-
Kuzidi kuwa tata vita vya Sudan; indhari ya Umoja wa Mataifa kuhusu kupanuka wigo wake
Dec 23, 2025 11:54Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa sanjari na kusisitiza umuhimu wa kusitisha vita nchini Sudan, ameonya kuhusu utambulisho wake tata na athari zake zinazopanuka kwa nchi jirani na eneo kwa ujumla.
-
Wanamgambo wa RSF wamewaachia huru wafanyakazi 9 wa sekta ya afya huko Darfur
Dec 20, 2025 14:03Mtandao wa Madktari nchini Sudan umeripoti kuwa wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) umewaachia huru wafanyakazi 9 wa sekta ya afya waliokuwa wakishikiliwa katika magareza na kikosi hicho huko Nyala makao makuu ya jimbo la Darfur Kusini. Hata hivyo kikosi cha RSF bado kinawashikilia wafanyakazi wengine wa afya 73.
-
Mashambulizi ya RSF yaua raia 16 eneo la Kordofan, Sudan
Dec 20, 2025 02:37Takriban watu 16 wameuawa katika shambulio la mizinga la waasi wa RSF lililolenga mji uliozingirwa katika eneo la Kordofan nchini Sudan, huku vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo vikiingia katika awamu hasasi kwenye mwaka wake wa tatu.
-
UN: Zaidi ya raia 1,000 waliuawa katika shambulio la RSF Darfur
Dec 18, 2025 11:52Ripoti iliyotolewa Alkhamisi na Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imesema zaidi ya raia 1,000 waliuawa wakati kundi la waasi wa Sudan lilipotwaa udhibiti wa kambi ya wakimbizi wa ndani huko Darfur nchini Sudan mwezi Aprili mwaka huu.
-
Takriban raia 2,000 waukimbia mji wa Heglig, Sudan baada ya kudhibitiwa na kikosi cha RSF
Dec 17, 2025 02:49Duru za habari ndani ya Sudan jana ziliarifu kuwa takriban raia 2,000 wameyaacha makazi yao katika mji wa Heglig wa magharibi mwa Sudan huko Kordofan Magharibi baada ya safari ngumu ya siku tisa ya kuhama makazi yao kufuatia kutekwa mji huo nawanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF).
-
UN yalaani shambulio lililoua askari 6 wa kulinda amani Sudan
Dec 14, 2025 02:36Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres ameeleza kusikitishwa na shambulio la ndege isiyo na rubani lililolenga kituo cha Umoja wa Mataifa nchini Sudan, na kuwaua askari sita wa kulinda amani wa umoja huo.
-
RSF yatuhumiwa kuhusika na mengi ya matukio 1,300 ya ukatili wa kingono katika vita vya Sudan
Dec 12, 2025 10:14Shirika moja la kutetea haki za wanawake limesema, limerekodi matukio yapatayo 1,300 ya vitendo vya ukatili wa kingono na kijinsia vilivyofanywa katika vita vya ndani nchini Sudan huku Kikosi cha Usaidizi wa Haraka (RSF) kikishutumiwa kuhusika na akthari ya vitendo hivyo.
-
Sudan Kusini yatuma wanajeshi kulinda eneo muhimu la mafuta la Heglig nchini Sudan
Dec 12, 2025 02:41Sudan Kusini imetuma wanajeshi wake katika nchi jirani ya Sudan kwa lengo kulinda kisima cha kimkakati cha mafuta cha Heglig karibu na mpaka. Haya yamebainishwa jana Alhamisi na Mkuu wa jeshi la nchi siku chache baada ya Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) kulidhibiti eneo hilo.
-
ICC imemhukumu kiongozi wa Janjaweed wa Darfur kifungo cha miaka 20 jela
Dec 09, 2025 11:35Majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) leo Jumanne wamemhukumu kiongozi wa wanamgambo wa Janjaweed katika jimbo la Darfur Sudan kifungo cha miaka 20 jela baada ya kupatikana na hatia ya kufanya ukatili katika jimbo la Darfur.
-
AU yalaani shambulio la RSF lililoua zaidi ya raia 100 katika mji wa Kalogi, kusini mwa Sudan
Dec 08, 2025 02:35Umoja wa Afrika, AU umelaani vikali mashambulizi ya ndege zisizo na rubani yaliyofanywa na Vikosi vya Usaidizi wa Haraka, RSF yaliyoua makumi ya watu wakiwemo watoto katika mji wa Kalogi kusini mwa Sudan.