Imarati na jitihada za kujinasua katika kinamasi cha vita huko Yemen
Msemaji wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amesema Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) unajaribu kila uwezavyo ili kujinasua kwenye kinamasi cha vita huko Yemen; ambapo sasa imeebainika kuwa nchi hiyo tayari imeanza kufanya juhudi kubwa katika uwanja huo.
Msemaji wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amesema Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) unajaribu kila uwezavyo ili kujinasua kwenye kinamasi cha vita huko Yemen na tayari imeanza kufanya juhudi kubwa katika uwanja huo.
Msemaji wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran ameshiria juhudi zinazofanywa na Saudia za kuzivuta nchi nyingine za Mashariki ya Kati kujiunga katika vita vya Yemen na kueleza kuwa, jitihada hizo hazijazaa matunda. Amesema kinyume chake, nchi nyingi hazijajiunga na muungano huo na baadhi yao kama Qatar zimejitoa katika muungano huo vamizi huko Yemen na zilizobaki zimejutia jambo hilo.

Sayyid Hussein Naqavi Husseini amesema kuwa vita dhidi ya watu wanaodhulumiwa wa Yemen vimeifanya Imarati ikabiliwe na vitisho chungu nzima na havijakuwa na na manufaa yoyote kwa nchi hiyo licha ya gharama zake kubwa.
Saudia ilianzisha vita dhidi ya taifa la Yemen mwezi Machi mwaka 2015 ikiungwa mkono na Marekani, Imarati na nchi nyingine kadhaa na hadi sasa Wayemeni zaidi ya elfu 16 wameuawa, makumi ya maelfu wamejeruhiwa na mamilioni ya wengine wamekuwa wakimbizi kutokana na vita hivyo.