-
Watu kadhaa waripotiwa kuuawa na kujeruhiwa Pemba, Tanzania katika ghasia za kabla ya upigaji kura ya mapema
Oct 27, 2020 04:50Watu kadhaa wanaoaminika kuwa wafuasi wa chama cha ACT Wazalendo wameripotiwa kuwa wameuawa na kujeruhiwa usiku wa kuamkia leo kisiwani Pemba, Zanzibar kabla ya kufanyika upigaji kura ya mapema ambao umezusha taharuki visiwani humo.
-
Wasimamizi wa uchaguzi Tanzania watakiwa kufuata sheria
Oct 20, 2020 04:13Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Tanzania (NEC) imewaagiza wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya majimbo kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria ili kuepuka malalamiko yanayoweza kusababisha uvunjifu wa amani.
-
Mpwa wa Rais wa Tanzania atishia 'kummaliza' Tundu Lissu kwa sindano ya sumu
Oct 18, 2020 10:43Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi CCM nchini Tanzania ametishia kumuua kwa kumdunga sindano ya sumu, mgombea urais wa nchi hiyo kwa tiketi cha Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Tundu Lissu kwa kile alichosema kuendelea 'kuwajaza upepo' wafuasi wake ili waandamane.
-
Ripoti ya matukio ya Kiislamu juma hili nchini Tanzania + SAUTI
Oct 16, 2020 12:46Viongozi wa dini Tanzania wakemewa na Baraza la Maulamaa la BAKWATA kwa kujihusisha na kuwapigia kampeni wagombea wa vyama vya siasa katika uchaguzi mkuu
-
Kauli ya Mufti wa Tanzania kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 28
Oct 16, 2020 03:58Sheikh mkuu na Mufti wa Tanzania Abubakari Zubeir amewataka watanzania kuhakikisha wanailinda amani ya nchi wakati huu ambapo taifa linaelekea kufanya uchaguzi mkuu.
-
Serikali ya Tanzania yatuhumiwa kubana na kukandamiza upinzani kuelekea uchaguzi wa Oktoba 28
Oct 12, 2020 10:26Serikali ya Rais John Pombe Magufuli wa Tanzania imetunga na kutekeleza sheria kali za kuogofya ili kukandamiza kila aina ya upinzani, wakati nchi hiyo inaelekea kwenye uchaguzi mkuu unaotazamiwa kufanyika tarehe 28 ya mwezi huu wa Oktoba.
-
Polisi visiwani Zanzibar yawaonya vikali wanasiasa 'wachochezi'
Oct 07, 2020 04:27Kamishna Mkuu wa Jeshi la Polisi Zanzibar nchini Tanzania amewatahadharisha wanasiasa dhidi ya kutoa matamshi ya kichochezi na uvunjifu wa amani visiwani humo, kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 28.
-
Tume ya Uchaguzi Tanzania yamfungia Lissu kufanya kampeni
Oct 02, 2020 10:56Kamati ya Maadili ya Kitaifa ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania (NEC) imemsimamisha mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, kufanya kampeni kwa muda wa siku saba, kwa madai ya kukiuka kanuni na taratibu za uchaguzi.
-
Magufuli asikitishwa na 'ajali' ya moto iliyoua wanafunzi 10 Tanzania
Sep 15, 2020 03:18Rais John Magufuli wa Tanzania ametuma salamu za rambirambi kwa uongozi wa Shule ya Kiislamu ya Byamungu iliyopo wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera kufuatia mkasa wa moto uliosababisha maafa. Rais Magufuli ametoa mkono wa pole kwa wazazi, ndugu, jamaa na marafiki wa wanafunzi 10 waliopoteza maisha katika ajali hiyo ya usiku wa kuamkia jana.
-
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania awasili Pemba kukabiliana na 'wachochezi'
Sep 04, 2020 02:33Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania Simon Sirro amewasili kisiwani Pemba, Zanzibar kwa ajili ya kile kilichotajwa kuwa kufanya vikao na vyama vya siasa na viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu wa mwezi ujao.