-
Wanazuoni wa dini zote duniani watakiwa waungane kupinga vikwazo vya kidhalimu vya Marekani dhidi ya Iran
Apr 16, 2020 14:49Mkuu wa Baraza la Maulamaa wa Kisuni nchini Iraq amewatolea mwito wanazuoni wa dini na madhehebu zote duniani kuchukua msimamo mmoja wa kupinga vikwazo vya kidhalimu vya Marekani dhidi ya wananchi wa Iran.
-
Makumi ya askari wa Marekani walioko Iraq wakumbwa na corona
Apr 11, 2020 15:04Makumi ya askari wa jeshi vamizi la Marekani nchini Iraq wameambukizwa ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwa na virusi vya corona.
-
Waziri Mkuu mteule wa Iraq: Mamlaka ya kitaifa ya kujitawala ni mstari mwekundu kwangu
Apr 11, 2020 04:15Waziri Mkuu mpya mteule wa Iraq Mustafa al-Kadhimi amesema, mafanikio ya nchi hiyo katika mahusiano ya kimataifa yatapatikana kwa "kuheshimiana na kushirikiana".
-
Kujiuzulu al-Zurfi na kufunguliwa njia ya kupatikana mshikamano wa kisiasa ndani ya Iraq
Apr 10, 2020 08:24Baada ya kujiuzulu Adnan al-Zurfi, Rais Barham Salih wa Iraq amemteua Mustafa al-Kadhimi kuwa waziri mkuu mpya na kumpa jukumu la kuunda serikali.
-
Kamisheni ya Usalama ya Bunge la Iraq yaonya kuhusu kupuuzwa uwepo wa Marekani nchini humo
Apr 08, 2020 13:06Mkuu wa Kamisheni ya Usalama na Ulinzi ya Bunge la Iraq ametahadharisha kuhusiana na kuendelea kuwepo majeshi ya Marekani katika kituo cha Ain al-Assad katika mkoa wa al-Anbar na al-Harir katika eneo lenye Mamlaka ya Ndani la Kurdestan.
-
Vuta nikuvute juu ya uwaziri mkuu wa al-Zurfi huku makundi ya Kiiraqi yakikaribia kufikia mwafaka
Apr 08, 2020 07:46Kufuatia upinzani mkali wa makundi ya Kishia kwa pendekezo la kumfanya Adnan al-Zurfi waziri mkuu mpya wa Iraq, waungaji mkono wa waziri mkuu huyo mteule aliyepewa jukumu la kuunda serikali wameyumba kimsimamo na hivi sasa makundi ya kisiasa nchini humo yanakaribia kufikia mwafaka wa kumpendekeza shakhsia mwingine mpya wa kushika wadhifa huo.
-
Kaburi jengine la halaiki lagunduliwa katika mkoa wa al-Anbar, Iraq
Apr 06, 2020 08:05Vikosi vya usalama vya Iraq vimegundua kaburi la halaiki lenye maiti za askari wa usalama na raia waliouawa katika mkoa wa al-Anbar magharibi mwa nchi hiyo.
-
Harakati ya Asa'ib Ahl al-Haq yatahadharisha juu ya malengo ya Marekani ya kubakia kwa muda mrefu nchini Iraq
Apr 06, 2020 02:33Mjumbe wa Ofisi ya Kisiasa wa Harakati ya Asa'ib Ahl al-Haq ya nchini Iraq ametahadharisha juu ya mipango ya Marekani ya kutaka kubakia kwa muda mrefu nchini humo.
-
Uafriti wa Trump wa kuanzisha chokochoko na mivutano katika eneo kwa kuzusha tuhuma dhidi ya Iran
Apr 03, 2020 06:57Licha ya hali ya dharura na isiyo ya kawaida iliyopo kimataifa kutokana na mripuko wa janga la corona lililoikumba dunia nzima, Marekani ingali inaendelea kufuata muelekeo wa utumizi wa nguvu za kijeshi na kushikilia kuchukua hatua za kijeshi katika siasa zake za nje.
-
Mjumbe wa kamati ya ulinzi na usalama Iraq: Maafisa wa Marekani walifanya vikao na Maba'ath
Apr 03, 2020 03:00Mjumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya bunge la Iraq amefichua kuwa, baadhi ya maafisa wa Marekani walioko katika nchi jirani na Iraq, walifanya vikao kadhaa na viongozi wa chama kilichopigwa marufuku cha Ba'ath.