-
Shujaa wa Iran aunga mkono uamuzi wa serikali ya Indonesia wa kuzuia timu ya Israel kuingia mjini Jakarta
Apr 02, 2023 04:25Mshindi wa medali ya dhahabu katika Michezo ya Para-Asia 2018 mjini Jakarta ametoa medali yake kwa watu wa Indonesia ili kuunga mkono hatua ya serikali ya nchi hiyo ya kuzuia timu ya soka ya Israel kuingia mjini Jakarta.
-
Hamas: Jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel hazitapita bila jibu
Apr 02, 2023 04:24Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imelaani mauaji yanayofanywa na askari wa utawala haramu wa Israel dhidi ya vijana wa Kipalestina katika Msikiti wa Al-Aqsa na kutangaza kuwa uhalifu huo hautapita bila kujibiwa.
-
Hamas yalaani kuwepo baadhi ya wanasiasa wa Kiarabu katika mkutano wa mapatano na Wazayuni
Apr 01, 2023 23:35Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina "HAMAS" imelaani vikali kuwepo kwa shakhsia wa Kiarabu na Kiafrika katika mkutano wa kuhalalisha uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel na kutoa wito wa kulaaniwa kitendo hicho sambamba na kutambuliwa kuwa ni kosa la jinai.
-
Amnesty International yakosoa undumakuwili wa nchi za Magharibi katika uwanja wa haki za binadamu
Mar 29, 2023 06:50Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limekosoa vikali misimamo ya undumakuwili na ya kinafiki ya nchi za Magharibi katika kushughulikia ukiukwaji wa haki za binadamu katika nchi zinazopinga sera za nchi za Magharibi na kulegeza msimamo laini wa nchi hizo kwa baadhi ya washirika wao ukiwemo utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Jihadul-Islami yatoa wito Wapalestina wote wazatitiwe kwa silaha kujibu mapigo kwa wazayuni
Mar 29, 2023 03:40Harakati ya Jihadul-Islami ya Palestina imewasilisha kwa wawakilishi wa makundi mengine ya mapambano ya Palestina mpango wa kuwapa silaha Wapalestina wote ili kukabiliana na mpango wa Itamar Ben Guer, waziri wa usalama wa ndani wa utawala haramu wa Israel kuhusu kuwapatia silaha walowezi wa Kizayuni.
-
Kanaani: Hasira za Netanyahu na Sunak kuhusu mabadiliko ya Asia Magharibi sio jambo ajabu
Mar 25, 2023 09:47Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuuri ya Kiislamu ya Iran, amejibu matamshi yaliyotolewa na Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni, Benjamin Netanyahu na mwenzake wa Uingereza, Rishi Sunak dhidi ya Iran ya Kiislamu katika mkutano wao hapo jana na kueleza kwamba, si jambo la kushangazwa kutolewa matamshi kama hayo na mawaziri hao.
-
Uamuzi madhubuti wa bunge la Jordan wa kumfukuza balozi wa Israel.
Mar 24, 2023 03:45Mvutano umeibuka katika uhusiano wa Amman na Tel Aviv kufuatia uamuzi imara wa Bunge la Jordan wa kumfukuza balozi wa utawala wa Kizayuni wa Israel nchini humo.
-
Ubaguzi wa rangi wa baraza la mawaziri la Netanyahu na hasira ya serikali ya Jordan
Mar 23, 2023 22:50Matamshi ya karibuni ya mmoja wa mawaziri wa baraza lenye misimamo ya kupindukia mipaka la Benhamini Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel yameikasirisha serikali ya Jordan. Misimamo mikali na ya ubaguzi wa rangi ya baraza hilo hadi sasa imeugharimu pakubwa utawala huo kieneo na kimataifa.
-
Kuendelea ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni kusini mwa Quds Tukufu
Mar 23, 2023 04:33Meya wa mji mtakatifu wa Quds ametoa idhini ya kujengwa vitongoji vipya vya walowezi wa Kizayuni katika mji huo, jambo ambalo linaenda kinyume na maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Bunge la Jordan lapasisha pendekezo la kutimuliwa balozi wa Israel mjini Amman
Mar 22, 2023 09:04Wawakilishi wa Bunge la Jordan wamepigia kura ya ndio pendekezo la kufukuzwa balozi wa utawala haramu wa Israel huko Amman wakilalamikia na kupinga hatua ya waziri wa fedha katika serikali ya mrengo wa kulia ya Israel, ambaye alizua utata mapema wiki hii.