• Abu Ubaida atangaza baadhi ya hasara za Israel katika Kimbunga cha al Aqsa

    Abu Ubaida atangaza baadhi ya hasara za Israel katika Kimbunga cha al Aqsa

    Nov 25, 2023 01:05

    Msemaji wa Brigedi za Izzuddin al-Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS), ametangaza kwamba zana na ala 335 za jeshi la Israel zimeharibiwa kabisa tangu kuanza mashambulizi ya utawala huo haramu dhidi ya watu wa Gaza na kusisitiza kuwa, utawala vamizi umelazimika kukubali suluhu na kusitisha mapigano.

  • Kiongozi wa Hizbullah akutana na maafisa waandamizi wa HAMAS Beirut

    Kiongozi wa Hizbullah akutana na maafisa waandamizi wa HAMAS Beirut

    Nov 22, 2023 23:37

    Katibu Mkuu wa Hizbullah jana Jumatano alikutana na ujumbe wa maafisa wa ngazi za juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS mjini Beirut kujadili matukio ya Gaza, huku idadi ya wananchi wa Palestina waliouawa shahidi kwenye mashambulizi ya kikatili ya Israel katika eneo hilo linalokaliwa kwa mabavu ikikaribia 15,000.

  • HAMAS yaipongeza Yemen; San'a yasema: Hatutosita kukamata meli yoyote ya Wazayuni

    HAMAS yaipongeza Yemen; San'a yasema: Hatutosita kukamata meli yoyote ya Wazayuni

    Nov 20, 2023 11:23

    Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imeipongeza Yemen na jeshi lake kwa hatua yao ya kishujaa ya kukamata meli ya utawala wa Kizayuni na kusema kuwa hatua hiyo ni mafanikio ya aina yake yaliyopatikana kutokana na damu za watu wasio na hatia zinazomwagwa na Israel huko Ghaza.

  • Brigedia Jenerali Qaani: Israel ni dhaifu kuliko utando wa buibui

    Brigedia Jenerali Qaani: Israel ni dhaifu kuliko utando wa buibui

    Nov 18, 2023 00:20

    Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema Operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa imefichua kuwa utawala haramu wa Israel ni dhaifu kuliko hata nyumba ya buibui.

  • Azimio la Baraza la Usalama kuhusu vita vya Gaza: Makubaliano ya kiwango cha chini

    Azimio la Baraza la Usalama kuhusu vita vya Gaza: Makubaliano ya kiwango cha chini

    Nov 16, 2023 23:47

    Uzembe wa Umoja wa Mataifa na hasa mkwamo katika Baraza la Usalama la umoja huo ambao una jukumu muhimu la kulinda amani na usalama wa kimataifa, kuhusu vita vya Gaza, jinai za kivita na mauaji ya kimbari ya Wapalestina yanayofanywa na utawala wa Kizayuni, umekosolewa vikali kimataifa.

  • Kuongezeka kukosolewa uungaji mkono wa Magharibi kwa utawala wa Kizayuni

    Kuongezeka kukosolewa uungaji mkono wa Magharibi kwa utawala wa Kizayuni

    Nov 16, 2023 00:41

    Kuendelea jinai , mauaji ya kimbari na kutokomezwa kizazi cha wananchi wa Gaza na utawala wa Kizayuni ambazo zimesababisha maelfu ya Wapalestina kuuawa shahidi na kujeruhiwa, kumepelekea kushtadi kukosolewa siasa za upendeleo za serikali za Magharibi kwa Israel.

  • Mabilionea wa Marekani kuendesha kampeni ya vyombo vya habari ili kuisafisha Israel na kuichafua HAMAS

    Mabilionea wa Marekani kuendesha kampeni ya vyombo vya habari ili kuisafisha Israel na kuichafua HAMAS

    Nov 13, 2023 22:55

    Bilionea mmoja mfanyabiashara nchini Marekani ameanzisha kampeni ya kuchangisha mamilioni ya dola ili kuvitumia vyombo vya habari visafishe sura chafu ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel sambamba na kuchafua haiba ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS, wakati maandamano ya kuunga mkono Palestina dhidi ya Israel yaknazidi kupamba moto ulimwenguni kote.

  • Kuadhibiwa waungaji mkono wa Palestina katika vyuo vikuu vya Marekani

    Kuadhibiwa waungaji mkono wa Palestina katika vyuo vikuu vya Marekani

    Nov 12, 2023 23:17

    Licha ya madai ya kuheshimiwa uhuru wa kujieleza katika nchi za Magharibi ikiwemo Marekani, lakini ukweli wa mambo ni kwamba kuna mistari miekundu katika uwanja huo, likiwemo suala la kutetea kadhia ya Palestina, ambapo waungaji mkono wa taifa hilo linalodhulumiwa hukabiliwa na vikwazo vya aina mbalimbali vikiwemo vya kuadhibiwa na kufungwa jela.

  • Kuongezeka  upinzani dhidi ya vitendo vya kijinai vya utawala wa Kizayuni katika nchi za Magharibi

    Kuongezeka upinzani dhidi ya vitendo vya kijinai vya utawala wa Kizayuni katika nchi za Magharibi

    Nov 06, 2023 23:01

    Mwezi mmoja ukiwa umepita tangu kujiri operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa na utawala wa Kizayuni kuanzisha mashambulizi makali ya mabomu ambayo hajawahi kushuhudiwa tena huko Ghaza, ambayo yamepelekea kuuawa shahidi na kujeruhiwa makumi ya maelfu ya Wapalestina, wengi wao wakiwa ni watoto na wanawake, mwenendo wa upinzani dhidi ya vitendo hivyo vya jinai vya Israeli, umeongezeka sana duniani ikiwa ni pamoja na nchini Marekani, ambayo ni mwitifaki mkubwa wa Tel Aviv.

  • Raisi: Vita dhidi ya Hamas ni sawa na vita dhidi ya demokrasia

    Raisi: Vita dhidi ya Hamas ni sawa na vita dhidi ya demokrasia

    Nov 05, 2023 11:05

    Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria nafasi ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) katika uongozi wa serikali halali katika eneo la Ukanda wa Gaza huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu na kusisitiza kuwa, vita dhidi ya kundi hilo la muqawama ni sawa na vita dhidi ya demokrasia.