-
Sudan Kusini yatuma wanajeshi kulinda eneo muhimu la mafuta la Heglig nchini Sudan
Dec 12, 2025 02:41Sudan Kusini imetuma wanajeshi wake katika nchi jirani ya Sudan kwa lengo kulinda kisima cha kimkakati cha mafuta cha Heglig karibu na mpaka. Haya yamebainishwa jana Alhamisi na Mkuu wa jeshi la nchi siku chache baada ya Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) kulidhibiti eneo hilo.
-
ICC imemhukumu kiongozi wa Janjaweed wa Darfur kifungo cha miaka 20 jela
Dec 09, 2025 11:35Majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) leo Jumanne wamemhukumu kiongozi wa wanamgambo wa Janjaweed katika jimbo la Darfur Sudan kifungo cha miaka 20 jela baada ya kupatikana na hatia ya kufanya ukatili katika jimbo la Darfur.
-
AU yalaani shambulio la RSF lililoua zaidi ya raia 100 katika mji wa Kalogi, kusini mwa Sudan
Dec 08, 2025 02:35Umoja wa Afrika, AU umelaani vikali mashambulizi ya ndege zisizo na rubani yaliyofanywa na Vikosi vya Usaidizi wa Haraka, RSF yaliyoua makumi ya watu wakiwemo watoto katika mji wa Kalogi kusini mwa Sudan.
-
Sudan yawatuhumu wanamgambo wa RSF kwa kuuwa raia 79 huko Kordofan Kusini
Dec 06, 2025 13:32Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan imewatuhumu wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) kuwa wameua raia 79 wakiwemo watoto 43 katika mauaji ya halaiki kwenye mji wa Kalogi katika jimbo la Kordofan Kusini.
-
UN: Kuna hatari ya kuzuka wimbi jipya la mashambulizi na janga la kibinadamu Kordofan, Sudan
Dec 05, 2025 02:57Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, ametoa indhari kuhusu hatari ya kuzuka wimbi jipya la ukatili katika eneo la Kordofan, Sudan, baada ya kushadidi mapigano kati ya Jeshi la Sudan (SAF), Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) na Kundi la Harakati ya Kaskazini ya Ukombozi wa Wananchi wa Sudan, (SPLM-N).
-
Madaktari Sudan watahadharisha kuhusu hatima ya watoto na wanawake waliokwama Kordofan magharibi
Dec 04, 2025 03:48Kundi la madaktari wa Sudan limesema kuwa lina wasiwasi mkubwa kuhusu hatima ya makumi ya watoto na wanawake katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi, baada ya mapigano kati ya jeshi la Sudan na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF).
-
Libya: Tutawatendea wakimbizi wa Sudan kama Walibya, watapatiwa huduma za skuli na hospitali
Dec 03, 2025 10:54Serikali ya Libya imetangaza kuwa itaongeza kasi ya kuwarejesha makwao wahamiaji wasio halali wa Kiafrika wa nchi za chini ya Jangwa la Sahara, lakini imesema, kwa upande wa wakimbizi wa Sudan watachukuliwa kama Walibya na kuruhusiwa kupata huduma za skuli na hospitali.
-
Ushahidi wa kwanza: Gesi ya klorini imetumika katika vita vya ndani Sudan
Nov 30, 2025 12:27Uchunguzi wa timu ya FRANCE 24 Observers unaonyesha namna gesi ya klorini ilivyotumika kama silaha katika vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea nchini Sudan.
-
Gavana wa Darfur: Katika kipindi cha siku tatu tu, RSF iliua Wasudan 27,000 El-Fasher
Nov 26, 2025 10:51Gavana wa Jimbo la Darfur nchini Sudan, Minni Arko Minnawi, ameviambia vyombo vya habari kuwa, katika kipindi cha siku tatu tu Wasudan 27,000 waliuliwa na Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) wakati wanamgambo wa vikosi hivyo walipoendeleza wimbi la mauaji baada ya kuuteka mji wa el-Fasher mwishoni mwa mwezi uliopita.
-
UN: Tangazo la RSF la kusitisha mapigano ni 'hatua katika mwelekeo sahihi'
Nov 26, 2025 07:13Umoja wa Mataifa umekaribisha kwa tahadhari tangazo la kibinadamu la kusitisha mapigano lililotolewa jana na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF), ukisema kuwa linawakilisha kupiga hatua lakini linahitaji kuidhinishwa kupitia hatua maidanini.