-
Trump azidi kuandamwa kwa uzembe aliofanya kuhusu COVID-19
Jun 29, 2020 03:45Wananchi wa matabaka mbalimbali nchini Marekani wameendelea kumshambulia na kumlaumu vikali rais wa nchi hiyo, Donald Trump kwa uzembe alioufanya wa kushindwa kuchukua tahadhari na hatua zinazotakiwa za kukabiliana na ugonjwa hatari wa corona.
-
Jitihada za Marekani za kuishawishi Ulaya iungane na Washington dhidi ya China
Jun 27, 2020 22:03Marekani katika kipindi cha utawala wa Rais Donald Trump imezididisha mienendo yake ya kukabiliana na China katika nyuga mbalimbali. Mbali na kutaka kuitwisha Beijing matakwa yake katika nyanja za kibiashara na kiuchumi, sasa Marekani inaingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo hususan katika maeneo mawili ya Hong Kong na Xinjiang kwa kisingizio cha haki za binadamu.
-
Biden: Trump amekuwa kama mtoto katika kukabiliana na corona, Wamarekani milioni 25 wamepatwa na corona
Jun 26, 2020 04:21Mgombea wa kiti cha rais wa Marekani kwa tiketi ya chama cha Democratic amesema kuwa Rais Donald Trump amekuwa na mwenendo kama wa mtoto mdogo katika kukabiliana na virusi vya corona.
-
Dunia nzima dhidi ya Trump; walimwengu walaani vikwazo vya Marekani dhidi ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu
Jun 25, 2020 01:56Mojawapo na sifa kuu za utawala wa Donald Trump huko Marekani ni sera na mtazamo mbaya wa kiongozi huyo kuhusiana na jumuiya na mashirika ya kikanda na kimataifa. Hatua ya karibuni zaidi ya Trump dhidi ya jumuiya za kimataifa ni vikwazo alivyoweka kwa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) ambayo ndicho chombo cha juu zaidi cha kimataifa chenye jukumu la kushughulikia uhalifu wa kivita na jinai zinazofanywa dhidi ya binadamu.
-
NYT: Trump anamsaka mtu aliyevujisha habari ya kujificha kwake chini ya handaki ya White House
Jun 19, 2020 03:47Rais Donald Trump wa Marekani anamsaka kwa udi na uvumba mfanyakazi wa White House aliyevujisha habari ya kukimbilia kwake kwenye handaki iliyoko chini ya ardhi ya White House wakati wa kilele cha maandamano makali ya kupinga ubaguzi wa rangi nchini Marekani wiki kadhaa zilizopita.
-
Trump aiomba China imsaidie kushinda uchaguzi mkuu ujao
Jun 18, 2020 04:01Mshauri wa zamani wa usalama wa taifa wa Marekani, John Bolton amesema katika kitabu chake kipya kwamba Rais Donald Trump wa nchi hiyo aliiomba China imsaidie katika kushinda uchaguzi mkuu wa rais uliopangwa kufanyika baadaye mwaka huu.
-
Amri mpya ya Trump yaidhinisha kuendelea ukatili wa polisi ya Marekani
Jun 18, 2020 02:53Ukatili na utumiaji mabavu usio na mipaka wa polisi ya Marekani dhidi ya watu wenye asili ya Afrika ambao unatekelezwa katika sera jumla ya ubaguzi wa rangi umeubia maandamano ambayo hayajawahi kushuhudiwa Marekani. Hali hiyo imempelekea rais mwenye utata wa nchi hiyo, Donald Trump, kutoa amri mpya ya kile alichodai kuwa ni mabadiliko katika muundo wa polisi nchini humo.
-
Malalamiko ya Ujerumani kwa vitisho vya Marekani dhidi ya usalama wa nishati barani Ulaya
Jun 15, 2020 03:30Baada ya Donald Trump kuingia katika Ikulu ya Marekani, White House, uhusiano wa Washington na Umoja wa Ulaya ikiwemo Ujerumani umevurugika na kufikia kiwango cha chini kabisa. Uhusiano huo umezidi kuwa mbaya baada ya Trump kuzungumzia suala la kuondoa wanajeshi wa Marekani huko Ujerumani.
-
Trump akosolewa kwa kuitisha mkutano wa kisiasa wakati huu wa corona
Jun 15, 2020 02:25Rais Donald Trump wa Marekani amekosolewa vikali na wataalamu wa afya nchini humo kwa kuitisha mkutano wa kisiasa kwa ajili ya kujipigia debe kuelekea uchaguzi mkuu wa mwishoni mwa mwaka huu, licha ya ugonjwa wa COVID-19 kuendelea kuua mamia ya Wamarekani kila siku.
-
Israel kujenga 'vitongoji 300 vya Trump' katika Milima ya Golan, Syria
Jun 15, 2020 02:23Utawala ghasibu wa Israel unapanga kujenga mamia ya vitongoji vipya vya walowezi wa Kizayuni katika Miinuko ya Golan nchini Syria, vitakavyoitwa "Miinuko ya Trump".