-
Iraq: OIC itakutana kujadili kuvunjiwa heshima tena Qur'ani katika nchi za Ulaya
Jul 23, 2023 13:40Wizara ya Mambo ya Nje ya Iraq imetangaza kuwa, Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) inapanga kufanya kikao cha dharura ili kujadili vitendo vya mara kwa mara vya kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu barani Ulaya.
-
Kuchomwa moto Qur'ani Tukufu, Waziri wa Mawasiliano wa Iraq ayapiga marufuku mashirika ya Sweden
Jul 21, 2023 11:08Waziri wa Mawasiliano wa Iraq ameyapiga marufuku mashirika yote ya Sweden kufanya kazi nchini humo ikiwa ni kujibu kitendo cha nchi hiyo ya Ulaya Magharibi cha kuruhusu kuvunjiewa heshima tena Qur'ani Tukufu na bendera ya Iraq.
-
Kuchomwa moto Qur'ani Tukufu, balozi wa Sweden atimuliwa Iraq
Jul 21, 2023 02:40Serikali ya Iraq imemfukuza balozi wa Sweden mjini Baghdad kulalamikia serikali ya nchi hiyo ya Ulaya Magharibi ya kuruhusu kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu.
-
Kushambulia ubalozi wa Uswidi jijini Baghdad; matokeo ya kuvunjiwa heshima matukufu ya Kiislamu
Jul 20, 2023 12:18Waandamanaji wa Iraq waliokuwa na hasira wameushambulia ubalozi wa Uswidi mjini Baghdad kujibu udhalilishaji uliopangwa dhidi ya Qur'ani Tukufu katika nchi hiyo ya Ulaya.
-
Kuvunjiwa heshima Qurani; Wairaq waushambulia ubalozi wa Sweden
Jul 20, 2023 07:33Wananchi wa Iraq waliokuwa na ghadhabu wameuvamia ubalozi wa Sweden mjini Baghdad na kuchoma moto sehemu moja ya ofisi za ubalozi huo, kulalamikia kibali cha pili kilichotolewa na serikali ya Stockholm cha kuruhusu kuvunjiwa heshima Qurani Tukufu katika nchi hiyo ya Ulaya.
-
Jumatatu, 17 Julai, 2023
Jul 17, 2023 03:02Leo ni Jumatatu tarehe 28 Mfunguo Tatu, Dhulhija 1444 Hijria, sawa na tarehe 17 Julai mwaka 2023 .
-
Wairaqi walaani njama za Marekani za kutaka kuwaua viongozi wa muqawama
Jul 15, 2023 06:48Wananchi wa Iraq wamefanya maandamano katika mji mkuu Baghdad, kupinga na kulaani uingiliaji wa Marekani katika masuala ya ndani ya nchi hiyo, na vile vile njama za Washington za kutaka kuwaua kigaidi viongozi wa kambi ya muqawama nchini humo.
-
Viongozi 6 hatari wa Daesh watiwa nguvuni Iraq
Jul 04, 2023 04:22Idara ya Intelijinsia ya Iraq imetangaza kuwatia mbaroni watu sita wanaotajwa kuwa magaidi hatari sana wa kundi la Daesh (ISIS) katika mkoa wa Nineveh nchini humo.
-
Ayatullah Sistani ataka Umoja wa Mataifa uzuie kukaririwa vitendo vya kuvunjia heshima Qur'ani
Jun 30, 2023 07:41Ayatullah Sayyid Ali Sistani, Marjaa wa Waislamu wa Kishia ameutaka Umoja wa Mataifa kuchukua hatua za kuzuia kukaririwa vitendo vya kuvunjiwa heshima kitabu cha Waislamu cha Qur'ani Tukufu.
-
Al Hashdu Shaabi ya Iraq yawatia mbaroni viongozi 3 wa Daesh
Jun 24, 2023 11:18Harakati ya wapiganaji wa kujitolea ya wananchi wa Iraq maarufu kama Al Hashdu al Shaabi (PMU) imetangaza kuwatia mbaroni viongozi watatu wa kundi la kigaidi la Daesh (ISIS) katika mkoa wa Kirkuk nchini humo.