-
Kuongezeka kukosolewa uungaji mkono wa Magharibi kwa utawala wa Kizayuni
Nov 16, 2023 00:41Kuendelea jinai , mauaji ya kimbari na kutokomezwa kizazi cha wananchi wa Gaza na utawala wa Kizayuni ambazo zimesababisha maelfu ya Wapalestina kuuawa shahidi na kujeruhiwa, kumepelekea kushtadi kukosolewa siasa za upendeleo za serikali za Magharibi kwa Israel.
-
Mabilionea wa Marekani kuendesha kampeni ya vyombo vya habari ili kuisafisha Israel na kuichafua HAMAS
Nov 13, 2023 22:55Bilionea mmoja mfanyabiashara nchini Marekani ameanzisha kampeni ya kuchangisha mamilioni ya dola ili kuvitumia vyombo vya habari visafishe sura chafu ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel sambamba na kuchafua haiba ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS, wakati maandamano ya kuunga mkono Palestina dhidi ya Israel yaknazidi kupamba moto ulimwenguni kote.
-
Kuadhibiwa waungaji mkono wa Palestina katika vyuo vikuu vya Marekani
Nov 12, 2023 23:17Licha ya madai ya kuheshimiwa uhuru wa kujieleza katika nchi za Magharibi ikiwemo Marekani, lakini ukweli wa mambo ni kwamba kuna mistari miekundu katika uwanja huo, likiwemo suala la kutetea kadhia ya Palestina, ambapo waungaji mkono wa taifa hilo linalodhulumiwa hukabiliwa na vikwazo vya aina mbalimbali vikiwemo vya kuadhibiwa na kufungwa jela.
-
Kuongezeka upinzani dhidi ya vitendo vya kijinai vya utawala wa Kizayuni katika nchi za Magharibi
Nov 06, 2023 23:01Mwezi mmoja ukiwa umepita tangu kujiri operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa na utawala wa Kizayuni kuanzisha mashambulizi makali ya mabomu ambayo hajawahi kushuhudiwa tena huko Ghaza, ambayo yamepelekea kuuawa shahidi na kujeruhiwa makumi ya maelfu ya Wapalestina, wengi wao wakiwa ni watoto na wanawake, mwenendo wa upinzani dhidi ya vitendo hivyo vya jinai vya Israeli, umeongezeka sana duniani ikiwa ni pamoja na nchini Marekani, ambayo ni mwitifaki mkubwa wa Tel Aviv.
-
Raisi: Vita dhidi ya Hamas ni sawa na vita dhidi ya demokrasia
Nov 05, 2023 11:05Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria nafasi ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) katika uongozi wa serikali halali katika eneo la Ukanda wa Gaza huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu na kusisitiza kuwa, vita dhidi ya kundi hilo la muqawama ni sawa na vita dhidi ya demokrasia.
-
Maangamizi ya kizazi Ukanda wa Ghaza na ubinadamu uliotoweka katika nchi za Magharibi
Nov 02, 2023 05:40Ni wakati mwingine wa kuwa nanyi wapenda wasikilizaji katika Makala ya Wiki hii na leo tutazungumzia maangamizi ya kizazi katika eneo la Ukanda wa Ghaza na kuporomoka kwa ubinadamu katika nchi za Magharibi.
-
Hamas yasema Marekani inawasaidia Wazayuni katika vita vya Ghaza
Nov 02, 2023 02:49Mmoja wa viongozi wa kundi la Wanamapambano wa Kiislamu wa Palestina Hamas amesema Marekani inaunga mkono na kuusaidia kwa hali na mali Utawala wa Kizayuni katika mapigano ya Ghaza.
-
Abdollahian na Haniya wakutana Doha na kujadili matukio ya Ukanda wa Gaza
Nov 01, 2023 01:04Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS, ambapo wamebadilishana mawazo kuhusu matukio yanayoendelea kushuhudiwa katika Ukanda wa Gaza.
-
Hatua mpya za Marekani katika fremu ya kuuunga mkono utawala wa Kizayuni wa Israel
Oct 30, 2023 08:05Tangu kuanza duru mpya ya vita kati ya utawala wa Kizayuni na makundi ya muqawama ya Palestina na operesheni ya Kimbunga ya Al-Aqsa na radiamali kali ya Wazayuni dhidi ya hatua hiyo, Marekani ikiwa mshirika wa kistratijia wa Israel imetoa himaya kubwa ya kisiasa, kidiplomasia na kijeshi kwa utawala huo ghasibu. Filihali Washington imechukua hatua mpya katika mwelekeo huu.
-
Kupasishwa azimio la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu Ghaza
Oct 28, 2023 08:39Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepasisha rasimu ya azimio lililopendekezwa na nchi za Kiarabu na kutaka kutekelezwa usitishaji vita wa kibinadamu haraka iwezekanavyo huko Ghaza.