini Uturuki, Jamal Khashoggi, mwandishi wa habari raia wa Saudia.
-
Serikali ya Qatar nayo yaitaka Saudi Arabia kueleza walipo raia wake waliotekwa nyara na nchi hiyo
Oct 15, 2018 01:16Huku dunia ikiwa bado inaishinikiza Saudia kuweka wazi hatma ya mwandishi wa habari na mkosoaji wake aliyetoweka katika ubalozi wa nchi hiyo nchini Uturuki, serikali ya Qatar kupitia mkuu wa kamisheni ya kitaifa ya haki za binaadamu, ameitaka Riyadh kuieleza Doha kuhusu hatma ya raia wake waliotekwa nyara na utawala wa Aal Saud.