-
Iran: Ni kwa manufaa ya US kulichukulia kwa uzito pendekezo letu
Jun 09, 2025 11:29Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baghaei amesema Tehran hivi karibuni itawasilisha pendekezo lake kuhusu makubaliano ya nyuklia kupitia Oman, akitoa wito kwa Washington kutopoteza fursa hii, na kulichukulia kwa uzito pendekezo la Jamhuri ya Kiislamu.
-
Iran: Vikwazo vya US dhidi ya majaji wa ICC vinakirihisha
Jun 09, 2025 02:49Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baqaei amekosoa vikali hatua ya Marekani ya kuwawekea vikwazo majaji wanne wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kutokana na uchunguzi wao juu ya uhalifu wa kivita uliofanywa na Israel huko Gaza na Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Iran, Imarati zasisitiza haja ya Waislamu kote duniani kuwa na umoja
Jun 07, 2025 07:00Rais Masoud Pezeshkian wa Iran na Kiongozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Sheikh Mohammed bin Zayed Al Nahyan wametoa wito wa umoja wa Waislamu.
-
Pezeshkian: Umoja wa mataifa ya Kiislamu ni wajibu wa kidini na kistratajia
Jun 05, 2025 06:54Rais Masoud Pezeshkian wa Iran, amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu inatazama umoja na mshikamano miongoni mwa mataifa ya Kiislamu kuwa ni wajibu wa kidini na wa kimkakati.
-
Iran: Tutaendelea kuiunga mkono Lebanon kwa hali na mali
Jun 05, 2025 06:51Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi amesisitiza utayarifu wa Jamhuri ya Kiislamu kuimarisha ushirikiano na Lebanon, alipokutana na Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah, Sheikh Naim Qassem mjini Beirut.
-
Trump na matakwa ya kupindukia kwa Iran: Je, Washington inataka kufikia makubaliano au kutwisha matakwa?
Jun 05, 2025 04:15Rais Donald Trump wa Marekani amekariri matakwa ya kupindukia mipaka ya Washington kuhusu mpango wa amani wa nyuklia wa Iran kwa ajili ya kufikiwa mapatano ya pande mbili.
-
Iran: Ripoti ya IAEA imetolewa kwa mujibu wa matashi ya kisiasa
Jun 01, 2025 07:19Iran imetoa wito kwa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) kuakisi hali halisi kuhusu mpango wa amani wa nishati ya nyuklia wa Jamhuri ya Kiislamu na kujiepusha na matashi ya kisiasa kwenye ufuatiliaji wake wa shughuli za nyuklia za nchi hii.
-
Iran: Hatutakubali utwishaji wa Magharibi; tutaendelea kurutubisha urani
May 31, 2025 11:36Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi amepinga vikali mashinikizo ya nchi za Magharibi ya kuitaka Jamhuri ya Kiislamu iache kurutubisha madini ya urani, akiyataja mashinikizo hayo kuwa ni juhudi za kulitwisha taifa la Iran matakwa yao.
-
Maandamano ya kuwaunga mkono Wagaza yafanyika Iran, Yemen
May 31, 2025 02:23Maelfu ya watu walimiminika barabarani na mitaani katika miji yote ya Iran baada ya Swala ya Ijumaa kushiriki maandamano ya kitaifa ya "Ijumaa ya Ghadhabu", wakitangaza uungaji mkono wao usioyumba kwa Wapalestina wa Gaza, na kulaani mauaji ya kimbari ya Israel katika eneo hilo lililozingirwa.
-
Onyo la Trump kwa Netanyahu baada ya kutishia kuishambulia Iran
May 29, 2025 06:17Rais wa Marekani, Donald Trump ameripotiwa kuvutana na Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu katika mazungumzo yao ya simu, baada ya nduli huyo wa vita wa utawala wa Kizayuni kutishia kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran, na hivyo kuhatarisha mazungumzo ya kidiplomasia yanayoendelea kati ya Tehran na Washington.