-
Shambulio la droni la RSF laua watu 24 wakiwemo watoto 8 Kordofan Kaskazini, Sudan
Feb 08, 2026 02:29Shambulio la ndege zisizo na rubani la Vikosi vya Usaidizi wa Haraka RSF lililolenga gari lililobeba familia za raia wa Sudan waliolazimika kuyahama makazi yao limeua watu wasiopungua 24, wakiwemo watoto wanane. Hayo ni kwa mujibu wa shirika la mtandao wa Madaktari wa Sudan.
-
Watu 22 wauawa katika shambulio la RSF katika hospitali ya kijeshi Kordofan Kusini
Feb 06, 2026 02:29Watu wasiopungua 22 wakiwemo wahudumu 4 wa sekta ya afya wameuawa na wengine wawane kujeruhiwa baada ya wanangambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) jana kuishambulia hospitali ya jeshi ya al Kuweik katika jimbo la Kordofan Kusini nchini Sudan.
-
Mashambulizi ya droni yaua watu 15 Kadugli, kusini mwa Sudan
Feb 04, 2026 10:22Raia wasiopungua 15, wakiwemo watoto saba, wameuawa katika mashambulizi ya ndege zisizo na rubani katika mji wa Kadugli kusini mwa Sudan. Hayo yamesemwa na kundi la kujitolea la wenyeji na mashuhuda wa hujuma hiyo ambao wameeleza kuwa, mashambulizi hayo yamejiri saa chache baada ya jeshi la Sudan kutangaza kuvunja mzingiro wa miaka mingi dhidi ya mji wa Kadugli.
-
UNICEF: Mgogoro mkubwa zaidi duniani: Sudan ina wakimbizi wa ndani milioni 9.5
Jan 31, 2026 02:42Mfuko wa Kuhudumia Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) amesema kuwa Sudan imekumbwa na mgogoro mkubwa zaidi wa wakimbizi wa ndani duniani, huku takriban watu milioni 9.5 wakilazimika kuhaka makazi yao katika majimbo 18.
-
IOM: Hali mbaya ya usalama imelazimisha mamia ya Wasudan kuhama makazi yao Kordofan Kusini
Jan 30, 2026 07:45Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) limetangaza kuwa watu wasiopungua 285 ni miongoni mwa wale waliolazimika kuyahama makazi yao kwenye kipindi cha siku mbili za karibuni katika miji ya Kadugli na Al-Kuwaik iliyoko kwenye Jimbo la Kordofan Kusini nchini Sudan kutokana na hali mbaya ya usalama.
-
Jeshi la Sudan lavunja mzingiro wa miaka 2 wa wanamgambo wa RSF dhidi ya mji muhimu huko Kordofan
Jan 28, 2026 04:28Jeshi la Sudan limeeleza kuwa limevunja mzingiro wa karibu miaka miwili wa wanamgambo wa RSF katika mji muhimu katika mkoa wa Kordofan, na kudhibiti njia kuu za usafirishaji.
-
Makaburi ya umati ya Khartoum yafichua sura ya giza katika vita vya Sudan
Jan 26, 2026 06:38Makaburi mawili ya umati yenye mabaki ya miili ya maelfu ya watu yalipatikana hivi majuzi mjini Khartoum mji mkuu wa Sudan. Kupatikana kwa makaburi hayo kumefichua sura ya giza katika mzozo unaoendelea Sudan kati ya jeshi la taifa na wanamgambo wa kundi la Rapid Support Forces (RSF)
-
Mwendesha Mashtaka wa Sudan: Tumewafungulia kesi mamluki 122 wa kigeni
Jan 25, 2026 11:44Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Sudan ameeleza kuwa kesi za jinai zimefunguliwa dhidi ya takriban mamluki 122 wa kigeni wanaopigana bega kwa bega na wanamgambo waasi wa Rapid Support Forces (RSF), huku watoto 135 waliosajiliwa kama wapiganaji katika vita hivyo wakirejeshwa kwa familia zao.
-
Pande za kisiasa Sudan kuunda muungano mpya ili kurejesha utawala wa kiraia
Jan 24, 2026 13:04Makundi ya kisiasa ya Sudan ambayo yamejitenga na muungano mkuu wa demokrasia yamesema kuwa yanafanya juhudi za kuunda muungano mpana unaolenga kurejesha utawala wa kiraia nchini humo baada ya karibu miaka minne ya serikali inayoongozwa na jeshi.
-
Save the Children: Sudan inapitia kipindi kirefu zaidi cha kufungwa shule duniani
Jan 23, 2026 03:22Shirika la Save the Children limeonya kwamba vita vinavyoendelea nchini Sudan vimewanyima elimu watoto zaidi ya milioni 8, katika kile kinachoelezwa kama kipindi kirefu zaidi cha kufungwa shule duniani.