-
Jeshi la Sudan lavunja mzingiro wa miaka 2 wa wanamgambo wa RSF dhidi ya mji muhimu huko Kordofan
Jan 28, 2026 00:58Jeshi la Sudan limeeleza kuwa limevunja mzingiro wa karibu miaka miwili wa wanamgambo wa RSF katika mji muhimu katika mkoa wa Kordofan, na kudhibiti njia kuu za usafirishaji.
-
Makaburi ya umati ya Khartoum yafichua sura ya giza katika vita vya Sudan
Jan 26, 2026 03:08Makaburi mawili ya umati yenye mabaki ya miili ya maelfu ya watu yalipatikana hivi majuzi mjini Khartoum mji mkuu wa Sudan. Kupatikana kwa makaburi hayo kumefichua sura ya giza katika mzozo unaoendelea Sudan kati ya jeshi la taifa na wanamgambo wa kundi la Rapid Support Forces (RSF)
-
Mwendesha Mashtaka wa Sudan: Tumewafungulia kesi mamluki 122 wa kigeni
Jan 25, 2026 08:14Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Sudan ameeleza kuwa kesi za jinai zimefunguliwa dhidi ya takriban mamluki 122 wa kigeni wanaopigana bega kwa bega na wanamgambo waasi wa Rapid Support Forces (RSF), huku watoto 135 waliosajiliwa kama wapiganaji katika vita hivyo wakirejeshwa kwa familia zao.
-
Pande za kisiasa Sudan kuunda muungano mpya ili kurejesha utawala wa kiraia
Jan 24, 2026 09:34Makundi ya kisiasa ya Sudan ambayo yamejitenga na muungano mkuu wa demokrasia yamesema kuwa yanafanya juhudi za kuunda muungano mpana unaolenga kurejesha utawala wa kiraia nchini humo baada ya karibu miaka minne ya serikali inayoongozwa na jeshi.
-
Save the Children: Sudan inapitia kipindi kirefu zaidi cha kufungwa shule duniani
Jan 22, 2026 23:52Shirika la Save the Children limeonya kwamba vita vinavyoendelea nchini Sudan vimewanyima elimu watoto zaidi ya milioni 8, katika kile kinachoelezwa kama kipindi kirefu zaidi cha kufungwa shule duniani.
-
WFP: Familia nchini Sudan zinapitia kipindi kigumu kufuatia mizozo ya kikatili, njaa na uhaba wa fedha
Jan 15, 2026 23:23Familia nchini Sudan zinasukumwa ukingoni huku "migogoro ya kikatili" na njaa vikiendelea. Mpango wa Chakula Duniani (WFP) pia umetahadharisha kuwa oparesheni zake za kibinadamu za kunusuru maisha ya wananchi wa Sudan zinasusua kufuatia uhaba mkubwa wa fedha.
-
Misri: Umoja wa Sudan ni mstari mwekundu kwetu, hatutasita kuchukua kila hatua kuulinda
Jan 15, 2026 22:42Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Badr Abdelatty amesema, nchi yake itachukua hatua zote zinazohitajika ili kuhifadhi umoja wa ardhi ya Sudan, wakati nchi hiyo jirani inakaribia kuingia mwaka wake wa nne wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyohusisha vikosi vya jeshi SAF na vile vya usaidizi wa haraka, RSF.
-
Madaktari Sudan watahadharisha kuhusu maafa tarajiwa ya kibinadamu huko Kordofan Kusini
Jan 04, 2026 03:35Kundi la madakatri wa Sudan limetahadharisha kuhusu maafa tarajiwa ya kiafya na kibinadamu katika mji wa Dalang unaopatikana katika jimbo la Kordofan Kusini. Kundi hilo limesema kuwa mji wa Dalang unaendelea kuzingirwa huku ukikabiliwa na mashambulizi makali ya wanagambo wa RFS.
-
UN yakumbana na hali mbaya El Fasher katika ziara yake ya kwanza tangu mji huo udhibitiwe na RSF
Jan 01, 2026 07:43Umoja wa Mataifa umeripoti kuwa mji wa El- Fasher huko Darfur Magharibi nchini Sudan unapitia hali ya kutisha kwa binadamu.
-
Jeshi la Sudan lakomboa miji miwili ya Kordofan Kaskazini kutoka mikononi mwa RSF
Jan 01, 2026 02:16Jeshi la Sudan SAF limetangaza kuwa siku ya Jumatano lilirejesha udhibiti wa miji ya Kazgeil na Riyadh iliyoko kwenye jimbo la Kordofan Kaskazini baada ya mapigano na kundi la RSF.