-
HAMAS: Muqawama utaipa Israel funzo lisilosahaulika kwa ukatili inaowafanyia Wapalestina
Jan 02, 2024 10:50Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imelaani kifo cha mateka mwengine wa Kipalestina aliyeuliwa kwenye kituo cha mahabusu cha utawala wa Kizayuni wa Israel katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu na kuahidi kuupa utawala huo funzo lisilosahaulika kutokana na ukatili wake unaoendelea kuwafanyia Wapalestina.
-
Mbali na kuua watoto wachanga, Wazayuni wanafanya uporaji pia Ghaza
Dec 23, 2023 23:09Mkuu wa Ofisi ya Upashaji Habari ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kuwa mbali na jinai zao nyingine nyingine kama za kuua watoto wachanga, wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wanafanya uporaji pia wa mali za Wapalestina wakati wanapoingia kwenye nyumba walizozivunja kwa mashambulizi ya kikatili na kinyama huko Ghaza.
-
HAMAS: Tuko tayari kwa vita vya muda mrefu na hatutaachana na Muqawama
Dec 14, 2023 04:19Osama Hamdan, Kiongozi Mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesisitiza azma thabiti ya harakati hiyo ya Muqawama wa Wapalestina yenye makao yake katika Ukanda wa Gaza ya kuendelea kupambana na utawala wa Kizayuni wa Israel, ambao umeliweka eneo hilo la pwani katika vita vya mtawalia vya mauaji ya kimbari.
-
Tunawaambiaje wale wanaolaani mapambano ya silaha ya Wapalestina?
Dec 12, 2023 06:39Hivi inafaa kweli kuwalaumu Wapalestina kwa kuendesha mapambano ya silaha dhidi ya Wazayuni Kama unaamini hivyo, basi anza kwanza kulaani mapambano ya mashujaa kama Nelson Mandela. Lakini pia si shujaa Nelson Mandela tu, bali wako wengi.
-
HAMAS: Hatutawaachia mateka wa Israel mpaka matakwa yetu yatakapotekelezwa
Dec 11, 2023 00:18Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema, kamwe haitasalimu amri kwa mashambulizi ya kinyama ya mtawalia yanayofanywa na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Gaza ili iwaachilie mateka wa utawala huo iliowakamata katika operesheni yake ya Kimbunga cha Al-Aqsa iliyotekeleza mapema mwezi Oktoba.
-
Kura ya veto ya Marekani dhidi ya azimio la Baraza la Usalama kuhusu vita vya Gaza
Dec 09, 2023 07:57Marekani, ambayo ni mwanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, imepinga azimio lililopendekezwa na UAE la kuanzisha usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza.
-
HAMAS yalaani kitendo cha askari wa Israel cha kuwakashifu Wapalestina kwa kuwavua nguo hadharani
Dec 09, 2023 02:49Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imelaani kitendo cha wanajeshi wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel cha kuwalazimisha kuvua nguo Wapalestina wapatao 100 waliowakamata; na kuwakashifu kwa kuwaweka hadharani katika barabara za Ukanda wa Gaza wakiwa wamebaki na nguo za ndani tu.
-
Hamas: Madai yasiyo na msingi ya Biden ni kielelezo cha kuporomoka kwake kimaadili
Dec 06, 2023 04:42Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetangaza kuwa, madai yasiyo na msingi ya Rais wa Marekani kuhusu operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa yanaonyesha kuporomoka kwake kimaadili.
-
Askari 60 wa Kizayuni waangamizwa katika operesheni ya HAMAS
Dec 03, 2023 07:13Makumi ya wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wameangamizwa katika operesheni ya Brigedi za Izzuddin al Qassam, Tawi la Kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu HAMAS.
-
WSJ: Mashirika ya ujasusi ya Israel yamepanga kuwaua viongozi wa HAMAS popote pale duniani
Dec 02, 2023 02:31Mashirika makuu ya ujasusi ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel yanaripotiwa kuwa yamedhamiria "kuwaua" viongozi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS duniani kote baada ya kumalizika vita vyake vya kikatili na kinyama unavyoendeleza dhidi ya Ukanda wa Gaza, ambavyo tayari vimeshaua Wapalestina wanaokaribia 16,000 hadi sasa.