-
'Kulifufua genge la kigaidi la Daesh ndilo lengo la kiistratijia la Marekani'
Feb 26, 2021 02:50Mbunge wa zamani wa Lebanon amesisitiza kuwa, suala la kulifufua genge la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) ndilo lengo la kiistratijia la Marekani kwani inaamini kwamba genge hilo ni turufu ya kufanikisha malengo yake haramu katika eneo hili.
-
Jumuiya ya Maulamaa Iraq: Mossad inaongoza kambi za magaidi wa Daesh huko Syria
Feb 24, 2021 02:42Mkuu wa Jumuiya ya Maulamaa wa Kiislamu katika mkoa wa Diyala huko Iraq amesema kuwa shirika la ujasusi la utawala wa Kizayuni wa Israel (Mossad) linasimamia kambi mbalimbali za magaidi wa kundi la ukufurishaji la Daesh huko Syria.
-
Umoja wa Maulamaa wa Kiislamu: Sehemu kubwa ya Madaesh wa kujiripua wameingia Iraq kutokea Syria
Feb 23, 2021 02:44Mkuu wa Umoja wa Maulamaa wa Kiislamu katika mkoa wa Diyala nchini Iraq amesema kuwa, sehemu kubwa ya magaidi wa Daesh (ISIS) wa kujiripua kwa mabomu wameingia nchini Iraq wakitokea Syria.
-
Ongezeko la wanajeshi wa NATO nchini Iraq, juhudi za kujaza nafasi ya Marekani
Feb 21, 2021 02:39Majeshi ya nchi za Magharibi yalipelekwa kwa wingi nchini Iraq baada ya Marekani kuivamia ardhi ya nchi hiyo mwaka 2003 na bado yanaendelea kuwepo nchini humo.
-
Mfadhili mkuu wa kifedha wa Daesh atiwa mbaroni mkoani Diyala, Iraq
Feb 20, 2021 08:05Idara ya Intelijinsia ya Jeshi la Iraq imetangaza habari ya kutiwa mbaroni mfadhili mkuu wa kifedha wa kundi la Daesh mkoani Diyala mashariki mwa nchi hiyo.
-
Wabunge wa Iraq wataka uingiliaji wa Marekani katika masuala ya nchi hiyo ukomeshwe
Feb 19, 2021 14:03Wabunge kadhaa wa Iraq wametoa indhari kuhusu uingiliaji wa Marekani hasa katika kadhia ya uchaguzi ujao wa bunge na katika masuala ya kijeshi na kiusalama ya nchi hiyo.
-
Iraq yaitahadharisha Uturuki kuhusu mashambulizi dhidi ya Sinjar
Feb 16, 2021 02:41Msemaji wa kikosi cha oparesheni za pamoja cha Iraq ameitahadharisha Uturuki kuhusu oparesheni ya jeshi katika eneo la Sinjar mkoani Nainawa huko Iraq na kueleza kuwa, Baghdad itachukua hatua zote za lazima iwapo itakabiliwa na shambulizi au uvamizi wowote wa nchi ajinabi.
-
Ammar al Hakim atilia mkazo ulazima wa askari wa Marekani kuondoka Iraq
Feb 13, 2021 02:55Kiongozi wa Harakati ya Hekima ya Kitaifa ya Iraq amesisitiza kuhusu ulazima wa Marekani kubadilisha mwenendo wake katika Asia Magharibi na askari wa nchi hiyo kuondoka katika eneo hilo.
-
Hashdu Shaabi kubuni mipango mipya ya kuwafukuza askari wa US Iraq
Feb 10, 2021 02:30Harakati ya kujitolea wananchi ya Hashdu Shaabi ya Iraq imeonya kuwa, iwapo wanajeshi vamizi wa Marekani hawataheshimu uamuzi wa bunge la nchi hiyo wa kuwataka waondoke, basi itazindua mipango mipya ya kuwatimua askari hao katika nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Tishio la kurejea upya kundi la Daesh huko Iraq
Feb 09, 2021 02:28Harakati za kundi la Daesh na pia mapigano kati ya kundi la Hashdu Shaabi la Iraq na masalia ya kundi hilo la kigaidi yameongezeka nchini humo katika miezi ya karibuni.