-
Kitengo cha "Kundi 26" cha RSF chajisalimisha kwa jeshi la Sudan
Aug 02, 2026 02:45Shirika la Habari la Sudan SUNA limetangaza kuwa, kitengo kimoja cha Vikosi vya Usaidizi wa Haraka RSF kimejisalimisha kwa jeshi na kukabidhi wanajeshi wake na vifaa kamili vya kijeshi.
-
Al-Burhan atembelea miji ya kimkakati ya Sudan iliyokombolewa kutoka kwa RSF
Jul 29, 2026 02:19Mwenyekiti wa Baraza la Mpito la Sudan Jenerali Abdel Fattah al-Burhan ametembelea miji ya Umm Sayala na Jabrat al-Sheikh katika jimbo la Kordofan Kaskazini siku moja baada ya jeshi kuchukua udhibiti wa maeneo mawili kutoka kwa wapiganaji wa RSF.
-
Jeshi la Sudan ladai kudhibiti barabara kuu inayounganisha Khartoum na El-Obeid
Jul 28, 2026 03:47Jeshi la Sudan limetangaza kuwa limerejesha udhibiti kamili wa barabara kuu inayounganisha mji mkuu wa nchi hiyo Khartoum, na El-Obeid, mji ambao umekuwa ukizingirwa na kundi la wanamgambo Rapid Support Forces (RSF).
-
Khartoum yatoa ushahidi dhidi ya UAE na kuikosoa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai
Jul 18, 2026 09:07Waziri wa Sheria wa Sudan, Abdullah Darf, amewasilisha kifurushi cha njia za kisheria "zisizo za kawaida" ambazo serikali ya Khartoum inakusudia kuchukua ili kufungua mashtaka dhidi ya serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na kundi la waasi la Rapid Support Forces (RSF), akisisitiza kwamba Khartoum ina "ushahidi wa kutosha na data kamili" kuhusu "ushiriki wa Abu Dhabi katika vita na uhalifu uliofanywa na pande hizo mbili dhidi ya watu wa Sudan."
-
Umoja wa Mataifa waonya dhidi ya kutumia vibaya rasilimali za Sudan kufadhili vita
Jul 16, 2026 03:04Umoja wa Mataifa umetangaza kwamba makundi yanayopigana nchini Sudan yanafaidika kutokana na udhibiti wa rasilimali za nchi hiyo, wakati uchumi wa vita ukichangia katika kuendeleza mzozo huo.
-
Jeshi la Sudan lakomboa eneo la Fashfoun katika jimbo la Blue Nile baada ya mapigano na waasi
Jul 14, 2026 11:03Jeshi la Sudan limesema mapema Jumanne kuwa limekomboa eneo la Fashfoun katika jimbo la Blue Nile baada ya mapigano na waasi wa makundi ya RSF na SPLM-N.
-
Shirika la haki za binadamu: RSF inawashikilia raia 6,000 katika magereza ya El Fasher
Jul 13, 2026 08:15Ripoti iliyoandaliwa na Tume ya Kitaifa ya Haki za Binadamu nchini Sudan imeonyesha kuwa watu 6,000 wanashikiliwa na wapiganaji wa kundi la waasi la Rapid Support Forces (RSF) katika magereza huko El Fasher, mji mkuu wa Jimbo la Darfur Kaskazini, magharibi mwa nchi, na pia imerekodi ukiukwaji wa haki za binadamu uliofanywa na kundi hilo dhidi ya raia.
-
Serikali ya Sudan na UNICEF zaonya kuhusu kuzorota hali ya kiafya katika maeneo yenye migogoro
Jul 12, 2026 10:46Serikali ya Sudan na Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF) zimeonya kuhusu mgogoro mbaya wa utapiamlo miongoni mwa watoto nchini Sudan, huku vita na mapigano ya ndani yakiendelea kwa mwaka wa nne sasa.
-
Shambulio la droni la RSF lauwa raia 10 waliokuwa wakielekea harusini katikati mwa Sudan
Jul 08, 2026 12:20Mtandao wa Madaktari wa Sudan leo umeripoti kuwa shambulio la ndege zisizo na rubani lililofanywa na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) limeua raia 10, wakiwemo wanawake watano kutoka familia moja, katikati mwa Sudan walipokuwa wakieleke harusini.
-
IOM : Mashambulizi ya RSF yanaweza kuifanya El Obeid nchini Sudan kuwa 'El Fasher nyingine'
Jul 06, 2026 02:48Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) limetahdharisha kuwa mji wa El-Obeid nchini Sudan, ambao ni makao makuu ya Jimbo la Kordofan Kaskazini, unaweza kukumbwa na hatima sawa na ile iliyoupata mji wa El Fasher katika jimbo jirani la Darfur Kaskazini iwapo mashambulizi yanayofanywa na wanamgambo wa kikosi cha Msaada wa Haraka, Rapid Support Forces (RSF) yataendelea.