-
Serikali ya Sudan na UNICEF zaonya kuhusu kuzorota hali ya kiafya katika maeneo yenye migogoro
Jul 12, 2026 10:46Serikali ya Sudan na Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF) zimeonya kuhusu mgogoro mbaya wa utapiamlo miongoni mwa watoto nchini Sudan, huku vita na mapigano ya ndani yakiendelea kwa mwaka wa nne sasa.
-
Shambulio la droni la RSF lauwa raia 10 waliokuwa wakielekea harusini katikati mwa Sudan
Jul 08, 2026 12:20Mtandao wa Madaktari wa Sudan leo umeripoti kuwa shambulio la ndege zisizo na rubani lililofanywa na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) limeua raia 10, wakiwemo wanawake watano kutoka familia moja, katikati mwa Sudan walipokuwa wakieleke harusini.
-
IOM : Mashambulizi ya RSF yanaweza kuifanya El Obeid nchini Sudan kuwa 'El Fasher nyingine'
Jul 06, 2026 02:48Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) limetahdharisha kuwa mji wa El-Obeid nchini Sudan, ambao ni makao makuu ya Jimbo la Kordofan Kaskazini, unaweza kukumbwa na hatima sawa na ile iliyoupata mji wa El Fasher katika jimbo jirani la Darfur Kaskazini iwapo mashambulizi yanayofanywa na wanamgambo wa kikosi cha Msaada wa Haraka, Rapid Support Forces (RSF) yataendelea.
-
Raia 11 wauawa katika shambulio la droni sokoni Kordofan Kaskazini nchini Sudan
Jun 07, 2026 11:08Shambulio la ndege zisizo na rubani sokoni katika jimbo la Kordofan Kaskazini nchini Sudan limeua takriban raia 11 na kujeruhi makumi ya wengine.
-
Jeshi la Sudan lazuia shambulio la RSF huko Blue Nile
Jun 04, 2026 11:19Jeshi la Sudan limetangaza kuwa limezima shambulio la Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) kwenye eneo la kimkakati la Al-Baraka nje kidogo ya mji wa Kurmuk katika Jimbo la Blue Nile, kusini mashariki mwa nchi hiyo.
-
Watetezi haki za binadamu: NBA ikomeshe ushirikiano na UAE katika mauaji ya halaiki Sudan
Jun 03, 2026 13:10Watetezi wa haki za binadamu wamekitaka Chama cha Kitaifa cha Mpira wa Kikapu cha Marekani (NBA) kukomesha ushirikiano wake na Umoja wa Falme za Kiarabuu (UAE), wakisema uhusiano wa ligi hiyo na Abu Dhabi unaikingia kifua nchi hiyo ya Ghuba ya Uajemi kutokana na kulaaniwa vikali kwa kuhusika kwake katika vita ndani nchini Sudan.
-
Waasi wa RSF wanaoungwa mkono na UAE wauwa raia 27 siku ya Eid nchini Sudan
May 30, 2026 11:49Waasi wa RSF wamewaua angalau raia 27, wakiwemo wazee, katika shambulio dhidi ya vijiji vilivyoko magharibi mwa Bara katika jimbo la North Kordofan nchini Sudan.
-
Wanamgambo wenye mfungamano na RSF wauwa raia 27 Kordofan Kaskazini
May 30, 2026 03:19Mtandao wa Madaktari wa Sudan umeripoti kuwa wanamgambo wenye mfungamano na Kikosi cha wapiganaji wa RSF kimewaua takriban raia 27, wakiwemo wazee, katika mashambulizi dhidi ya vijiji kadhaa magharibi mwa Bara katika jimbo la Kordofan Kaskazini.
-
Sudan yazituhumu Imarati na Ethiopia kushambulia uwanja wa ndege wa Khartoum
May 05, 2026 11:41Sudan leo Jumanne imrudisha nyumbani balozi wake nchini Ethiopia kwa mashauriano na kuzituhutumu Ethiopia na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kuwa zimehusika na mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (droni) katika uwanja wa ndege wa Khartoum.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan: Tumekataa majaribio ya kulazimisha masuluhisho kutoka nje
May 02, 2026 06:59Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan, Mohi El-Din Salem, amefichua kwamba serikali ya nchi yake itafanya tathmini ya uhusiano wake wa kimataifa na kikanda baada ya vita, na hautakuwa sawa na hapo awali. Amesema kuwa wizara yake imezuia majaribio ya kulazimisha masuluhisho ya kigeni kwa nchi yake na haitakubali mashinikizo ya aina yoyote.