-
Kuongezeka hasira za kimataifa kuhusu jinai za utawala wa Kizayuni huko Gaza
Nov 11, 2023 23:37Sambamba na kuendelea vitendo vya jinai vya utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Gaza, ambavyo hadi sasa vimepelekea kuuawa shahidi zaidi ya Wapalestina elfu 11 na kujeruhiwa wengine zaidi ya elfu 27, hasira na ukosoaji wa kimataifa unaendelea kuongezeka kwa kadiri kwamba mbali na maandamano makubwa yanayofanyika katika pambe tofauti za dunia, baadhi ya wanasiasa wa Magharib pia wanaukosoa utawala huo kutokana na ukatili wake wa kutisha dhidi ya Wapalestina wasio na hatia.
-
Nukta tano muhimu katika barua ya Islami kwa Grossi kuhusiana na tishio la utawala wa Kizayuni kutumia bomu la nyuklia dhidi ya Ghaza
Nov 11, 2023 07:32Katika barua yake kwa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA, Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran amelitaka shirika hilo kulibainishia wazi Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, hatari zinazoweza kusababishwa na matumizi au tishio la matumizi ya silaha za nyuklia za utawala wa Kizayuni dhidi ya wananchi wa Palestina.
-
Idadi ya wanajeshi wa Kizayuni walioangamizwa yafika 365
Nov 11, 2023 03:30Idadi ya askari na maafisa wa jeshi la utawala ghasibu wa Israel waliouawa tangu tarehe 7 Oktoba hadi sasa imefika 365.
-
Netanyahu akataa ombi la Biden la kusitisha mapigano kwa siku 3 huko Gaza
Nov 08, 2023 22:48Rais Joe Biden wa Marekani amemtaka Benjamin Netanyahu Waziri Mkuu wa Israel asitishe mapigano kwa siku tatu ili kutatua suala la mateka. Kuhusiana na jambo hilo, Biden amesema katika mazungumzo ya simu yaliyofanyika siku ya Jumanne alimuomba Benjamin Netanyahu asitishe mapigano ili kuandaa uwanja wa kushughulikiwa suala la mateka wa Israel.
-
Siku ya 33 ya vita Gaza; waliouawa shahidi kwa mashambulio ya kinyama ya Israel wafikia 10,569
Nov 08, 2023 08:55Wizara ya Afya ya Palestina imetangaza kuwa idadi ya waliouawa shahidi kutokana na mashambulio ya kinyama ya utawala wa Kizayuni katika eneo hilo imeongezeka na kufikia 10,569.
-
Marekani na kukana mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Gaza
Nov 07, 2023 23:11Zaidi ya mwezi mmoja umepita sasa tangu kuanza kwa vita vya Gaza na tangu kutekelezwa kwa operesheni ya "Kimbunga cha Al-Aqsa" huku utawala wa Kizayuni unaoendesha operesheni za ardhini katika Ukanda wa Gaza dhidi ya wapiganaji wa Hamas ukizidisha mashambulizi yake ya anga dhidi ya eneo hilo. Mashambulio hayo ya kinyama ya Israe; yameendelea kusababisha mauaji makubwa ya watu wanaodhulumiwa wa Ukanda wa Gaza.
-
Kuongezeka upinzani dhidi ya vitendo vya kijinai vya utawala wa Kizayuni katika nchi za Magharibi
Nov 06, 2023 23:01Mwezi mmoja ukiwa umepita tangu kujiri operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa na utawala wa Kizayuni kuanzisha mashambulizi makali ya mabomu ambayo hajawahi kushuhudiwa tena huko Ghaza, ambayo yamepelekea kuuawa shahidi na kujeruhiwa makumi ya maelfu ya Wapalestina, wengi wao wakiwa ni watoto na wanawake, mwenendo wa upinzani dhidi ya vitendo hivyo vya jinai vya Israeli, umeongezeka sana duniani ikiwa ni pamoja na nchini Marekani, ambayo ni mwitifaki mkubwa wa Tel Aviv.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Mashinikizo ya kisiasa yazidishwe dhidi ya Marekani na utawala wa Kizayuni
Nov 06, 2023 10:49Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza udharura wa kuongezeka mashinikizo ya kisiasa ya Ulimwengu wa Kiislamu dhidi ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel ili kusimamisha mauaji yanayofanywa dhidi ya watu wa Gaza na kusema: Iraq, ikiwa nchi muhimu katika eneo la Magharibi mwa Asia, inaweza kuwa na nafasi maalumu katika uwanja huu na kuanzisha mstari mpya katika ulimwengu wa Waarabu na wa Kiislamu.
-
Hitilafu kati ya Warepublican and White House kuhusu msaada kwa Israel na Ukraine
Nov 04, 2023 22:55Katika hali ambayo serikali ya Biden imetangaza kuunga mkono kikamilifu jinai za utawala wa Kizayuni huko Ukanda wa Ghaza na hata kupinga usitishaji vita, lakini suala la msaada wa kifedha kwa Israel ambalo linatiliwa maanani na Warepublican sambamba na mtazamo wa White ambayo inataka kutolewa kwa wakati mmoja misaada ya fedha na silaha kwa Ukraine limezusha hitilafu kubwa kati ya Kongresi na White House.
-
Kan'ani: Marekani imezitoa muhanga haki za binadamu kwa maslahi ya Israel
Nov 03, 2023 04:36Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema: Marekani na nchi chache zimeuteka Umoja wa Mataifa na kutoa muhanga amani na usalama wa kimataifa kwa ajili ya maslahi ya utawala wa kibaguzi, ghasibu na unaotenda jinai wa Israel.