-
Mgogoro baina ya Qatar na nchi za Kiarabu umezidi kupamba moto
Nov 23, 2017 03:49Kwa mara nyingine tena nchi za Saudia, Imarati, Misri na Bahrain zimetoa tuhuma kali dhidi ya Qatar kwa kudai kuwa inaunga mkono ugaidi. Jana usiku nchi hizo ziliongeza katika orodha yao ya makundi ya kigaidi taasisi mbili na watu 11 ambao zinadai wanafanya ugaidi kwa uungaji mkono wa Qatar.
-
Hariri arejea Lebanon, ombi lake la kujiuzulu lasimamishwa, akutana na Rais Aoun
Nov 22, 2017 23:56Saad Hariri, Waziri Mkuu wa Lebanon amesimamisha kwa muda ombi lake la kutaka kujiuzulu wadhifa wake huo baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Rais Michel Aoun mjini Beirut.
-
Qatar: Saudia inafanya ukandamizaji ndani ya nchi na uchochezi nje ya nchi
Nov 21, 2017 10:06Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar amekosoa vikali sera ya utawala wa Aal-Saud ya kuwakandamiza wananchi wa Saudi Arabia na wakati huo huo kuzichochea nchi nyingine.
-
Mkuu wa Idara ya Mahakama ya Iran: Saudi Arabia ni mhimili wa shari katika eneo
Nov 20, 2017 11:02Mkuu wa Idara ya Mahakama ya Iran ameitaja Saudi Arabia kuwa mhimili wa Shari na kusisitiza juu ya ulazima wa kusimama kidete mbele ya njama mbovu na za kifisadi za Marekani na waitifaki wake katika eneo hili la Mashariki ya Kati kwa kuwepo umoja na kushikamana zaidi watu wa eneo hili.
-
Mamilioni Yemen yamkini wakafariki kutokana na mzingiro uliowekwa na Saudia
Nov 20, 2017 10:55Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula Dunaini, WFP, limeonya kuwa mamilioni ya watu wa Yemen wanakabiliwa na hatari ya mauti kufuatia mzingiro uliowekwa na Saudi Arabia dhidi ya nchi hiyo na hivyo kuzuia misaada kuwafikia wanaohitajia.
-
Zarif: Ni maskhara kuona Saudi Arabia ikiituhumu Iran kuwa inasababisha machafuko
Nov 19, 2017 23:19Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa ni maskhara kwa Saudia Arabia kuituhumu Iran kuwa inasababisha machafuko katika hali ambayo nchi hiyo ndiyo inayowachochea magaidi na iliyoanzisha vita huko Yemen.
-
Tume ya Kimataifa yapinga madai ya Saudia kuhusu mzingiro wa Yemen
Nov 19, 2017 23:18Tume ya kimataifa iliyoundwa na Umoja wa Mataifa imefichua kwamba Saudi Arabia inazuia kwa makusudi misaada ya kibinadamu inayotumwa kwa watu wanaozongwa na maradhi na njaa huko Yemen na kutangaza kuwa, tume hiyo haikubali sababu zilizotolewa na utawala wa Riyadh za kuendelea kuizingira nchi hiyo.
-
Qatar: Uhusiano wetu na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni wa "kipekee"
Nov 19, 2017 00:39Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar ameutaja uhusiano uliopo kati ya nchi yake na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuwa wa "kipekee".
-
Iran: Sumu hatari ya Uwahabi na Utakfiri ilizaliwa Saudi Arabia
Nov 18, 2017 04:22Mshauri na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema Saudi Arabia ndio chimbuko na sehemu ilikozaliwa idiolojia hatari ya Utakfiri inayotumiwa na magenge ya kigaidi kama vile Daesh (ISIS).
-
Qatar: Saudia inayakandamiza 'mataifa madogo' kwa lengo la kuyapigisha magoti
Nov 18, 2017 04:05Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar amesema utawala wa Saudi Arabia unachochea migogoro na mivutano katika eneo la Mashariki ya Kati sambamba na kuzikandamiza na kuzinyanyasa nchi ndogo katika eneo ili kuzishinikiza zipige magoti mbele yake.