-
Jeshi la Iraq laamuru kutiwa mbaroni wahusika wote wa uharibifu kwenye maandamano nchini humo
Nov 08, 2019 08:12Msemaji wa Kamanda wa Majeshi ya Iraq ametoa amri yenye lengo la kukabiliana na wahusika wa uharibifu katika mitaa ya nchi hiyo.
-
Juhudi za Ulaya za kujipapatua kutoka kwenye kinamasi cha shari za "Madaesh" wake
Nov 06, 2019 08:51Nchi kubwa za barani Ulaya kama vile Uingereza na Ufaransa zina mchango mkubwa wa kuundwa na kupata nguvu magenge mbalimbali ya kigaidi kama vile Daesh (ISIS) na lengo lao kubwa lilikuwa ni kuwatumia magaidi hao kuipindua serikali halali ya Syria. Hata hivyo nchi hizo zimefeli vibaya.
-
Marekani na Israel zachochea na kuunga mkono machafuko ya Iraq
Nov 06, 2019 08:05Rais wa Marekani na Waziri wa Mambo ya Nje wa utawala wa Kizayuni wa Israel wameeleza kufurahishwa na machafuko ya Iraq na kusema wanaunga mkono hali hiyo.
-
Pande tatu za Marekani, Israel na Imarati sababu ya kushadidi machafuko Iraq
Nov 04, 2019 12:01Katibu Mkuu wa Harakati ya Asa'ib Ahlul Haq ya nchini Iraq amesema kuwa pande tatu za Marekani, Imarati na utawala wa Kizayuni zimeazimia kushadidisha machafuko na mapigano huko Iraq.
-
Harakati ya Hashdu sh-Sha'abi yatangaza kuwaunga mkono waandamanaji Iraq
Nov 01, 2019 12:59Harakati ya Wananchi ya Hashdu sh-Sha'abi ya nchi Iraq imetangaza kuwa, haiingilii masuala ya kisiasa nchini humo lakini inaunga mkono matakwa halali ya wananchi kupitia maandamano ya amani.
-
Magaidi walioua watu katika maandamano ya Iraq watiwa nguvuni
Oct 31, 2019 10:34Kamanda wa Operesheni ya Baghdad amesema kuwa magaidi waliowalenga na kuua raia wanaoandamana nchini humo wametiwa nguvuni.
-
Kiongozi Muadhamu: Watu wa Iraq, Lebanon wafuatilie matakwa yao ya haki kwa njia za kisheria
Oct 30, 2019 12:02Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria njama za maadui za kuvuruga usalama katika baadhi ya nchi za eneo na kusema: "Wanaojali Iraq na Lebanon wafahamu kuwa, kipaumbele chao kinapaswa kuwa kuondoa hali ya ukosefu wa usalama na wananchi wa nchi hizo nao wafahamu kuwa, matakwa yao ya haki yanaweza tu kukidhiwa katika fremu ya mfumo wa kisheria."
-
Mousavi: Iraq na Syria ziliisambaratisha kitambo ISIS kwa msaada wa Iran
Oct 28, 2019 12:21Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS) lilisambaratishwa na Iraq na Syria muda mrefu umepita, kwa msaada wa kilojistiki wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Muosavi: Iran inafuatilia kwa makini matukio ya Iraq
Oct 27, 2019 07:32Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameeleza kusikitishwa kwake na yanayojiri katika nchi jirani ya Iraq ambayo yamepelekea kuuawa na kujeruhiwa makumi ya watu na kuharibiwa mali ya umma na kusema: Tehran inafuatilia kwa makini yanayojiri nchini humo.
-
Iraq yasema maafisa wa usalama hawajatumia silaha dhidi ya waandamanaji
Oct 27, 2019 02:38Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Iraq amesema vikosi vya usalama nchini humo havijatumia silaha dhidi ya waandamanaji katika maandamano ya hivi karibuni nchini humo.