-
Uchunguzi: Nusu ya Waingereza hawajui kama Saudia imeanzisha vita dhidi ya Yemen
Mar 18, 2017 12:32Uchunguzi mpya wa maoni uliofanywa unaonyesha kuwa zaidi ya nusu ya raia wa Uingereza hawana habari kuhusu vita angamizi vilivyoanzishwa na Saudi Arabia dhidi ya Yemen pamoja na kwamba serikali yao ni mmoja wa wauzaji wakuu za silaha zinazotumiwa na utawala wa Aal Saud katika vita hivyo.
-
Radiamali ya Iran kwa madai ya 'kipuuzi' ya Mwana Mfalme wa Saudia alipokutana na Trump
Mar 18, 2017 04:04Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekosoa vikali madai ya kipropaganda ya Riyadh na kuyataja kama ya kipuuzi na yasiyokuwa na msingi matamshi dhidi ya Tehran yaliyotolewa na Mwana Mfalme wa Saudi Arabia alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Marekani, Donald Trump katika Ikulu ya White House hivi karibuni.
-
UN, IOM zalaani mauaji ya wakimbizi 42 wa Kisomali, pwani ya Yemen
Mar 18, 2017 03:44Shirika la Kimataifa la Wahajiri (IOM) limekosoa vikali shambulio lililoua makumi ya wakimbizi raia wa Somalia katika pwani ya Yemen usiku wa kuamkia jana.
-
Wairani kufanya ibada ya Hija mwaka huu baada ya Saudia kukubali masharti ya Tehran
Mar 17, 2017 23:20Maelfu ya raia wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wanatazamiwa kwenda Saudi Arabia kwa ajili ya kufanya ibada ya Hija baada ya maafisa wa seriakali ya Saudi Arabia kukubali masharti ya kudhamini mahitaji ya mahujaji wa Iran.
-
Amnesty yaitaka US ikome kuziuzia silaha Saudia na Bahrain
Mar 16, 2017 11:05Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limeitaka Marekani iache kuziuzia silaha serikali za Saudi Arabia na Bahrain kutokana na nchi hizo kutumia silaha hizo kuvunja haki za raia.
-
Wayemen wataka kuundwe kamati ya kuchunguza jinai za Saudia nchini mwao
Mar 16, 2017 00:28Serikali ya Yemen imetaka kuundwe kamati huru ya kimataifa ya kuchunguza jinai za Saudi Arabia nchini humo.
-
Wanawake Yemen waandamana nje ya ofisi za UN kulaani jinai za Saudia
Mar 15, 2017 03:29Wanawake wa Yemen wamefanya maandamano na kukita kambi nje ya ofisi za Umoja wa Mataifa katika mji mkuu Sana’a, kuutaka umoja huo usitishe jinai na uvamizi wa Saudi Arabia dhidi ya nchi hiyo.
-
Yemen yakosoa kimya cha jamii ya kimataifa kuhusu jinai za Saudia
Mar 14, 2017 01:00Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Uokovu wa Kitaifa ya Yemen ameikosoa jamii ya kimataifa kwa kushindwa kusimamisha jinai, vita na mzingiro uliowekwa dhidi ya nchi hiyo.
-
Wapinzani Maldives wapinga Saudia kuuziwa visiwa
Mar 11, 2017 10:54Vyama vya upinzani nchini Maldives vimepinga safari ya mfalme Salman bin Abdulaziz wa Saudia nchini humo baada ya kuvuja ripoti kuwa anataka kununua sehemu kubwa ya visiwa vya nchi hiyo ndogo ya kusini mwa Asia.
-
Jeshi la Yemen lalipiza kisasi, laua wanajeshi na mamluki 12 wa Saudia
Mar 10, 2017 10:39Jeshi la Yemen na vikosi vya kujitolea vya wananchi wa nchi hiyo vimeshambulia kituo cha kijeshi cha Aal-Saud katika mkoa wa Najran, kusini mwa Saudi Arabia na kuua wanajeshi na mamluki 12 wa utawala huo wa kifalme.