-
Pendekezo jipya kwa Israel na Hamas la kusimamisha mapigano kwa miezi minne
Jan 29, 2024 02:51Shirika la habari la Anadolu la Uturuki limelinukuu Jarida la Wall Street Journal na kuripoti kuwa nchi patanishi zimewasilisha pendekezo la kusitisha mapigano kwa miezi 4 kati ya harakati ya Hamas na utawala wa Kizayuni ikiwa ni pamoja na kuachiwa huru mateka wote wa upande wa utawala wa Kizayuni.
-
HAMAS: Netanyahu anataka kurefusha vita vya Gaza kwa malengo ya kisiasa
Jan 28, 2024 23:34Mwanachama mwandamizi wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kundi hilo la muqawama linataka usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza, lakini Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel, Benjamin Netanyahu anataka vita hivyo viendelee kutokana na sababu zake binafsi na za kisiasa.
-
WSJ: 80% ya handaki za HAMAS huko Gaza zingali zinafanya kazi
Jan 28, 2024 09:55Gazeti la Wall Street Journal la Marekani limeripoti kuwa, asilimia 80 ya njia za chini kwa chini za Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS katika Ukanda wa Gaza zingali zinafanya kazi, licha ya mashambulizi ya kinyama ya utawala wa Kizayuni dhidi ya eneo hilo lililozingirwa, tokea Oktoba 7, 2023.
-
Axios: Israel imependekeza kwa HAMAS mpango mpya wa kubadilishana mateka
Jan 23, 2024 02:29Utawala haramu wa Kizayuni wa Israel umependekeza kwa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS mpango mpya wa kubadilishana mateka kupitia "usitishaji" mapigano kwa muda wa hadi siku 60 ili mateka wote waliosalia, ambao wanashikiliwa na harakati hiyo, waweze kuachiwa.
-
HAMAS: Wapalestina 500,000 wa Gaza wapo katika hatari ya kufa njaa
Jan 22, 2024 23:40Afisa mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema zaidi ya watu nusu milioni wakazi wa Ukanda wa Gaza wapo katika hatari ya kufa njaa kutokana na taathira hasi za vita vya mauaji ya kimbari vya utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina wa eneo hilo lililozingirwa.
-
HAMAS: Shambulio la Oktoba 7 ilikuwa "hatua ya lazima" dhidi ya ukaliaji ardhi kwa mabavu wa Israel
Jan 22, 2024 00:17Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema, shambulio la tarehe 7 Oktoba 2024 dhidi ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel lilikuwa "hatua ya lazima" dhidi ya ukaliaji ardhi kwa mabavu unaofanywa na utawala huo dhalimu katika maeneo ya Palestina.
-
Wazayuni washangazwa na uwezo mkubwa wa HAMAS wa kuzalisha silaha
Jan 21, 2024 23:29Utawala wa Kizayuni umelazimika kukiri kuwa umeshangazwa sana na jinsi Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS ilivyo na uwezo mkubwa wa kuzalisha silaha ndani ya Ukanda wa Ghaza ambao umezingiwa kila upande kwa miaka mingi.
-
Marekani: Israel imeshindwa kufikia lengo la vita, HAMAS ingali iko imara, ina silaha za kutosha
Jan 21, 2024 09:18Mashirika ya intelijensia ya Marekani yamesema, idadi ya vifo vya wapiganaji wa harakati ya HAMAS vilivyotokana na uvamizi unaoendelea wa Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza haifikii lengo la utawala huo la kulitokomeza kundi hilo la muqawama wa Palestina.
-
Ujumbe wa HAMAS ya Palestina waitembelea Russia
Jan 20, 2024 00:33Ujumbe wa ngazi ya juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina(HAMAS) umeitembelea Moscow, mji mkuu wa Russia.
-
Khalid Mash'al: Taifa la Palestina linataka kuwa huru na kujikomboa kutoka katika minyororo ya maghasibu
Jan 17, 2024 23:20Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) nje ya Palestina amesema kuwa taifa la Palestina linapigania uhuru, linataka kujikomboa na kuunda nchi huru mji wake mkuu ukiwa Quds Tukufu.