-
Usalama wa kikanda; ajenda ya mazungumzo ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Algeria na Libya
Apr 20, 2021 07:59Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria jana Jumatatu alikutana na mwenzake wa Libya na kufanya mazungumzo kuhusu usalama wa kikanda na kuziunga mkono pande za Libya kwa lengo la kuupatia ufumbuzi mgogoro wa kisiasa wa nchi hiyo.
-
Mshauri wa Rais wa Algeria: Ufaransa ilieneza ujinga nchini zama za ukoloni
Apr 19, 2021 11:21Mshauri wa Rais wa Algeria amesema kuwa Ufaransa ilifanya kazi ya kueneza ujinga wa kutojua kusoma na kuandika wakati wa ukoloni wa nchi hiyo nchini Algeria.
-
Maelfu waandamana dhidi ya serikali nchini Algeria
Apr 17, 2021 06:03Maelfu ya watu wamefanya maandamano katika miji mbalimbali ya Algeria wakitaka kuachiwa huru wanaharakati wa kisiasa na kutoa wito wa kususiwa uchaguzi mkuu wa mapema wa Bunge nchini humo.
-
Algeria: Ufaransa itaendelea milele kuwa adui wa taifa letu
Apr 11, 2021 03:37Waziri wa Kazi wa Algeria ametoa taarifa rasmi na huku akiashiria ripoti zilizofichua kwamba Ufaransa ilifanya majaribio ya nyuklia katika ardhi ya Algeria amesema, mkoloni huyo wa Ulaya ataendelea daima na milele kuwa adui wa taifa letu, kama ambavyo hivi sasa pia Ufaransa ni adui mkongwe na wa zamani sana wa Algeria.
-
Kuendelea mgogoro nchini Algeria; kususiwa uchaguzi wa Bunge na vyama vya siasa
Apr 07, 2021 02:34Mgogoro wa kisiasa nchini Algeria ungali unaendelea kufukuta kwani licha ya juhudi za serikali za kutuliza hali ya mambo na kuitisha uchaguzi wa Bunge wa mapema, lakini vyama vinne vya siasa vya nchi hiyo vimetangaza kususia uchaguzi huo.
-
Mtetemeko mkubwa wa ardhi waikumba Algeria mapema leo afajiri
Mar 18, 2021 07:14Mtetemeko mkubwa wa ardhi wenye ukubwa wa daraja 6 kwa kipimo cha rishta umetokea katika eneo la kaskazini mashariki mwa mji wa Bejaia, katika umbali wa kilomita 10 chini ya ardhi huko Algeria.
-
Maandamano yafanyika nchini Algeria kwa wiki ya pili mfululizo
Mar 07, 2021 08:21Maelfu ya raia wa Algeria wamefanya maandamano kwa wiki ya pili mfululizo kulalamikia siasa za serikali ya nchi hiyo.
-
Kuvunjwa Bunge na mwanzo wa kipindi kipya cha kisiasa nchini Algeria
Feb 20, 2021 10:17Katika miaka ya karibuni Algeria imekumbwa na misukosuko na matukio mengi ya kisiasa. Tukio la karibuni kabisa nihatua ya Rais Abdelmadjid Tebboune wa nchi hiyo ya kulivunja Bunge na kuitisha uchaguzi wa mapema. Tebboune alitangaza hatua hiyo Alkhamisi iliyopita katika hotuba yake kwa taifa iliyotolewa kwa mnasaba wa maadhimisho ya Siku ya Taifa ya Shahidi.
-
Bunge la Algeria lavunjwa; rais aitisha uchaguzi
Feb 19, 2021 07:07Rais wa Algeria ameagiza kuvunjwa bunge la nchi hiyo. Rais Abdul Majid Tebboune wa Algeria jana usiku alisema kuwa amelivunja bunge ili kuendesha uchaguzi pasina ufisadi na kuandaa fursa za ajira kwa ajili ya nguvu kazi ya vijana nchini humo.
-
Maelfu ya wapinzani waandamana Algeria kuunga mkono harakati ya Hirak
Feb 17, 2021 07:58Maelfu ya watu waliandamana jana katika mji wa Kherrata nchini Algeria kuunga mkono Harakati ya Hirak ambayo ilimuondoa madarakani rais mkongwe Abduaziz Bouteflika mwaka 2019. Maandamano hayo yalisitishwa baada ya kuanza maambukizi ya COVID-19 mwaka jana.