Feb 03, 2019 08:26
Ni matumaini yangu kuwa, hamjambo wapenzi wasikilizaji popote pale yanapokufikieni matangazo haya ya Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hususan huko nyumbani Afrika Mashariki. Katika siku hizi, wananchi wa Iran wanaendelea na sherehe za Alfajiri Kumi katika kona zote za nchi kwa ajili ya kuadhimisha miaka 40 ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya mwaka 1979 nchini Iran.