Assalaam Aleikum wasikilizaji wapenzi wa Idhaa ya Kiswahili, Sauti ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inayokutangazieni kutoka mjini Tehran. Tuna furaha kukutana nanyi tena katika sehemu hii ya 14 ya kipindi hiki cha Aya na Hadithi, ambayo itazungumzia Aya takatifu na Hadithi tukufu ambazo zinamtahadharisha mwanadamu dhidi ya kujishughulisha na mambo yanayompelekea kumsahau Muumba wake na matokeo mabaya ya jambo hilo.