-
Mwaka wa tisa wa kuasisiwa Hashd al Shaabi, sisitizo la viongozi wa Iraq la kuimarishwa harakati hiyo ya ukombozi
Jun 17, 2023 08:16Rais Abdul Latif Rashid wa Iraq pamoja na Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Mohammed Shayya’ Sabbar al-Sudani wametuma ujumbe mbalimbali kwa mnasaba wa kumbukumbu ya mwaka wa tisa wa kuasisiwa harakati ya ukombozi ya wananchi wa Iraq maarufu kwa jina la Hashd al Shaabi na wametilia mkazo wajibu wa kuimarishwa zaidi harakati hiyo.
-
Iraq yavunja mtandao wa mabaki ya ISIS mkoani Al-Anbar
Jun 06, 2023 05:32Vyombo vya usalama nchini Iraq vimefanikiwa kusambaratisha mtandao wa mabaki ya wanachama wa kundi la kigaidi la ISIS katika mkoa wa Al-Anbar, wa magharibi mwa nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Iraq: Jordan imegeuzwa maficho ya Waba'athi zaidi ya elfu tano waliotoroka nchi
May 29, 2023 01:32Kiongozi mmoja wa Muungano wa al-Fat'h ya Iraq amesema, Jordan sasa hivi imegeuzwa maficho ya Maba'athi zaidi ya elfu tano waliotoroka nchi.
-
"Waliomzatiti kwa silaha Saddam wanatiwa kiwewe na uwezo wa kiulinzi wa Iran"
May 27, 2023 01:48Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amejibu kile kilichotajwa kuwa 'wasiwasi' wa nchi za Magharibi juu ya ustawi na mafanikio ya Jamhuri ya Kiislamu katika uga wa ulinzi na kusisitiza kuwa, madola hayo yanayotiwa kiwewe na uwezo mkubwa wa kiulinzi wa Iran ndiyo yaliyomshajiisha na kumzatiti kwa silaha dikteta wa zamani wa Iraq, Saddam Hussein ili awashambulie Wairani.
-
Nujabaa ya Iraq: Tutapambana mpaka tuhakikishe hata askari mmoja wa Marekani habakii Iraq
May 02, 2023 02:14Msemaji wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Nujabaa amesisitiza kuwa vita dhidi ya wavamizi wa Kimarekani vitaendelea hadi itakapohakikishwa hakuna hata mwanajeshi mmoja wa Marekani aliyesalia katika ardhi ya Iraq.
-
Rais Raisi: Azma ya viongozi wa Iran na Iraq ni kustawisha uhusiano baina ya pande mbili
Apr 29, 2023 12:10Rais Ebrahim Raisi amesema: azma ya viongozi wa nchi mbili za Iran na Iraq ni kustawisha uhusiano baina ya pande mbili.
-
Alkhamisi tarehe 13 Aprili 2023
Apr 13, 2023 02:38Leo ni tarehe 22 mwezi Mtukufu wa Ramadhani 1444 Hijria inayosadifiana na tarehe 13 Aprili 2023.
-
Chanzo cha usalama Iraq kimeonya: Daesh wanarejeshwa al Anbar chini ya usimamizi wa Marekani
Apr 10, 2023 07:52Chanzo cha ngazi za juu cha usalama katika mkoa wa al Anbar nchini Iraq kimetangaza kwamba maafisa wa serikali ya nchi hiyo wanapaswa kuwa na wasiwasi wa kujirudia hali ya mwaka 2014 magharibi mwa mkoa huo na kurudi kwa wapiganaji wa kundi la Daesh (ISIS).
-
Wairaqi zaidi ya milioni moja wametoweka na hawajulikani waliko
Apr 05, 2023 11:25Umoja wa Mataifa umetangaza katika ripoti yake kuwa, zaidi ya watu milioni moja wametoweka nchini Iraq na hawajulikani waliko; katika kipindi cha miaka hamsini iliyopita, ikiwa ni pamoja na enzi za udikteta wa Saddam Hussein, za uvamizi wa Iraq ulioongozwa na Marekani, na za kuibuka kwa kundi la kigaidi na ukufurishaji la DAESH (ISIS).
-
Seneti ya Marekani yafuta kibali cha Pentagon kuhusu oparesheni za kijeshi Iraq
Apr 01, 2023 03:13Seneti ya Marekani Jumatano wiki hii ilihitimisha kibali ilichokuwa imekitoa kwa Wizara ya Ulinzi ya nchi hiyo (Pentagon) mwaka 1999 na 2002 kwa ajili ya vita huko Iraq na imepasisha uamuzi wa kufutwa kibali cha Pentagon kwa ajili ya kutekeleza oparesheni za kijeshi huko Iraq bila ya kuhitaji idhini ya Kongresi.