Assalaam Alaykum wapenzi wasikilizaji wa Idhaa ya Kiswahili, Sauti ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inayokutangazieni kutoka mjini Tehran. Katika vipindi viwili vilivyopita tulichunguza na kujadili Aya za 38 hadi 41 za Surat al-Haj na Hadithi zinazozifasiri kwa kwina Aya hizo ambapo tulifahamu kwamba wale watu walioruhusiwa kupigana Jihadi na Mwenyezi Mungu kujilazimisha kuwanusuru kutokana na hilo, ni kundi maalumu la waja wake waumini ambao wamepambika kwa sifa ya kuwa na ikhlasi ya hali ya juu