Wimbi la pili la maandamano na harakati ya malalamiko ya wananchi nchini Bahrain kwa mnasaba wa mwaka wa saba wa mapinduzi ya tarehe 14 Februari, limeanza jioni ya leo Jumatano katika maeneo tofauti ya nchi hiyo ya Kiarabu.
Mahakama ya Jinai ya Bahrain leo imeendeleza sera kandamizi za utawala wa kiimla wa Aal Khalifa kwa kuwahukumu adhabu ya kifo, kifungo cha maisha jela na kuwavua uraia makumi ya raia wa nchi hiyo.
Mkuu wa Kituo cha Haki za Binadamu cha nchini Bahrain amesema kuwa hukumu zilizotolewa na mahakama dhidi ya wapinzani nchini humo ni za kisiasa na ulipizaji kisasi.
Utawala wa kiimla wa Bahrain unaendelea kutumia wanajeshi wake kuwakandamiza wananchi wanaoandamana kwa amani wakitaka utawala wa demokrasia katika nchi hiyo ndogo ya Ghuba ya Uajemi.
Sheikh Abdullah al Daqaq mwakilishi wa Baraza la Maulama la Bahrain na ambaye pia ni mwakilishi wa Ayatullah Sheikh Issa Qassim wa nchi hiyo amesisitiza hapa Tehran juu ya umuhimu wa kuwa na umoja katika hali ya hivi sasa katika ulimwengu wa Kiislamu na kueleza kuwa Waislamu wanahitajia umoja ili kuzifukuza Marekani na Israel katika eneo.
Mjumbe mwandamizi wa Umoja wa Maulamaa wanaounga mkono Muqawama amesema hatua za utawala wa Bahrain dhidi ya kiongozi wa kidini wa nchi hiyo Ayatullah Sheikh Isa Qassim ni sawa na kumuua mwanazuoni huyo wa Kiislamu kwa njia isiyo ya moja kwa moja.
Duru zenye uhusiano na familia ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kitaifa ya al-Wifaq nchini Bahrain, zimeeleza kuwa utawala wa Aal-Khalifa umemwekea vizuizi vikubwa Sheikkh Ali Salman na shakhsia wengine mashuhuri wanaoshikiliwa katika jela za nchi hiyo.
Shaikh Hussain Al Daihi, Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya al-Wifaq ya nchini Bahrain amesema kuwa, tuhuma dhidi ya Sheikh Ali Salman, Katibu Mkuu wa harakati hiyo, ni za kubuni na ni za kulipiziana kisasi Bahrain na Qatar.
Utawala wa Aal Khalifa umeweka sheria kali za usalama nchini Bahrain sambamba na kukaribia mwezi mtukufu wa Muharram.
Wizara ya Ulinzi ya Marekani Pentagon imetangaza kuwa, nchi hiyo imeafiki mpango wa kuuzia silaha utawala wa kifalme wa Bahrain wa Aal Khalifa wenye thamani ya takribani dola bilioni nne na ambao unajumuisha ndege za kivita aina ya F-16, makombora na boti za doria.