-
Hashdu Shaabi: Marekani iondoke Iraq kwa khiari badala ya kusubiri kutimuliwa
Jan 25, 2020 07:41Harakati ya kujitolea wananchi ya Hashdu Shaabi ya Iraq imemtaka Rais Donald Trump kuwaondoa wanajeshi wa Marekani katika nchi hiyo ya Kiarabu kwa khiari badala ya kusubiri watimuliwe kwa nguvu.
-
Idadi ya askari wa Marekani waliojeruhiwa katika jibu la Iran 'yaongezeka'
Jan 25, 2020 07:34Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) imesema makumi ya askari wa nchi hiyo walijeruhiwa na kupatwa na matatizo ya kisaikolojia kufuatia shambulizi la makombora la Iran dhidi ya kambi mbili za kijeshi za nchi hiyo huko Iraq mapema mwezi huu, licha ya utawala wa Washington hapo awali kudai kuwa hakuna askari wake hata mmoja aliyeuawa au kujeruhiwa katika majibu hayo makali ya ulipizaji kisasi yaliyotolewa na Iran.
-
Mamilioni ya Wairaqi waandamana wakitaka kuondoka wanajeshi vamizi wa Marekani nchini kwao
Jan 24, 2020 17:00Mamilioni ya wananchi wa Iraq leo Ijumaa wameandamana katika mji mkuu wa nchi hiyo Baghdad wakitaka kuondoka nchini humo wanajeshi wa Marekani kufuatia shambulio kubwa la kigaidi lililofanywa na Marekani hivi karibuni nchini humo.
-
Iraq yasubiri kushuhudia tukio la kihistoria; Mapinduzi ya Ishiri ya pili
Jan 24, 2020 08:15Huku Wairaki wakiwa wanasubiri kushuhudia maandamano makubwa ya mamilioni ya watu dhidi ya uwepo wa kijeshi wa Wamarekani katika ardhi ya nchi hiyo, makundi mbalimbali ya Wairaki wanayataja maandamano hayo kuwa 'Mapinduzi ya Ishirini' ya pili.
-
Ulinzi mkali Iraq sambamba na kuanza maandamano ya milioni ya watu ya kuifukuza Marekani
Jan 24, 2020 08:01Duru za usalama za Iraq zimetangaza habari ya kuwekwa ulinzi mkali katika kona zote za nchi hiyo ya Kiarabu hasahasa Baghdad kufuatia kuanza maandamano ya milioni ya watu ya kushinikiza kufukuzwa wanajeshi wa Marekani nchini humo.
-
Mbunge wa Iraq: Maandamano ya Ijumaa ni kura ya maoni ya kuondoa askari wa Marekani
Jan 23, 2020 11:50Mbunge wa Muungano wa Al Fath katika Bunge la Iraq amesema maandamano ya kesho Ijumaa nchini Iraq ni sawa na kura ya maoni ya wananchi wanaopinga kuwepo wanajeshi wa Marekani katika nchi hiyo.
-
Rais wa Iraq: Kutaka majeshi ya kigeni yaondoke kumetokana na kuvunjwa heshima ya mamlaka ya kujitawala
Jan 23, 2020 07:41Rais Barham Salih wa Iraq amesema: Miito ya kutaka majeshi ya kigeni (Marekani) yaondoke Iraq ni jibu kwa kitendo cha kuvunjia heshima haki ya kujitawala ya nchi hiyo.
-
Shambulizi la maroketi lajiri karibu na ubalozi wa Marekani nchini Iraq
Jan 21, 2020 07:35Eneo lenye ulinzi mkali la Green Zone karibu na ubalozi wa Marekani katika mji mkuu wa Iraq, Baghdad limeshambuliwa kwa maroketi usiku wa kuamkia leo.
-
Mohammed Tawfiq Allawi, ateuliwa kuwa waziri mkuu mpya wa Iraq
Jan 21, 2020 03:50Duru za habari nchini Iraq zimetangaza kuwa, aliyekuwa waziri wa Mawasiliano, Mohammed Tawfiq Allawi ameteuliwa kuwa waziri mkuu mpya wa nchi hiyo.
-
Iraq: Hatua ya Marekani ya kujiondoa JCPOA, ndio chanzo cha mzozo Asia Magharibi
Jan 19, 2020 04:34Wizara ya Mambo ya Nje ya Iraq imesema kuwa hatua ya Marekani ya kujiondoa kwenye mapatano ya nyuklia mashuhuri kama JCPOA ndio sababu kuu ya ongezeko la mzozo wa hivi karibuni katika eneo la Asia Magharibi.