-
Russia: Iran ina haki ya kujitetea mbele ya mashambulizi ya Marekani, Israel
Mar 13, 2026 07:36Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina haki ya kujitetea na kukabiliana na hujuma za Marekani na Israel na ametoa wito wa kusitishwa mashambulizi ya Marekani na Israel na kurejea kwenye meza ya mazungumzo.
-
IRGC yashambulia meli nyingine ya mafuta ya US Ghuba ya Uajemi
Mar 13, 2026 07:27Kikosi cha Majini cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran IRGC kimetangaza habari ya kushambulia meli nyingine ya mafuta Marekani katika Ghuba ya Uajemi.
-
Larijani: Asia Magharibi itatumbukia gizani US ikishambulia mtandao wa umeme wa Iran
Mar 13, 2026 06:59Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran ametoa onyo kali akijibu vitisho vipya vilivyotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu kushambulia giridi ya taifa ya umeme wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Waisraeli 2,700 wajeruhiwa katika mashambulizi ya kisasi ya Iran
Mar 13, 2026 06:43Ripoti ya Wizara ya Afya ya utawala wa Kizayuni wa Israel imesema Waisraeli zaidi ya 2,700 wamejeruhiwa katika mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran yaliyoanza Februari 28.
-
Rais wa Iran atangaza masharti ya kusitishwa vita vya kutwishwa vya US, Israel
Mar 12, 2026 07:21Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian ametangaza masharti kadhaa ya kuhitimisha vita vya kichokozi vilivyoanzishwa na Marekani na utawala wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu; huku tawala mbili hizo za kigaidi zikiendelea kushambulia maeneo muhimu ya kiraia kama shule, hospitali, makazi ya watu, na turathi za kihistoria za nchi hii.
-
Araghchi aonya UN: Kunyamazia kimya uvamizi wa US, Israel kutashadidisha taharuki katika eneo
Mar 12, 2026 06:53Waziri wa Mambo ya Nje ya Iran amesema katika mazungumzo yake ya simu na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres kuwa, kufumbia macho au kutochukua hatua za maana mkabala wa vitendo vya kivamizi vya Marekani na Israel dhidi ya Iran kutafungua njia ya kushadidi ukosefu wa utulivu na taharuki katika eneo.
-
Pezeshkian amhutubu Trump: Wavamizi huja na kwenda, lakini Iran itabaki
Mar 11, 2026 08:04Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amekosoa vikali vitisho vya kukaririwa vya Rais wa Marekani, Donald Trump kwamba ataisambaratisha Iran, akisiitiza kuwa, wavamizi na waharibifu mithili Trump walikuja na wakaondoka, lakini Iran imeendeelea kubakia.
-
Iravani alaani mauaji ya wanadiplomasia 4 wa Iran nchini Lebanon
Mar 11, 2026 07:48Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa ameyataja mauaji ya kigaidi ya wanadiplomasia wanne wa Jamhuri ya Kiislamu katika mji mkuu wa Lebanon, Beirut kama 'jinai ya kihaini'.
-
Msemaji wa Majeshi ya Iran: US inawatumia watu wa Asia Magharibi kama ngao
Mar 10, 2026 17:08Msemaji wa Vikosi vya Ulinzi vya Iran, Brigedia Jenerali Abolfazl Shekarchi amesema baadhi ya makamanda na wanajesh wa Marekani wanawatumia raia wa eneo la Asia Magharibi kama ngao za binadamu vitani.
-
Msemaji wa IRGC: Majibu ya Iran yamemtia kiwewe Donald Trump
Mar 10, 2026 07:44Msemaji wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amejibu upuuzi na uongo wa Rais Donald Trump wa Marekani akisema: "Rais muongo wa Marekani ametoa madai ya kumaliza nguvu ya vikosi vya jeshi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ili kujaribu kukwepa mashinikizo ya vita na kukomesha hali ya kukata tamaa wanajeshi wa Marekani katika eneo la Asia Magharibi."