-
Vifo na wasiwasi wa wakimbizi katika safari ya kuelekea Ulaya
Dec 30, 2021 23:19Huku mizozo ya kisiasa na kiuchumi ikiendelea kupanuka Asia Magharibi na katika nchi nyingi za Afrika, wimbi la watu wanaotafuta hifadhi na wakimbizi barani Ulaya linaendelea kwa kasi kubwa.
-
Borell asisitiza ushirikiano wa masharti kati ya Brussels na Taliban
Dec 15, 2021 03:53Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amesema kuwa udharura wa kuwepo ushirikiana na kundi la Taliban lakini ushirikiano huo unapaswa kufanyika kwa masharti.
-
Umoja wa Ulaya: Hatutaitambua serikali ya Taliban Afghanistan
Nov 28, 2021 04:32Mkuu wa Kamisheni ya Umoja wa Ulaya amesisitiza kuwa umoja huo hautaitambua serikali ya kundi la Taliban inayotawala nchini Afghanistan.
-
Afrika Kusini yaikosoa UK kwa kusimamisha safari za ndege, kisa spishi mpya ya corona
Nov 27, 2021 01:08Afrika Kusini imeikosoa vikali serikali ya Uingereza kwa kupiga marufuku raia wa hiyo pamoja na nchi za Botswana, Namibia, Zimbabwe, Lesotho na Eswatini kuingia katika nchi hiyo ya Ulaya, kufuatia kugunduliwa spishi mpya ya corona kwa jina B.1.1.529 katika nchi hiyo ya kusini mwa Afrika.
-
Umoja wa Mataifa wakosoa vitendo vya mabavu vya nchi za Ulaya dhidi ya wakimbizi
Nov 13, 2021 08:19Akizungumza katika bunge la Ulaya Filippo Grandi Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR amekosoa vitendo vya mabavu na ukandamizaji wa Umoja wa Ulaya dhidi ya wakimbizi na kusisitiza kuwa siku zote na mara kwa mara tunashuhudia raia wanaotafuta hifadhi barani Ulaya wakifukuzwa kwa mabavu na visingizio vya kisheria kutumika katika kuwanyima hifadhi raia hao.
-
Kupamba moto mgogoro wa wakimbizi barani Ulaya
Nov 11, 2021 07:10Kwa mara nyingine tena, wimbi la wakimbizi wanaomiminika kwenye mipaka ya nchi za Ulaya limeongezeka na kuwa mgogoro mkubwa. Nchi za Ulaya zimeamua kufunga mipaka yao ili kukabiliana na wimbi kubwa la wakimbizi wapya.
-
Mtaalamu wa WHO: Ulaya inaweza kukumbwa na vifo vingine vya corona laki tano
Nov 04, 2021 20:25Kiwango cha sasa cha maambukizi ya corona barani Ulaya kinatia wasiwasi mkubwa na bara hilo linaweza kukumbwa na vifo vingine laki tano vya corona ifikapo mapema mwakani. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa WHO barani Ulaya.
-
Kukosoa Uturuki utendaji wa Umoja wa Ulaya ulio dhidi ya Uislamu
Nov 04, 2021 20:23Ukosoaji mtawalia wa viongozi wa Uturuki dhidi ya Umoja wa Ulaya hususan sera za chuki dhidi ya Uislamu za umoja huo, zinapaswa kutathminiwa kama juhudi za Ankara za kukabiliana na sera za madola ya Magharibi dhidi ya serikali ya Rais Recep Tayyip Erdogan na kuimarisha wenzo wa kuishinikiza jumuiya hiyo ya Ulaya.
-
Madai ya Ufaransa kuhusu miradi ya nyuklia ya Iran, kuendelezwa sera za kindumakuwili za Ulaya
Oct 23, 2021 22:55Sambamba na mkutano wa Ijumaa ya wiki hii baina ya wawakilishi wa Marekani na nchi za Ulaya uliofanyika mjini Paris, Ufaransa imeitaka Iran ipunguze shughuli zake za kuzalisha nishati ya nyuklia.
-
Ungamo la Josep Borrell la kupungua ushawishi wa Umoja wa Ulaya
Oct 12, 2021 08:32Hatua ya Umoja wa Ulaya ya kuifuata kibubusa Marekani imeitilia alama ya swali utendaji na mamlaka ya uchukuaji maamuzi ya umoja huo katika medani za kimataifa.