-
Msemaji wa Ansarullah: Vita vya Yemen ni wenzo wa kufanikisha "Muamala wa Karne"
Sep 14, 2018 19:28Msemaji wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema kuwa vita vya muungano vamizi unaoongozwa na Saudi Arabia dhidi ya watu wa Yemen ni kibiashara inayotumiwa na Marekani ili kuendeleza njama mpya ya Washington na Wazayuni ya "Muamala wa Karne" dhidi ya Palestina.
-
Utawala wa Aal-Saud washadidisha siasa za ubaguzi wa kimadhehebu katika mwezi Muharram
Sep 12, 2018 22:12Sambamba na kuanza mwezi wa Muharram ambao ndani yake Waislamu hufanya maombolezo ya kukumbuka tukio chungu la Ashura la kuuawa shahidi Imam Hussein (as) mjukuu wa Mtume (saw), askari wa utawala wa Aal-Saud wameanzisha ukandamizaji wa kimadhehebu katika eneo la mashariki mwa nchi hiyo dhidi ya Waislamu wa Shia.
-
Serikali ya Saudia yampandisha kizimbani mwendesha vipindi wa TV kwa kuiunga mkono Ikhwanul Muslimin
Sep 11, 2018 00:15Mahakama ya Jinai nchini Saudia imemsomea mashitaka mwendesha vipindi wa televisheni ya nchi hiyo kwa tuhuma za kuiunga mkono harakati ya Ikhwanul Muslimin.
-
Iran katu haitafanya mazungumzo kuhusu uwezo wake wa makombora
Sep 09, 2018 23:07Mshauri wa Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi Yote ya Iran katika masuala ya viwanda vya kijeshi amesisitiza kuwa: "Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitafanya mazungumzo kuhusu uwezo wake wa makombora."
-
Vipigo vya makombora ya Yemen dhidi ya mishipa ya kiuchumi ya Saudia na Imarati
Sep 05, 2018 01:40Jeshi na kamati za kujitolea za wananchi wa Yemen zimeamua kulipiza kisasi cha jinai zinazofanywa na Saudi Arabia na wavamizi wenzake, kupitia kushambulia kwa makombora mishipa ya kiuchumi ya Saudia na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).
-
Uhispania yafuta mkataba wa kuiuzia Saudia mabomu 400
Sep 04, 2018 09:06Uhispania imetangaza kubatilisha mkataba wa kuiuzia Saudi Arabia mabomu 400 yenye thamani ya Euro milioni 9.2 kufuatia jinai za hivi karibuni za muungano unaoongozwa na Saudia ambao umeua idadi kubwa ya watoto Wayemen.
-
Hizbullah: Kukombolewa Idlib kutapiku turufu ya mwisho ya Marekani, Israel na Saudia nchini Syria
Sep 03, 2018 03:24Naibu Mkuu wa Baraza la Utendaji la Hizbullah ya Lebanon amesema, kukombolewa mkoa wa Idlib kaskazini magharibi mwa Syria ambayo ni ngome ya mwisho ya magaidi katika nchi hiyo litakuwa pigo kubwa kwa Magharibi, Marekani, utawala wa Kizayuni wa Israel na Saudi Arabia.
-
Majeshi wa majini ya Yemen yalenga meli ya kivita ya Saudia pwani ya Jizan
Sep 01, 2018 21:50Majeshi ya majini ya Yemen, yakishirikiana na Kamati za Wananchi, yamelenga meli ya kivita ya Saudia katika eneo la mpakani la Jizan kusini magharibi mwa Saudi Arabia.
-
Saudia na Imarati zinailaghai Jordan iunge mkono mpango wa Marekani wa Muamala wa Karne
Aug 31, 2018 23:38Mbunge wa Jordan, Khalid Ramadhan amefichua hila na ulaghai mpya unaofanywa na Saudi Arabia ikishirikiana na Umoja wa Falme za Kiarabu, Imarati wa kuishawishi Jordan iunge mkono mpango wa Marekani wa kuiangamiza Palestina unaojulikana kama "Muamala wa Karne".
-
Qatar yazishutumu Saudia, UAE kwa kushirikiana na magaidi wa al Qaeda nchini Yemen
Aug 31, 2018 02:02Balozi wa Qatar nchini Marekani amezishutumu Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kwa kuwa na ushirikiano wa siri na magaidi wa al-Qaeda nchini Yemen.