-
Ushahidi wa kwanza: Gesi ya klorini imetumika katika vita vya ndani Sudan
Nov 30, 2025 12:27Uchunguzi wa timu ya FRANCE 24 Observers unaonyesha namna gesi ya klorini ilivyotumika kama silaha katika vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea nchini Sudan.
-
Gavana wa Darfur: Katika kipindi cha siku tatu tu, RSF iliua Wasudan 27,000 El-Fasher
Nov 26, 2025 10:51Gavana wa Jimbo la Darfur nchini Sudan, Minni Arko Minnawi, ameviambia vyombo vya habari kuwa, katika kipindi cha siku tatu tu Wasudan 27,000 waliuliwa na Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) wakati wanamgambo wa vikosi hivyo walipoendeleza wimbi la mauaji baada ya kuuteka mji wa el-Fasher mwishoni mwa mwezi uliopita.
-
UN: Tangazo la RSF la kusitisha mapigano ni 'hatua katika mwelekeo sahihi'
Nov 26, 2025 07:13Umoja wa Mataifa umekaribisha kwa tahadhari tangazo la kibinadamu la kusitisha mapigano lililotolewa jana na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF), ukisema kuwa linawakilisha kupiga hatua lakini linahitaji kuidhinishwa kupitia hatua maidanini.
-
Mamluki wa kigeni wana jukumu gani katika kuchochea vita nchini Sudan?
Nov 25, 2025 02:39Kamati ya Uchunguzi wa Haki za Binadamu imetangaza kuhusu ushirikiano uliopo kati ya mamluki wa kigeni na Vikosi vya Msaada wa Haraka vya Sudan RSF katika vita vya ndani nchini humo.
-
Jeshi la Sudan lakabiliana vikali na kikosi cha RSF huko Kordofan; raia wazidi kutaabika
Nov 23, 2025 13:03Jeshi la Sudan limekabiliana vikali mapiganoni dhidi ya wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) katika medani tofauti za vita huko Kordofan ya Kaskazini na Magharibi huku makumi ya maelfu ya raia wakiendelea kukimbia machafuko na mapigano yanayoshtadi kila uchao.
-
Ni ipi nafasi ya pande za kigeni katika mgogoro wa Sudan?
Nov 13, 2025 12:55Vita nchini Sudan vimechukua sura mpya kufuatia kuendelea uingiliaji kati wa nchi ajinabi nchini humo na kudhibitiwa mji wa Al Fasher na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF).
-
Shirika la Umoja wa Mataifa: Kuna Ushahidi wa matumizi ya kimfumo ya ubakaji nchini Sudan
Nov 12, 2025 07:39Shirika la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Wanawake limeonya kwamba kuna "ushahidi unaoongezeka kwamba ubakaji unatumika kwa makusudi na kwa utaratibu maalumu" nchini Sudan, huku njaa na ukosefu wa usalama wa chakula vikiendelea kutesa watu nchini humo.
-
IOM: Hatua za haraka zinahitajika ili kuwanusuru mamilioni ya raia walioathiriwa na vita Sudan
Nov 11, 2025 07:51Shirika la Kimataifa la Uhamaji (IOM) limetaka kuchukuliwa hatua za haraka ili kuwasaidia mamilioni ya raia walioathiriwa na vita vya Sudan kati ya jeshi la nchi hiyo na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF).
-
Mkurugenzi Mkuu wa WHO ataka kusitishwa umwagaji damu nchini Sudan
Nov 11, 2025 03:09Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) ametaka kusitishwa ghasia nchini Sudan baada ya kuuawa daktari katika mji ulioathiriwa na vita wa Al Fasher.
-
RSF imezika kwa halaiki na kuchoma moto maiti za mamia ya raia El-Fasher kuficha jinai za mauaji ya kimbari
Nov 10, 2025 06:18Mtandao wa Madaktari wa Sudan umeripoti kuwa, maiti za mamia ya raia zimezikwa katika makaburi ya pamoja na nyingine zimechomwa moto na Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) mjini El-Fasher magharibi mwa nchi hiyo.