-
Biden: Trump ni rais fisadi zaidi katika historia ya sasa ya Marekani
Jul 12, 2020 23:38Mgombea urais wa Marekani kwa tiketi ya chama cha Democrat amesema, Donald Trump ni rais fisadi zaidi katika historia ya sasa ya nchi hiyo kwa namna anavyotumia vibaya mamlaka yake kwa ajili ya kuwanufaisha watu wake wa karibu.
-
Tishio jipya la Donald Trump dhidi ya Venezuela
Jul 12, 2020 08:05Katika hali ambayo siasa za chuki na hasama za Marekani dhidi ya Venezuela hadi sasa zimeshindwa na kugonga mwamba, Rais Donald Trump kwa mara nyingine tena ametoa matamshi ya vitisho kwa kusema: Kuna mambo yatatokea kuhusiana na Venezuela.
-
Wasomi, wanachuo wa Kenya nchini Marekani wakosoa agizo la Trump dhidi yao
Jul 11, 2020 10:18Wahadhiri na wanachuo raia wa Kenya walioko Marekani wamekosoa vikali agizo lililotolewa na rais wa nchi hiyo, Donald Trump, la kutaka wanafunzi wote wa kigeni waondoke nchini humo ndani ya miezi miwili ijayo.
-
Kujiondoa rasmi Marekani katika Shirika la Afya Duniani WHO
Jul 09, 2020 04:51Msimamo wa serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani ni kupuuza, kukosoa, kutoa vitisho na hatimaye kujitoa katika mashirika ya kimataifa na hasa yale yanayopinga matakwa na maslahi haramu ya nchi hiyo na ya washirika wake na hasa utawala haramu wa Israel.
-
Sisitizo la Umoja wa Mataifa la kukiuka sheria mauaji dhidi ya Luteni Jenerali Qassem Soleimani
Jul 08, 2020 02:02Mnamo Januari 3 mwaka huu, jeshi la kigaidi la Marekani kwa amri ya Rais wa nchi hiyo Donald Trump lilitenda jinai kwa kumuua kidhulma Luteni Jenerali Qassem Soleimani aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran akiwa uraiani nchini Iraq tena akiwa mgeni rasmi wa serikali ya Baghdad.
-
Associated Press: Wakuruba wa Trump wamepora mabilioni ya dola za corona
Jul 06, 2020 22:00Kundi moja la ukaguzi nchini Marekani limefichua kwamba watu wa karibu na Rais Donald Trump wa nchi hiyo wamepora na kutafuna mabilioni ya dola zilizokuwa zimetengwa kama bajeti ya kuwasaidia waathirika wa virusi vya corona.
-
Trump ajifanya tena daktari bingwa wa corona; FDA yaja juu
Jul 06, 2020 03:17Shirika la Chakula na Madawa la Marekani FDA limekosoa vikali matamshi mapya ya rais wa nchi hiyo, Donald Trump aliyedai kuwa asilimia 99 ya kesi za corona hazina hatari yoyote na kusema kuwa madai hayo si sahihi hata kidogo.
-
Waandamanaji wateketeza bendera ya Marekani nje ya White House baada ya hotuba ya Trump
Jul 05, 2020 03:18Waandamanaji waliokuwa na hasira waliteketeza moto bendera ya Marekani nje ya Ikulu ya White House mjini Washington baada ya hotuba ya Rais Donald Trump kwa mnasaba wa siku ya 'uhuru' wa nchi hiyo jana Julai nne.
-
Faili la kuuawa Qassim Soleimani: Iran yatoa waranti wa kutiwa mbaroni Trump
Jun 29, 2020 23:16Mwendesha Mashtaka wa Tehran ametoa waranti wa kutiwa mbaroni watu 36 akiwemo Rais Donald Trump wa Marekani wakihusishwa na mauaji ya aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) Luteni Jenerali Shahid Qassem Soleimani.
-
Ukosoaji wa Putin kwa hatua za upande mmoja za Magharibi chini ya uongozi wa Marekani
Jun 29, 2020 22:03Njama za nchi za Magharibi za kutaka kuyatwisha mataifa mengine shabaha na malengo yake zimekumbwa na upinzani wa nchi nyingine duniani. Hasa ikitiliwa maanani kuwa nchi za Magharibi hususan Marekani siku zote zimekuwa zikitaka kuidhibiti dunia na kutwisha misimamo na hatua zake za upande mmoja duniani.