May 07, 2017 14:27
Kwa mara nyingine tena na kama ilivyotarajiwa, utawala wa kidikteta wa Aal-Khalifa nchini Bahrain, umeahirisha tena kesi ya Sheikh Isa Qassim, Kiongozi wa ngazi ya juu wa kidini nchini Bahrain kutokana na hofu ya kushindwa kudhibiti hali ya mambo nchini ikiwa utatoa hukumu dhidi yake.