-
Zakzaky: Mashambulizi ya kigaidi ya Israel yanapasa kulaaniwa duniani kote
Jun 16, 2025 07:08Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria (IMN), Sheikh Ibrahim Zakzaky amelaani mashambulizi ya Israel dhidi ya Iran na kuelezea hujuma hizo za utawala wa Kizayuni dhidi ya nchi huru kuwa ni kitendo cha juu zaidi cha uchokozi, kinachopaswa kulaaniwa duniani kote.
-
Mashambulio ya makombora na ndege zisizo na rubani ya Iran dhidi ya Israel, mwisho wa zama za "kushambulia na kukimbia" kwa Israel.
Jun 15, 2025 12:15Baada ya utawala wa Kizayuni kuishambulia Iran kwa ushirikiano wa Washington asubuhi ya Ijumaa, Juni 13, na kupelekea kuuawa shahidi idadi kubwa ya makamanda waandamizi wa kijeshi na wanasayansi, pamoja na raia wa kawaida, Iran, kama ilivyoahidi awali, ilianza kutoa jibu kali kwa jinai hiyo na mauaji ya kimbari Ijumaa usiku kupitia operesheni ya mashambulio ya makombora na ndege zisizo na rubani, iliyopewa jina la Ali ibn Abi Talib.
-
Israel yaendelea kukabiliwa na mvua ya makombora ya Iran; mkuu wake wa ujasusi ajiuzulu
Jun 15, 2025 03:09Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) usiku wa kuamkia leo limetekeleza wimbi jipya la mashambulizi ya makombora na ndege zisizo na rubani dhidi ya utawala wa Kizayuni, kufuatia awamu ya kwanza ya operesheni ya kulipiza kisasi ya "Ahadi ya Kweli III" Ijumaa usiku.
-
Iran yapiga shabaha 150 za Israel katika Operesheni ya Ahadi ya Kweli 3
Jun 14, 2025 07:13Afisa wa ngazi ya juu wa Jeshi la Iran amesema kwa akali shabaha 150 zimepigwa wakati wa operesheni ya kulipiza kisasi ya Jamhuri ya Kiislamu dhidi ya utawala haramu wa Israel, ikiwa ni pamoja na kambi kadhaa za kimkakati za kijeshi za utawala huo pandikizi.
-
Iran yatungua ndege 2 za kivita za Israel za F-35, yamkamata rubani
Jun 14, 2025 07:05Kikosi cha Ulinzi wa Anga cha Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kimefanikiwa kutungua na kuteketeza ndege mbili za kivita za Israel aina ya F-35, na idadi kubwa ya ndege zisizo na rubani. Iran imekuwa nchi ya kwanza duniani kuweza kutungua ndege ya kijeshi ya F-35.
-
Jenerali Hatami ateuliwa kuwa Kamanda mpya wa Majeshi ya Iran
Jun 14, 2025 07:04Brigedia Jenerali Amir Hatami ameteuliwa na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, kuwa Kamanda Mkuu mpya wa Majeshi ya Iran.
-
Tehran: Mazungumzo ya nyuklia na US 'hayana maana' baada ya uvamizi wa Israel
Jun 14, 2025 06:49Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, mazungumzo na Marekani kuhusu mpango wa nyuklia wa Tehran "hayana maana" kufuatia mashambulizi ya kinyama ya Israel, huku akiishutumu Washington kwa kuunga mkono uchokozi huo.
-
Iran: EU ikishinikiza turejeshewa vikwazo vya UN, tutajitoa NPT
Jun 12, 2025 02:53Iran imeonya kwamba, huenda ikatumia haki yake ya kisheria ya kujiondoa kwenye Mkataba wa Kuzuia Uzalishaji na Uenezaji wa Silaha za Nyuklia (NPT) ikiwa mataifa ya Ulaya yataendelea na jaribio lisilo na msingi wa kisheria la kuamilisha mchakato wa kurejeshwa vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Je, mashirikiano ya Iran na Afrika yataimarika vipi?
Jun 12, 2025 02:09Katika kikao chao na Abbas Araqchi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, mabalozi wa Senegal na Sierra Leone wamesisitiza utayari wa nchi za Kiafrika kwa ajili ya kuendeleza ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara na Iran.
-
Iran: Tutapiga vituo vya siri vya nyuklia vya Israel iwapo tutashambuliwa
Jun 10, 2025 03:03Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran (SNSC) limeonya kuwa, Jamhuri ya Kiislamu itavishambulia vituo vya siri vya nyuklia vya Israel iwapo utawala huo wa Kizayuni utafanya kitendo chochote cha uchokozi dhidi ya taifa hili.