-
Sudan yazituhumu Imarati na Ethiopia kushambulia uwanja wa ndege wa Khartoum
May 05, 2026 11:41Sudan leo Jumanne imrudisha nyumbani balozi wake nchini Ethiopia kwa mashauriano na kuzituhutumu Ethiopia na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kuwa zimehusika na mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (droni) katika uwanja wa ndege wa Khartoum.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan: Tumekataa majaribio ya kulazimisha masuluhisho kutoka nje
May 02, 2026 06:59Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan, Mohi El-Din Salem, amefichua kwamba serikali ya nchi yake itafanya tathmini ya uhusiano wake wa kimataifa na kikanda baada ya vita, na hautakuwa sawa na hapo awali. Amesema kuwa wizara yake imezuia majaribio ya kulazimisha masuluhisho ya kigeni kwa nchi yake na haitakubali mashinikizo ya aina yoyote.
-
Ripoti: Viongozi wa RSF wamejenga na kulimbikiza mali za mamilioni ya pesa kwa himaya ya Imarati
Apr 28, 2026 09:34Viongozi wa wanamgambo wa Sudan wanaojulikana kwa jina la Kikosi cha Msaada wa Haraka au Rapid Support Forces (RSF) na mtandao wao wamekusanya mamilioni ya mali za kifahari huko Dubai katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).
-
CIG: UAE iliwalipa mamluki wa Colombia ili kuwasaidia wanamgambo Sudan kufanya mauaji ya kimbari
Apr 26, 2026 08:45Umoja wa Falme za Kiarabu uliwapa mamluki wa Colombia kulisaidia kundi la wanamgambo wa Sudan, la Rapid Support Forces (RSF), kuwaua maelfu ya raia katika nchi hiyo ya kaskazini mashariki mwa Afrika.
-
Mgogoro wa binadamu nchini Sudan waongezeka baada ya mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran
Apr 25, 2026 05:05Uchokozi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran katika Vita vya Ramadhani na ukosefu wa usalama katika Mlango-Bahari wa Hormuz na kuzingirwa kwake na Marekani, ambayo ndiyo njia kuu ya kupitisha nishati na vifaa vya matibabu kote duniani, kumezidisha mgogoro wa binadamu nchini Sudan.
-
Al-Burhan atoa fursa ya msamaha kwa wapiganaji wa RSF watakaoweka silaha zao chini
Feb 25, 2026 03:29Mwenyekiti wa Baraza la Utawala la Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, ametangaza fursa ya msamaha kwa wapiganaji wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) ikiwa wataweka silaha zao chini.
-
Sudan: Pendekezo lolote la kumaliza vita linapasa kulinda maslahi ya taifa na umoja wa ardhi ya nchi hiyo
Feb 24, 2026 04:30Sudan imesema kuwa pendekezo lolote la kumaliza vita na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) linapasa kuzingatia maslahi makuu ya nchi hiyo, mshikamano na umoja wa ardhi nzima ya nchi hiyo.
-
Chad yatangaza kufunga mpaka wake na Sudan kuzuia kuenea mapigano mpakani mwake
Feb 24, 2026 00:35Chad imetangaza kuwa, ili kuzuia kuenea mapigano kwenye maeneo ya mpakani, inaufunga mpaka wake wa pamoja na Sudan hadi itakapotolewa taarifa nyingine.
-
Al-Burhan: Hakutakuwa na suluhu Sudan mpaka RSF iondoke kwenye maeneo yote inayoyakalia
Feb 20, 2026 22:53Mkuu wa Baraza la Utawala la Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, amesema hakutakuwa na usitishaji mapigano mpaka pale Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) vitakapojiondoa kwenye kile alichokieleza kuwa ni maeneo vinayoyakalia na kujikusanya upya katika maeneo yaliyotengwa.
-
Wachunguzi wa UN: Yumkini mauaji ya halaiki yamefanyika El-Fasher
Feb 19, 2026 23:57Ujumbe wa kutafuta ukweli wa Umoja wa Mataifa umesema ukatili uliofanywa na Vikosi vya Usaidizi wa Haraka RSF wakati wa kuutwaa mji wa El-Fasher huko Darfur Magharibi nchini Sudan mwezi Oktoba mwaka jana, una "alama za mauaji ya kimbari" dhidi ya jamii za Zaghawa na Fur.