24
Sibtain katika Qur'ani na Hadithi
Assalaam Alaikum wapenzi wasikilizaji wa Idhaa ya Kiswahili, Sauti ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inayokutangazieni kutoka mjini Tehran, na karibuni kusikiliza sehemu nyingine ya kipindi hiki cha Sibtain katika Qur'ani na Hadithi. Mwenyezi Mungu alipowaumba Manabii, Mitume na Maimamu waongofu kwa ajili ya kuwaongoza wanadamu, aliwapa watukufu hao uwezo, fadhila na vipawa maalumu kwa ajili ya kufikia lengo hilo la kuwaongoza wanadamu kwenye njia nyoofu.