-
Araqchi: Wanachama wa JCPOA hawaitambui Marekani kama mshirika wao
Sep 01, 2020 23:01Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayehusika na masuala ya kisiasa amesema nchi zilizosalia katika makubaliano ya nyuklia ya Iran haziitambui Marekani kuwa mwanachama au mshirika wa mapatano hayo ya kimataifa.
-
Rais Rouhani: Mitazamo ya Iran na Niger katika masuala ya kimataifa inafanana
Sep 01, 2020 03:18Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika mazungumzo yake ya simu na mwenzake wa Niger kuwa nchi mbili hizi zimekuwa na ushirikiano amilifu na mitazamo inayofanana katika masuala na taasisi za kimataifa na kubainisha kuwa, nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika bila shaka itakabiliana na uchukuaji wa maamuzi ya upande mmoja wa Marekani katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Iran: Marekani haina haki wala kibali cha kutumia "Snapnack Mechanism"
Sep 01, 2020 03:16Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema Marekani haina haki, idhini wala kibali cha kutumia utaratibu wa kurejesha upya vikwazo ilivyokuwa imewekewa Iran huko nyuma na UN unaofahamika kama 'Snapback Mechanism."
-
Iran: Magaidi wa MKO wanapewa hifadhi na US na EU licha ya kuua maelfu ya Wairani
Aug 30, 2020 06:32Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesema nchi za Ulaya na Marekani zinawapa hifadhi wanachama wa kundi la kigaidi la Munafikin (MKO) licha ya genge hilo kuua kikatili maelfu ya Wairani.
-
Umbumbumbu wa Marekani katika masuala ya sheria, wameshindwa na sasa wanatoa vitisho
Aug 29, 2020 05:48Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran amekosoa jitihada zinazofanywa na Marekani kwa ajili ya kurejesha vikwazo vya kimataifa dhidi ya Iran kuanzia tarehe 20 Oktoba mwaka huu wa 2020 na kusema: Viongozi wa serikali ya Marekani ni mbumbumbu katika masuala ya sheria na hawajui lolote kuhusiana na tendaji wa Umoja wa Mataifa.
-
Zarif aipa Marekani somo la sheria baaada ya kubwagwa mara 3 katika UNSC
Aug 29, 2020 03:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameeleza kushangazwa kwake na kitendo cha Marekani cha kutishia tena kumwekea vikwazo mtu au taasisi yoyote inayoshirikiana na Iran, licha ya kupigwa mweleka mara tatu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Ufaransa yakaribisha mapatano kati ya Iran na wakala wa IAEA
Aug 28, 2020 03:19Ufaransa imekaribisha uamuzi wa Iran wa kuuruhusu Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA kukagua maeneo mawili ya miradi yake ya nyuklia na kusema hiyo ni hatua kuelekea upande sahihi.
-
Harris: Sera za Trump dhidi ya Iran zimeifanya Marekani itengwe zaidi
Aug 27, 2020 21:53Makamu wa Joe Biden, mgombea wa chama cha Democratic katika uchaguzi wa rais wa mwezi Novemba mwaka huu nchini Marekani amesema sera za Rais Donald Trump dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zimeifanya nchi hiyo itengwe zaidi wakati huu kuliko wakati wowote ule.
-
Taarifa ya pamoja ya Tehran; nia njema ya Iran na matarajio ya Tehran kwa IAEA
Aug 27, 2020 05:12Baada ya mazungumzo ya kina ya siku mbili ya Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) mjini Tehran, Iran na wakala huo wamefikia makubaliano kuhusu namna ya kutatua masuala mbalimbali kwa nia njema.
-
Grossi: Safari yangu Iran ilikuwa ya mafanikio
Aug 27, 2020 01:59Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) ametangaza kuwa, tarehe iliyoafikiwa kati ya wakala huo na Iran kwa ajili ya IAEA kufanya uhakiki ipo karibu sana.